Mtoto Samuel Nkya na chini ni kamati ya kuandaa safari yake ya matiabu India. Toka shoto ni Athumani Hamisi, Baba yake Mzee Nkya, Mwenyekiti wa kamati David Sawe na Balozi wa ZainVyombo vya habari vya ITV,Guardian,TSN na Blog ya Michuzi vitakuwepo Airport saa 6:00 ili kupokea neno la shukurani na kuagana na mwanetu.
Aidha pamoja na salaam hiyo, ninaungana nanyi kumwobea mwenzetu Athumani Hamisi aendelee kupona na kupata afya njema.
Narejea kuwashukuru sana kwa kazi kubwa mliyoifanya.Nawiwa kuwaomba radhi kwa usumbufu au vikwazo vyovyote katika harakati zote za kukusanya misaada ya mtoto huyu. Mimi kama mwanadamu mwingine yeyote sikamiliki.
Nitaendelea kuwasiliana nanyi moja kwa moja kutoka hospitali ya Workhardt Mumbai kuwapa taarifa za muhimu
Nawatakia afya njema na kila la heri siku zote..
Emanuel Nkya
Safarini Mumbai
Nawatakia afya njema na kila la heri siku zote..
Emanuel Nkya
Safarini Mumbai
Habari kamili ya mtoto Samuel inapatikana kwa kubofya hapa


Nilifikiri wa kwanza kushoto ni Rashid - au labda kabadili jina na kuitwa Athumani Khamis...
ReplyDeleteKWAKO KAKA MICHUZI, HABARI YA MTOTO SAMUEL NILIIONAGS HUMU, INASIKITISHA ILA SIKUIFUATILIA ZAIDI..LEO KUKUTA HABARI YA SAFARI YA MUMBAI,KWAKWELI IMENIGUSA SANA,SINA LA KUSEMA ILA KWA UFUPI NASEMA..
ReplyDeleteMUHIDIN ISSA MICHUZI, MWENYEZI MUNGU AKULIPIE SAWASAWA NA MATENDO YAKO,UBINADAMU MLIOMFANYIA HUYU MTOTO, MWENYEWE MUNGU NDO ATAKULIPA/ATAKULIPENI.
MUNGU MBARIKI MTOTO SAMUEL, MATIBABU YAENDE SALAMA NA ARUDI TUMUONE TENA KWENYE HII BLOG.
Mdau,
Scandinavia.
Inshallah Mungu amwongeze katika katibabu yake kwa uwezo wa Allah yeye ndio mweza wa kila kitu tuzidi kumwombea.
ReplyDeleteKatochi