HAYATI NDALIMA YUSUPH NZARO

Kwa masikitiko makubwa Familia ya Mohamed Nzaro na Balozi Eva Nzaro inatangaza kifo cha mtoto wao Ndalima Yusuph Nzaro kilichotokea jana Alhamisi Katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Michigan mjini Ann Arbor ambapo alikuwa amekimbizwa kutibiwa baada ya ajali ya gari iliyotokea usiku wa kuamkia Jumanne ya Oktoba 14, 2008.

Gari alilokuwa akiendesha marehemu liligongwa na gari nyingine wakati likisubiri taa za kuongozea magari.

Mipango ya kuusafirisha mwili wa marehemu nyumbani Tanzania kwa mazishi inaendelea. Vile vile, utoaji wa heshima za mwisho mjini Detroit unatarajiwa kufanyika siku ya Jumamosi tarehe 18 Oktoba, 2008. Muda rasmi utatangazwa baada ya maandalizi kukamilika.

Familia inapenda kutumia nafasi hii kuwashukuru na kuwaomba msaada wenu wa hali na mali katika kufanikisha safari hii ya mwisho ya kijana wao mpendwa Ndalima.

Michango kwa ajili ya msiba huu inaweza kupelekwa moja kwa moja kwenya akaunti maalum ifuatayo:

Bank Of America:
A/C Name: Mboja Nzaro (Dada wa Marehemu)
Routing No. 072000805
A/C No. 5407722411

Mawasiliano zaidi Kuhusu habari za msiba huu wasiliana na wafuatao:
Anna Royal Mfinanga 248-778- 6395
Abdul Kufakunoga 248-515- 5509
Salum Ndolanga 248-796-1267
Philemon Mnzava 248-417-5015
Leo The Saint 614-426-3422

Msiba huu kwa Detroit unafanyika nyumbani kwa binamu yake Ayubu Mfinanga.
Anuani ya Kwa Ayub:
22255 Hessel Detroit,
MI 48219
Tutaendelea kuwahabarisha kwa kadiri mipango inavyoendelea.
Asanteni kwa sala zenu, ushirikiano wenu na misaada yenu.
FAMILIA YA NZARO
--------------------------------------------------
KWA NIABA YA WADAU WOTE GLOBU HII YA JAMII INATOA POLE KWA FAMILIA YA MAREHEMU KWA MSIBA HUU MZITO AMBAO UMEGUSA HISIA ZETU SOTE NA KUTUTIA SIMANZI ISIVYOELEZEKA.
MUNGU AMLAZE MAHALA PEMA PEPONI NDUGU YETU NDALIMA
AMIN

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 46 mpaka sasa

  1. NATOA POLE NA SALA ZANGU MUNGU AWAFARIJI KATIKA KIPINDI HIKI KIGUMU CHA MOJONZI FAMILIA YA MOHAMED NZARO PAMOJA NA NDG, JAMAA NA MARAFIKI,
    Mdau

    ReplyDelete
  2. Mungu aiweke mahali pema peponi roho ya Ndalima.Poleni sana wafiwa.

    ReplyDelete
  3. RIP Yusuf.

    ReplyDelete
  4. Ndali you will always be remembered go in peace brother and rest in peace. To your son,parents,Da Mboja,Iddi,Mwamvita may almighty god give you strength and courage.

