Uongozi wa Jumuiya ya Watanzania Italy unasikitika kutangaza kifo cha Ndugu MOHAMED ABDUL SHAKUR (PAMA) kilichotokea jana asubuhi katika hospitali ya SAN GIOVANNI DI DIO E RUGGI D'ARAGONA" SALERNO.
Kutakuwa na Mkutano wa Watanzania wote leo jioni saa kumi na moja 17:00 pm.
Sehemu: LAGO PATRIA MABEMBEANI.
TAFADHALI TUZINGATIE WAKATI NA KUFIKA BILA KUKOSA.
Mwenyekiti wa jumuiya ya Watanzania Italy,kwa niaba ya uongozi na watanzania wote hapa Italy,anapenda kutoa salam za rambirambi kwa wazazi na ndugu wa marehemu nyumbani na popote walipo, kuwa tumepokea taarifa hizi kwa masikitiko makubwa na tunaungana nanyi katika wakati huu mgumu wa maombolezo.
Mungu ailaze roho yake mahala pema .
Amin.
Abdulrahaman A.Alli.
Mwenyekiti
*****************************************************************
*****************************************************************
WA WALE WOTE WALIO NJE YA ITALY KWA MAWASILIANO TUPIGIGIE SIMU NAMBA:
+39 3271753565(Mwenyekiti)
AU
+39 3453118431 (DULLAH)
au
+39 331 8360509 (Katibu mkuu)
au
+081 3340635 (ofisi ya jumuiya)
e-mail: tnzncommunity@yahoo.com
HABARI ZAIDI: http://www.tnzncommunity.blogspot.com
Poleni sana ndugu zetu wa italy kwa msiba mzito wa Mpendwa wetu PAMA,namjua mshikaji vizuri sana tulikuwa nae kinondoni mkwajuni,na pia Brother wake anaitwa STIBA mshikaji wangu wa karibu mno
ReplyDeleteMUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALA PEMA PEPONI AMEN
Mdau kutoka UK
mungu amsamehe makosa yake amjalie makazi mema na poleni ndugu na jamaa wote wa karibu lkn duh jamaa ameturushia ngumi sana bila sababu za msingi ama kweli kila chenye mwanzo kina mwisho wake lkn natumaini waliopigwa ngumi na huyu kaka watamsamehe wote na kumtakia makazi mema. Amina!!
ReplyDeleteduuu si mchezo, yaani kila mara tunasikia italy mtz mmoja anafariki kunani huko, duu PAMA amefariki, hakuna mtu asiemjua PAMA ambaye anatokea tanga, tanga nzima jamaa wanajulikana PAMA STIBA NA MKUSA. MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALA PEMA PEPONI AMEN
ReplyDeletePoleni sana kwa msiba mzito ndugu na jamaa,cpt PAMA ni kama mdogo wangu na si kweli kama jamaa hapo juu kuwa anapiga bila sababu,kwa kujitetea ndio kama kila mtu duniani,Mungu ailaze roho yake pema Amin.mdau andrew neri
ReplyDeleteMungu ailaze roho ya marehemu wetu peponi Amen! Bwana ametoa na Bwana ametwaa.... Rest in peace brother PAMA
ReplyDeleteKAKA PAMA NAIANGALIA PICHA YAKO KWA HUZUNI. UMETULEA MIMI NA AKINA ABDALAH SHAKUR. TWASHUKURU NA HATUNA LA KUKULIPA LEO HII SISI NDIGUZO ILA KUKUOMBEA DUA MUNGU AKUPELEKE PEPONI.AMEEN.
ReplyDeleteMDAU NA NDUGU WA KARIBU SANA WA MAREHEM. UK..DAH ALHAMDULILAH.
innalillah wainnailaih rajiuun. sote tuko njiani. mdau andrew namtafuta nduguyo R, je nitampataje?
ReplyDeleteMdau finland