Pole kwa kuendesha mtanange wa mdau wa milioni 5.Mara baada ya Refa kupuliza kipenga cha kuashilia kumaliza mpambano niliuliza hakuna mshindi wa tatu na wa pili kwenye hili pambano? Mheshimiwa ukala jiwe.Mimi nikaona ngoja nife na kizibiti changu kwapani. Sasa kwa kuwa umesema tukuletee, haya ushahidi wangu huu hapa mheshimiwa. Nadhani mimi nitakuwa Mshindi wa Pili. Asante kwa kutufuta Jasho maana leo tumeamka alfajiri kwelikweli kuwahi mpambano. Haahaaahaaaaaaa.
Mdau wako wa Cardiff,UK
(email kapuni tafadhali)
--------------------------------------------------------------------------

Mimi naitwa Evans Ishengoma Kaijage, kwa sasa naishi Eindhoven, The Netherlands. Ni mmoja wa wadau wa "globu" hii ya jamii. Sasa nimekuwa nikijaribu kupata hiyo dola 500 kila mara ila nashindwa kwa namba moja. Naona hii bahati hainikuti tu. Yaani hata nimeamka mapema kutegesha lakini wapi ... nimebahatika kupata 5,000,001. Jamani ... siwezi kufikiriwa? haha ...
Endapo mshindi hatajitokeza, nipewe mimi. Uthibitisho nimeu attach
Evans.
---------------------------------------------------------------------

Kaka Mpambano ulikuwa mkali sana nimeambulia +4.
Kama kutakuwepo runner up ingawa haikutajwa kuwapo tafadhali.
(email na jina kapuni tafadhali)

Kaka Mpambano ulikuwa mkali sana nimeambulia +4.
Kama kutakuwepo runner up ingawa haikutajwa kuwapo tafadhali.
(email na jina kapuni tafadhali)
Mdau wa Nanihii...
-----------------------------------------------------
HAHAHA.... MDAU WA NANIHII, MDAU EVANS NA MDAU WA CARDIFF MMENIKOSHA KWELI. BAJETI YA MFADHILI HAINA ZAWADI YA MSHINDI ZAIDI YA MMOJA. HATA HIVYO KWA MOYO MLIOONESHA TUWASILIANE KWA NJIA HII HII YA MLANGO WA UANI, IKIWEZEKANA NIPENI NAMBA ZA SIMU.YAANI HAPO TABIDI NIJIPIGE-PIGE MWENYEWE ANGALAU MPATE ZA VOCHA. AKIPATIKANA MDAU WA MILIONI 5+3 ITAKUWA RAHA KWELI. TUMSUBIRI...
NTAONGEA PIA NA MFADHILI TUONE CHA KUFANYIKA. HUWEZI JUA, ANAWEZA TOA OFA YA DEODORANTI...SI MNAJUA TENA MAMBO YA VIKWAPA NI NOMA....
-MICHUZI
Huyu ni nani tena ambaye anajina kama langu na kabila langu la kihaya?
ReplyDeleteMichuzi Mbona comment zangu umebania sana, na unaendelea kubania?? mimi nimekutumia email kwa issamichuzi@gmail.com na nikakupa kithibitisho halali kabisa kwamba nilikuwa wa Mil5 kuzuru blog ya jamii, sasa mbona umeminya??? basi kama changa la macho ungeniandikia email kuniambia nikaminya na mimi, sijamind na wala siihitaji zawadi manaake najua ni jinsi gani mhamini kajiminya kuzitoa, tena ningefurahi sana kwamba shindano lisingetuhusu sisi tulio Nje ya nchi... wa Nyumbani ingenoga zaidi......AU ndio ushindi wangu kapewa binti wa ireland??? manaake inawezekana lolote lile, kutangaza mshindi wakati ushahidi unao si unaweza kuamia tu kumtangaza yoyote. nani ataufanya nini na blog yako na sisi wadau hatuachi NG'o kuzuru....Lakini mi nalia na Uadilifu, si unajua ilivyo fresh kushinda, unajisikia uo juuuuu kwenye hii dunia.....
ReplyDeletePoa poa kaka michu, kazi njema... Email yangu imefika kwako bila shaka, cheki cheki uone nini kimetokea....NB Jumapili Leo itakuwaje? utatutumka kwa wana wa buluu??? mi natabiri moja Bila mnafungwa..... samahani lakini...
ndugu unaesikitika na kuweka ushahidi wako samahani lakini ushahidi wako una kasoro kubwa. Nadhani umebabaika, aliekuwa akitafutwa ni mtu alotuma ujumbe wa wa milioni tano, sio visitor wa blog wa milioni tano. hiyo counter inaonyesha ni mgeni (visitor) wa ngapi katika blog. unadhani kama alikuwa anataka kutowa zawadi kwa visitor wa milioni tano angeliwacha counter kila mtu aone?
ReplyDelete