    ReplyDelete
  5. NAMI NAUNGANA NA MTOA MAONI WA KWANZA KUWAKILISHA POLE ZANGU KWA NDUGU WA MAREHEMU KWA MSIBA MKUBWA AMBAO KWA KWELI UMENIGUSA MIMI BINAFSI.JANA NILIPOSOMA AJALI HII NILIJIFUNZA KWAMBA KILA KUNAPOKUCHA NI MUUJIZA MKUBWA SANA MUNGU ANAOTUFANYIA KATIKA MAISHA YETU. HIVYO TUNAPASWA KUMUOMBA MUNGU NA KUSAMEHE WALIOTUKOSEA KILA SIKU KABLA YA KUANZA SAFARI NA TUNAPOMALIZA SIKU NA KWENDA KULALA. JAMBO LOLOTE LINAWEZA KUTOKEA.KIJANA HUYU MAREHEMU, HANA KOSA BARABARANI LAKINI IMESABABISHWA NA MTOTO MTOVU WA NIDHAMU BARABARANI. MUNGU AWATIE NGUVU NDUGU WA MAREHEMU HUKO MAREKANI, NASI TUNAWAOMBEA MASAFIRI SALAMA KURUDI BONGO KWA MAZISHI.
    ANNA

    ReplyDelete
  6. Mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi, pole sana idd nzaro, mboja pamoja na baba na mama, tunawasubiri huku Tanzania tushirikiane msibani. Ni ngumu sana kwa wakati huu lakini tunamuomba mwenyezi mungu awape subira na imani pole sana

    hellen - Rafiki yake marehemu swaumu

    ReplyDelete
  7. kwani nini? huko michigani ndiyo kunakuwa na habari hizi za kutisha kila siku. mola amlaze mahali pema peponi.

    ReplyDelete
  8. God Rest is Soul in Peace. This is tragic..Mwenyenzi Mungu awajaze nguvu familia ya marehemu.

    ReplyDelete
  9. Poleni wafiwa. Poleni watanzania wa Detroit. RIP our beloved young man. Grandma

    ReplyDelete
  10. Inna Lilaahi wa Inna ilaihi raaji'una.
    Tunakuomba mwenyezi mungu umsamehe marehemu dhambi zake, umuepushe na adhabu ya kaburi, umuepushe na adhabu ya siku ya kiama, umpe kauli thabit siku ya mwisho na umpe malaika wema wamlinde mpaka siku ya kiyama.
    Mwenyezi mungu tunakuomba uwajaze subira wafiwa haswa wazazi wake wawili, ndugu zake, jamaa na marafiki. Amin

    ReplyDelete
  11. RIP Yusuf, loh! Such handsome kaka. Poleni wafiwa

    ReplyDelete
  12. Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi. AMIN

    ReplyDelete
  13. JAMANI POLENI SANA SANA,NILISOMA JANA NIKASIKITIKA ROHONI NIKASEMA PENGINE HAJAUMIA SANA ATAPONA,MUNGU NDIYO MWEZA WA YOTE AWAPE FARAJA NDG NA MARAFIKI NA AIPOKEE ROHO YA MAREHEMU PAHALI PEMA PEPONI,SIKU YA SIKU NASI TUTAMUONA KWA KUWA NDIYO MAKAO YETU YA MILELE.

    ReplyDelete
  14. Natoa pole kwa wafiwa na kumuombea marehemu alazwe pema peponi. Naomba kuuliza tu kuhusu utumiaji wa neno "hayati" kwa sababu mimi nafikiri neno hili lina maanisha alotutoka lakini yuko hai nyoyoni mwetu - kwa kifupi "martyr". Sijui kama ni sahihi kulitumia kama mbadala wa neno "marehemu".

    ReplyDelete
  15. INNALILLAHI WAINNA ILAIHIRAJUUN!

    'hakika sisi sote ni wa M/Mungu na kwake tutarejea'

    M/Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi, amiin!

    ReplyDelete
  16. Kwakweli sisi binadamu tuna kila sababu ya kumuomba na kumshukuru Mungu kwa kila siku anayotupa, kwani hatujui siku wala saa ya kutwaliwa. Kaka wa watu alikuwa na safari zake tu jamani, wala hakujua lililopo mbele yake.
    Hatuna jinsi sisi wengine tuliobaki... ni kumuomba Mungu tu na kujiweka tayari kwa saa ya kutwaliwa.

