Meneja wa kundi la TMK wanaume family Mkubwa Said Fella akipeana mkono wa asante kutoka kwa mganga mfawidhi wa hospitali ya Sokoine iliopo Mjini Lindi bw.Edga Mlawa baada ya kundi hilo kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwenye wodi ya watoto na wazazi,vitu hivyo kadha wa kadha zikiwemo nepi ,poda/uji wa ulezi/Lishe na vinginevyo.Kundi la TMK Wanaume family lilikwenda kanda ya kusini kwa ziara ya kimuziki

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. ebwana hiyo powa sana mkuu said fella na kundi lako lw wanaume, mioyo kama hiyo ndio mwake katika jamii yetu ya kimasikini sio mpaka uwe na hela kama za EPA ndio utoe msaada.

    ReplyDelete
  2. naona siku hizi fani nzima ya sanaa imetiwa hamasa sana na hili suala la uotaji wa misaada sehemu mbali mbali, naunga mkono hili suala lakini kwa yale makampuni makubwa kama haya ya utoaji huduma za simu nafikiri ni vyema wakawa na utaratibu wa kudumu wa utoaji misaada katika sehemu hizi hasa vituo vya kulelea watoto yatima. inawezekana kabisa kampuni kuchukua kama vituo viwili ama vitatu na kuwapa fungu flani kila mwezi kwa ajili ya huduma ya vi/kitio hicho. badala ya kuoneka tu siku za Idd na christmass wakipiga picha huku wakitoa mbuzi mmoja na gunia la mchele wakati huo ni muda wa maongezi wa mtu mmoja tu tena wa siku moja kama sio dakika kadhaa.

    ReplyDelete
  3. hao tmk wenyewe wanahitaji msaada

    ReplyDelete
  4. Fella Umenenepa Kupita Mitaji Yako(Waimbaji)

    ReplyDelete
  5. safi sana, saidieni watu bwana, lakini huyu manager mbona anavaa kama kibaka.

    ReplyDelete
  6. we Fella bado huja acha mambo ya ubichi boy ndo mavazi gani hayo ktk ghafla kama hio sio unaenda na li carwash lako tumbo kubwaa vaa kiheshma
    japo nakupa sifa kwa msaada pia wasaidie wanamuziki wako sio unenepe wewe tuuu kama walivo kuimba ktk ndege tunduni tunasuburi msaada mwengine ukitoa uvae suruali na shat sio ka bukta na ze fulanazz aina ya kawoshi kuwanusisha wezio vikwapa tu

    ReplyDelete
  7. hahahahaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
    sina mbavu,,,
    wanaume mmeiteka nchi,kanisa,misikiti,shulez nk na mmetuaribia watoto
    ila mmna sauti swaaafi mashalaah
    IVI WANAUME FAMILY NDI KINA CHEGE,TEMBA AU NANI YULE NSHAMSAHAU JINA YANI

    ReplyDelete
  8. hawa wote ni mafisadi, wametumwa na yule fisadi chipukizi namba moja joni mashaka.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...