kikosi kabambe cha tanzanite fc ya atlanta
nyota ya mchezo Hadji Helper akimtoka Piere Stockovic wa timu pinzani
Timu ya soka ya Tanzanite Fc ya Atlanta wikiendi hii imefanya mauaji ya kutisha katika ligi daraja la tatu inayoendelea hapa Georgia.
Wakiwa wageni wa HCAG UF ya Lethonia GA waliweza kuwatandika wenyeji wao hao kwa bao 3-1. Hadi wanakwenda papumziko washindi walikuwa chini kwa bao moja bila.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku Tanzanite wakijalibu kila njia kusawazisha mabao hayo. Iliwachukua dk. 15 kuswazisha bao hilo lililowekwa kimyani na mshambuliaji hatari Khamza Liganga "Liga".
Alikuwa Liga huyo huyo aliyewainua vitini washabiki pale alipopachika bao la pili baada ya kupokea pasi kutoka kwa Mzindwelha Ghaninze "Muzi".
Dakika ya 35 almanusura nyota ya mchezo wa leo Hadji Helper awapatie washindi bao baada ya kuunganisha krosi safi kutoka winga ya kulia iliyopigwa na Muzi. Alikuwa ni Khamza Liganga tena aliyepachika bao safi la ushindi baada ya kupokea krosi safi ya chini iliyopigwa na winga nyota mchachari Hadji helper.

Ushindi huo ni wa pili kwa timu hiyo inayoshiriki ligi hii kwa mara ya kwanza hapa USA.
Mechi ya hii imekuwa gumzo kubwa hapa Lethonia GA baada ya solid perfomance iliyoonyeshwa na wachezaji Hadji helper, Elvis Doto Mnyamuru, Khamza Liganga, Muzi, Capt. Fredrick Mburushi, Said "Jogoo" Chambuso, Adrei Savu, Aaron, malik, Abdulshareef, Sajo na Mbelkwa Dramin.
Mungu ibariki Tanzania na watu wake,
Mungu Ibariki Tanzanite Fc.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. jitahidini mtanyakuwa kikombe.

    ReplyDelete
  2. 3-1 ni mauaji ya kutisha? mnasema kama vile hijawahi kutokea au ni vigumu mno timu kushinda 3-1!!!!!!

    ReplyDelete
  3. These brothers are serious. The brothers know what they are doing. I am so proud of them. See how energetic they look. Keep up the good work. Well done and good luck in your games.

    ReplyDelete
  4. mchangiaji wa tatu tusidanganyane bwana! serious gani? na unatutaka tuangalie nini? ukiangalia picha tu unaona kam wote hawako fit kabisa, vitambi vimefunikwa na jezi na ni wanene kupita kiasi. ENERGETIC? yeah yeah yeah

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...