    ULALE MAHALI PEMA KAKA YUSUPH JAMANI.. Ndugu, jamaa, marafiki na wazazi wa marehemu...tuko pamoja katika kipindi hiki kigumu na cha majonzi ya kuondokewa na kaka yetu mpendwa.

    ....BWANA ALITOA...NA BWANA AMETWAA.. JINA LAKE LIBARIKIWE... AMEN...

    ReplyDelete
  17. Poleni sana ndugu za marehemu.Ndalima nilisoma naye Oysterbay primary school ,alikua classmate wangu na pia nilikutana naye Dretoit MI, ni rafiki yangu ,kwa kweli kweli nita mmiss sana .

    Kitu kimenishangaza ni kwamba, juzi nilikutana na rafiki yangu mmoja ambaye sijakutana naye toka tumemaliza primary school hapo Oyterbay mwaka 1987. Akawa excited kuniona kasema "Miaka mingi tume poteana leo tunakutana na tuko hai wakati kuna magongwa na ajali nyingi ,wenzetu wengi wamefariki , Mungu mkubwa" sikujali kabisa usemi huo na cha ajabu tuka mzungumzia Ndalima, yeye akasema alikutana naye , mimi nikamwambia mara ya mwisho nimekutana na Ndalima 2003 kwenye harusi huko Michigan, baadaye usiku ndio napata taarifa ya ajali.

    R.I.P Ndalima

    ReplyDelete
  18. kusema kweli imenistua hii habari!!
    jana nimesoma hii habari nanikajuwa atapona tu!!. kumbe ilikuwa ndiyo safari yake jamani!!

    TUSEME NINI BABA,HATUNA LA KUSEMA BALI TUNASHUKURU KWANI NI WEWE ULIYETOA NA NI WEWE UMEMCHUKUWA.

    tulimpenda ndalima ila wewe umempenda zaidi!!

    kusema kweli ni njia ya wote mbele yetu nyuma yako
    habari imenistua ila nakutakia mapumziko mema!!

    ReplyDelete
  19. POLENI WAFIWA, NDUGU NA JAMAA WOOTE WA NDALIMA.. TUMUOMBEE APUMZIKE MAHALI PEMA..

    ReplyDelete
  20. siamini jaman dear cousin ndio umeniacha hivyo, ama kweli duniani tunapita mungu awape faraja note ndugu wa marehem Mboja, Iddy, Mwamvita ,Eddy pamoja na Moddy. tuko pamoja nanyi.
    cousin

    ReplyDelete
  21. Mungu amlaze Ndali mahali pema peponi. It was a shock to me still is,it remind me of my late bro Longo. Da Mboja, Mwamvita,Iddi, Mama na Baba poleni sana, I know the feeling.

    ReplyDelete
  22. Nawapa pole ndugu,jamaa na marafiki wote kwa kuondokewa na Yusuph.

    Sisi wote tu wasafari na mwenzetu katutangulia nasi tutafuata.

    Rest in Peace brother.Amen

    ReplyDelete
  23. Si wezi kuamini kabisa!!. Lakini cha muhimu nikujua kwamba sisi ni wa safiri hapa duniani. Poleni sana Baba,Mama, Dada Mboja, Iddi, Mwamvita, Eddy na Moddy. Mwenyezi mungu awape nguvu na awa fariji.
    Ndalima you will be greatly missed and thanks for being a great friend and brother.
    RIP

    ReplyDelete
  24. Mungu aiweke roho ya marehemu mahala pema peponi. Lakini zaidi alete faraja na nguvu kwa familia ya marehemu.
    Ukishapata matatizo una-appreciate sana maisha na kuona kwamba siku zetu zinahesabika. Kwasisi tuliobaki basi tuzidi kupendana na kudumisha yale aliyopigania marehemu.

    Mdau
    Texas

    ReplyDelete
  25. RIP Ndalima.

    Poleni sana Da Mboja, Iddi, Mwamvita, Ayubu, Baba na Mama.

