waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa mh. bernad membe akiongea na wafanyakazi wa wizara hiyo (hawapo pichani) wakati wa hafla fupi ya kumkaribisha naibu katibu mkuu mpya wa wizara hiyo, mh sethi kamuhanda asubuhi hii. kabla ya hapo mh. kamuhanda alikuwa msaidizi wa rais (hotuba) ikulu. na kabla ya hapo alikuwa bosi wa tanzania standard newspapers, wachapishaji wa daily news na habari leo. shoto ni naibu wazari katika wizara hiyo, balozi seif.
naibu katibu mkuu mpya wa wizara ya mambo ya nje na uhusiano wa kimataifa mh. sethi kamuhanda akiongea na wafanyakazi wizarani hapo leo asubuhi. kulia kwake ni waziri membe na naibu waziri balozi seif. Picha na mdau assah mwambene wa mambo ya nje


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Tunashukuru kwa wizara hii kupata Naibu Katibu mkuu ambae atasaidiana na Katibu Mkuu pamoja na Waziri husika ili waweze kulisaidia taifa letu liweze kupiga hatua katika mambo ya kidplomasia na kupambana na changamoto nyingi za dunia ya kisasa.


    Tuna imani pia Naibu Katibu atasaidia kuhakikisha kuwa watendaji wale wote wanao pata nafasi ya kufanya kazi katika balozi zetu mbali mbali ni wale wenye uwezo wa kuhimili changamoto na kulisaidia taifa letu. Kwa mantiki hiyo basi, wale wote wanao bahatika kupata nafasi za kuliwakilisha taifa katika kada mbali mbali nje ya nchi wawe watu makini yaani wachapa kazi na sio kwa kujuana na baadae kuliabisha taifa.

    Naibu Katibu mkuu anatakiwa kuhakikisha kuwa wastaafu na wale ambao wameshastaafu lakini wakabahatika kuongezewa muda wachape kazi kwa kulisaidia taifa kwa moyo thabiti na sio kufanya kazi kwa maslahi yao binafsi.

    Tunakutakia kila la heri katika eneo lako jipya la kazi.

    ReplyDelete
  2. It has started....na bado! Safisha safisha ya wakati huu itawashitua au/na kuwashangaza wengi!

    Ngoja uone......

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...