Kiota kipya cha maraha matata sana kimefunguliwa mitaa ya Sae jijini Mbeya. Ni full kiyoyozi, muziki mkubwa, Satelaiti TVs kila kona, sakafu ya nguvu na vikolombwezo lukuki. Kwa ufupi huwezi kuamini uko Mbeya. Wadau mlio Mbeya na wengineo mtembeleao nyanda hizo, pigeni chabo mfurahie hadhi ya dunia ya kwanza jijini Mbeya.
wadau wakipasha msuli club e point hivi majuzi

kona ya viti virefu
satelite kila kona




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. Naona kuna mtu mkubwa mh EM na Bwana JB mtalaam wa kungfu, duh picha imenikumbusha wakati wa Mzumbe sekondari, Mirambo number mbili, ni mimi wako Mzee wa Usudusu

    ReplyDelete
  2. JB bado upo? this is one of the ladies wa kilakala enzi hizo Mzumbe- Kilakala. Bado unadai mzee JB!!!!

    ReplyDelete
  3. Picha za rooms kama zipo
    pliiz.Naweza kuja na 'mzigo' wangu??(Joke)

    ReplyDelete
  4. huyo sio Lucy Koro?

    ReplyDelete
  5. MDAU WA BWENI NACHANGIA

    WAKATI MAGABACHOLI YANAENDELEA KUFUNGUA MADUKA NA BIASHARA ZA MAANA SISI ANASA TU. MATOKEO YAKE TUNAKUA NA MITOTO UNDER AGE MILEVI NA WAZAZI WAO WANASHEHEREKEA NA UKIMWI KUONGEZEKA. TUJIFUNZE MILA NA DESTURI ZETU. HAYA MABO YA KIZUNGU TUWACHIE WENYEWE.

    ReplyDelete
  6. Ebwana huyo si Mashiba? Nadhani hapo ni maeneo ya SAE, Kaka Mashiba hongera sana nashukuru umetimiza ahadi yako nakumbuka ulikua unazungumzia hayo maboresho nikirudi toka ughaibuni break ya kwanza hapo, ila angalia wahudumu wa ajabu ajabu wasikuharibie kiota.

    ReplyDelete
  7. namwona mashiba pale AKA waziri wa starehe mzumbe na lawyer James B huyu alikuwa akikipiga(ndinga) sana pale mzumbe,wakuu naona mambo safi maana hamjabadilika sana na vitambi na vipara vimewasamehe mpaka sasa,tutawatembelea tukija huko nakila la kheri wakuu najua mtafanikiwa...mdau california!

    ReplyDelete
  8. Comment yako ya magabacholi na biashara za maana, offcource walianza biashara tangu miaka mingi kwahiyo capital yao ni kubwa huwezi kuwalinganisha na wabongo ungewapa hongera kwa kujaribu especially mbeya, ni maendeleo hayo sio Dsm tu ndio kuwe kuna kila kitu "mimi sio mnyakyusa wala siwajui" nafikiri mtu anajikuna anapoweza kufungua biashara,anasa ziko kila mahali huwezi kuwa attack kwa hilo, kwasababu ulevi mtu anaji control mwenyewe na mazingira gani alio lelewa, watoto walevi under age sio responsible yao,wazazi wahusika wanapaswa kuwakanya na kutowapa watoto wao,kama uzinzi upo kila mahali binadamu wakipata nafasi kwenye miti ya mikahawa,karafuu,mikoroshoni,ufukweni,vijijini watu kibao wana ngoma huko ambako hakuna sanaa,na ukimwi ni ugonjwa kama magonjwa mengine,ukiniambia cancer nitakuelewa kwasababu mtu anajua atakufa tuu, na hakuna uzinduzi wowote wakumuokoa binadamu kama madawa ya ukimwi yalivyo piga hatua,mpaka sasa hivi wachache wenye ugonjwa wa cancer wana survive,labda kwasababu madawa ya ukimwi yanabaniwa bongo,ama watu wanafanya siri "tabuu kuongelea" wakipata ngoma kuogopa kuchekwa kwamba ni mhuni ama mzinzi,na labda akipewa dawa na kupata nafuu kidogo ana acha,hivyo kupunguza nguvu za dawa na kufanya zisifanye kazi kama zinavyotakiwa,na lishe vile vile inaweza kuwa tatizo,development ya dawa kwa nchi za europe na nyingine nyingi zinamfanya mtu kuishi mpaka siku yake aliyopangiwa kuondoka hapa duniani,ila inatakiwa ijulikane mapema kabila hujazohofika. Sorry nilienda out of topic kidogo kuelimishana,ndondondo si chururu siku moja hakutakuwa na tofauti kati ya gabacholi na mbongo kwasababu ukiangalia maendeleo yana kwenda mbele nchini kwetu,yes we can why not,kwahiyo usiwakatishe tamaa kwamba wao ndio wanasababisha, ungeniambia kufanya compain ya hayo matatizo ningekuwelewa point yako.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...