    Mpo kwenye sala zetu, na tupo pamoja kwenye msiba huu.

    Kwa wakuu mliokua huko kuna mwenye simu ya Iddi, Ayubu au Da mboja?

    Tunaomba mtuwekee pamoja na hizo mlizoweka.

    ReplyDelete
  26. This is a wake up call to us left behind. Mwanadamu kumbuka u mavumbi na mavumbini utarudi. My dear people.. Pause and ask yourself, if this happens to you today, ARE YOU READY? Have you forgiven those who wronged you? Have you ask God to forgive your sins? Rest In Peace brother Yusuf Ndalima. Mwenyezi Mungu akulinde na adhabu ya Kaburi. Upumzike kwa amani katika usingizi wa milele.
    Poleni sana wafiwa wote. Mungu awape nguvu katika kipindi hiki kigumu.

    ReplyDelete
  27. RIP Ndalima. Poleni sana wafiwa.

    ReplyDelete
  28. R.I.P Ndali. Inna Lillahi Wainna Ilaihi Raajiun.

    You'll always be missed.

    ReplyDelete
  29. Pole sana Familia ya Mzee na Mama Nzaro. na ndugu zake Ndalima. Nina furaha moyoni kwamba nilipata kumfahamu Marehemu Ndalima na alikuwa kaka mtaratibu mno mwenye amani. Natumaini ameenda na amani na upendo kama alivyoishi hapa duniani. Wote tunaenda huko huko katika muda na nyakati tofauti. Tuwe tayari. tubebe misalaba yetu, tumshukuru Mwenyezi Mungu kila wakati kwa kutujalia familia zenye upendo, tuombe kuepushwa na majanga ya dunia. maana hatujui saa wala dakika na wala siku atakayokuja Mwana wa aliye juu!!!

    R.I.P NDALIMA

    ReplyDelete
  30. You are very right Anon 17,2008 4:09. This is WAKE UP CALL! Are we ready for this. Sababu tuko barabarani kila siku. Tumshukuru Mungu kwa kila siku anayotupa hapa duniani. Tumrudie Mungu, tumwabudu katika roho na kweli. Bwana YESU asifiwe sana!

    ReplyDelete
  31. inalilah waina ilayhi rajiun.. mwenyezi mungu ailaze roho ya maehemu pahala pema peponi.. AMIN

    POLENI SANA NDUGU JAMAA NA MARAFIKI KWA MSIBA HUU....

    ReplyDelete
  32. HUYO MTOTO ALIESABABISHA AJALI DAWA YAKE NI KUTIWA NDANI YEYE NA HUYO MAMA YAKE MAANA NDIO ALIEMFUNDISHA KUWASHA GARI NA NA KUTIA GEA....MAANA WAPO WATU WAKUBWA HUMU HAWAJUI HATA KUZUNGUSHA USUKANI HUYO KAFUNDISHWA NA MAMA YAKE TU KWA SABABU WAO HUA HAWAJALI NAFSI ZAO...

    ReplyDelete
  33. poleni sana !!
    huyu kijana simjui ila nilisoma habari za ajali jana ,leo nimefika na kukuta ameshakufa roho imeniuma mno

    kweli tunapita
    rest in peace my dear brother!

    ReplyDelete
  34. Hivi wazazi wengine mboma wako so irresponsible hivi. Kwanza hako katoto kametoa wapi funguo? Na nani aliyemuonyesha kuwasha gari. Soon tutasiki mara hawezi kushitakiwa kwa kuwa alikuwa na upungufu wa akili (Sijui wanasema autism) na vile alikufa ni mwafrika I tell yuo wote subirini nini watakachokifanya kwa huyo muuaji!!!! Haki lazima itendeke, najua hatuwezi kumrudisha kaka yetu duniani lakini haka katoto kanapaswa kufundishwa adabu ili iwe fundisho kwa wengine. Poleni wafiwa kusema kweli nina hasira sana, nikimwangalia mwanangu wa miaka 13 na mtu aje amchukue kipuuziu naman hii, this is not fare. Simjui personally, but it pains to see people dying innocently, Inshallah tunawaombea wazazi wetu waliopoteza kijana huyo Mwenyezi mungu awape tahfif na uvumilivu. ITS NOT EASY TO LOOSE A CHILD, DUUUH. POLENI.

