Wananchi wakiliangalia basi la abiria aina ya DCM lililoteketea kwa moto baada ya kuacha njia na kugonga nguzo za umeme zenye Transfoma na kusababisha mlipuko karibu na kituo cha daladala Banana, Ukonga, Dar.
Ajali hiyo iliyotokea jana usiku haikuleta madhara kwa abiria waliokuwemo ndani ya basi hilo.
Chini mafundi umeme wa Shirika la Ugavi wa Umeme Nchini(tanesco) wakiondoka eneo la tukio baada ya kuangalia uharibifu uliotokea.Eneo la Banana litaendelea kuwa gizani kwa kipindi kisichojulikana mpaka itakapofungwa transfoma nyingine kutokana na Transfoma iliyokuwa ikifanya kazi kuungua .
Picha na Aron Msigwa - MAELEZO.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Sijui kwa huko nyumbani inakuwaje, lakini kama ingekuwa ni hapa ninapoishi Japan, huyo dereva angelipa hiyo transformer pamoja na hizo siku watu watazokakosa umeme. Hata kama ni lofa hana kitu, angefanyishwa kazi jela hata kama ni maisha yake yote, na pesa inayopatikana kutokana na kazi anayofanyishwa akiwa jela ndiyo ingelipa deni.
    Lakini kwetu si ajabu ukamuona jamaa anadunda barabarani kama kawa na hakulipa chochote.

    ReplyDelete
  2. Hiyo daladala ina insurance. nani atagharamikia kutengeneza hiyo transformer.

    Bongo tambarare

    ReplyDelete
  3. Kaka michuzi hiyo daladala si kwamba ilikuwa ikitembea ndio ikagonga hilo Transfoma, ukweli ni kwamba lilikuwa likisumkumwa ili liwekwe kando maeneo ya hapo banana, kwa vile trasfoma nyingi za tanesco zipo ajili ya kuzalisha umeme tu! bila ya hadhari yoyote ya hatari,likagusa nyaya ambazo zikapiga shoti, na kusababisha huo moto. Hali iliyowanya waliokuwa wakilisukuma watoke nduki na kuliacha likiteketea. Hakika pia nikiri raia wengi wa nchi hii hatuna elimu ya kuepuka majanga sababu huo moto mwanzoni haukuonekana kuwa na madhara na bahati njema Tanesco waliwhi kuzima umeme eneo lote hata baadhi ya vitongiji vya jirani viliathirika. Still tukabaki tukiutaza moto huo ukifanya vitu vyake.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...