Mtunzi bin Fulani, ahsante kwa majibu
Niloleta barazani, siswali setaka jibu
Niliwapa burudani, kwamambo yalonisibu
Ukweli sikula penzi, pweza ameniumbua
Utunzi ni kitu fani, kwakweli umejaribu
Wewe kwangu nimtani, au niseme swahibu
Ufafanuzi wa ndani,niko nao mahabubu
Ukweli sikula penzi, pweza ameniumbua
Moyo upo furahani, kwazako zote sababu
Shairi nilolibuni, kiutunzi limesibu
Mmefika malengoni, nakuhakiki karibu
Ukweli sikula penzi pweza ameniumbua.
Nimefika ukingoni, sitaki tunga kitabu
Malenga mbele songeni, tutimize taratibu
Ingieni ulingoni,tuache zetu hesabu
Ukweli sikula penzi,pweza ameniumbua.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. PWEZA
    Moyo kumkinai,iwache mbovu tabia
    taaban bin hoi, humtaki watwambia
    Hutaitwa bedui,pweza kumkimbia
    Pweza sote hatufai, wala kumkurubia

    Muhibu rohoni, na magesti kuhamia
    Bara na visiwani, kote kuvinjairia
    Watokapo ndani,nawe uliwaipamia
    Pweza sote hatufai, wala kumkurubia

    Msako masokoni, kwa fedha kumnunua
    Bei poa jamani, au ghali maridhia
    Hujihisi burudani, kila ukiparamia.
    Pweza sote hatufai, wala kumkurubia

    Hima mavyumbani, pweza kumtumia
    kwa mziki na asumini, uturi kunukia
    Vifupi vigauni, na vidani kupambia
    Pweza sote hatufai, wala kumkurubia


    Kila ulipotamani, kuwa beep huamua
    Huwaficha ndani,Esta,Lily na Ua
    Hutaka wawe laini,urojo hujilia
    Huna kinga jamani, peku huingia

    kwa sasa hutamani, pweza wamkataa
    Miwasho mapajani, mabaka amekutoa
    Tiba hospitalini,bado hawajaitoa
    Pweza sote hatufai, wala kumkurubia

    Waganga wa darubini,waijua sababu
    Mwili hauna amani,kwa dhiki na tabu
    Kinga zote mwilini,kufifia taratibu
    Pweza sote hatufai, wala kumkurubia

    Hongera kuamua, kwa msimamo thabiti
    Sote tungejua, majuto ni laiti
    Giza penye jua, huo ndio usimart
    Pweza sote hatufai, wala kumkurubia

    ReplyDelete
  2. Profesa Mlimani, mtihani wataka jibu
    Aloleta barazani, swali lataka jawabu
    Hakuleta burudani, kwa yalomsibu
    Ukweli kala nini,hayo nimasaibu


    Tungo yakale fani,muuliza hana jibu
    Nashangaa jamani, ni mtihani wa hesabu
    Sasa ni mwalim gani,test iso majibu
    Eti kaleta utani, kijiwe cha ma swahibu?

    Ukweli na undani,pweza kamuumbua
    Moyo haupo furahani, kwa zake zote sababu
    Shairi aliolobuni, kingano apata aibu
    Eti kaleta utani, kijiwe cha ma swahibu?

    Ushauri nasaha fani, msaada wa karibu
    Au nyota ya kijani, AMREF si tabu
    ANGAZA wako mtaani, usiwe bubu
    Waeleze kwa makini, pweza alivyokusibu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...