    ReplyDelete
  35. The family of Nzaro and friends.I was deeply saddened to hear of your loss. My thoughts are with you.

    Rest in peace Yusuf.You were the best friend that a person has ever asked for.Although we loved you dearly, we could not make you stay. A golden heart stopped beating, hardworking hands at rest. God broke our hearts to prove to us, He only takes the best.
    Mungu ailaze Roho yako mahali pema peponi.

    Kohai -Japan

    ReplyDelete
  36. INNALILLAHI WAINNA ILAYHI RAJIUN
    Poleni sana wafiwa M/MUNGU amjaalie marehemu amlaze mahala pema peponi na awape subira wafiwa wote katika kipindi hiki kigumu.

    ReplyDelete
  37. Surely life is too short!!! What a shock to all friends and family of the deceased? Rest in Peace brother, and stay strong all who knew and loved him dearly.

    ReplyDelete
  38. Pole sana mzee wangu mohamed nzaro,mama eva,iddi,mboja na mwawita.mungu amuweke peponi mdogo wangu ndali.posted by iqbal visram and family bukoba tanzania

    ReplyDelete
  39. poleni jamani.Its so sad. RIP.

    ReplyDelete
  40. Jamani kaka wa watu...RIP

    Nilisoma hii habari jana asubuhi nikajua atapona tu.

    Cha kushangaza ni kuwa usiku wakati naangalia news ikatokea habari ya mwizi mwingine wa gari kagonga watu na wamefariki wawili. Kilichonifanya nikuumbuke hii habari yake ni kuwa ni kama copycat ya hiyo ya huyu kaka. Gari lilikuwa linakimbizwa na police ni benzi na lililogongwa ni Honda na wao walikua wanasubiri green light hivi hivi.

    I wonder kwanini bado wanachase hawa waizi wa magari hivi kila siku? Hilo gari linaworth kweli uhai wa mtu???

    ReplyDelete
  41. Another young life taken away b'se of car accident. This is definitely a life taken too early and so senselessly! But why do police continue to chase these stupid thieves?

    My heart and prayers go out to his family and friends.

    RIP you will be missed

    ReplyDelete
  42. Poleni sana kwa msiba huu mzito wa mdogo wetu Ndalima. Nimeshtushwa na kusikitishwa sana na hizi habari. Ni miaka mingi imepita tangu nimuone Ndalima lakini namkumbuka vizuri akiwa mtaratibu kama watu wanavyomuelezea.
    Mwamvita rafiki yangu, Da Mboja, Iddy, Eddy, baba, mama, mtoto wa Ndali, na ndugu wote tunawaombea mungu awape nguvu ya kuendelea. Mungu muweke mahali pema peponi Ndali. Milembe

    ReplyDelete
  43. RIP Ndalima, sikujui ila nimeumia sana baada ya kusoma taarifa hapa kwa michuzi juzi ulipata ajali the same day na mimi nilipata ajali lakini nikajisemea moyoni Mungu atusaidie,leo nimepata mshtuko sana baada ya kuona umeaga dunia.
    Mungu awape uvumilivu wapendwa wazazi wako Ndugu jamaa na marafiki sote tu wapitaji!

    ReplyDelete
  44. Amina kavira,umenikumbusha kuhusu Longo,kwa kweli ni msiba mkubwa ulionistua katika maisha yangu yote na still siamini kama longo amefariki.Mungu awaweke peponi my dear friend Longo Kavira na Ndalima.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...