Kaka Mkuu wa Wilaya ya nanihii,
Anagalia Taswira ya Bustani ya Forodhani baada ya ukarabati.
Zenj kumekucha!!!
Mdau Visiwani

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. Safi sana. Inapendeza namna hii na naamini patatunzwa maana hilo ndio lililo gumu. Si kujenga, si kupendezesha bali kupaweka pawe kama palivyokusudiwa. Inapendeza sana na asante mdau kwa taswira mwanana

    ReplyDelete
  2. Panavutia. Ila je, mimi mlalahoi niliokuwa nauza urojo hapo kabla ukarabati haujaanza ntapata nafasi?, au watapata kina nanihii tu?(wanajijua)

    ReplyDelete
  3. Duh, pamependeza sana hapo forodhani. cant wait kupaona. ila watu wasianze kuleta uchafu wao kutupatupa ovyo na kukanyaga majani halafu ikawa kazi bure.

    ReplyDelete
  4. Tatizo la huku kwetu hata tukitengenezewa vitu tambarare lazima tuvisambaratishe. Haichelewi hiyo bustani mara utaona chupa za maji, mifuko ya rambo, vifuu na takataka lukuki za masalia ya vyakula!! usishangae kugeuzwa kijiwe cha wavuta bangi, vibaka nk!! Yetu macho! Ila nawasifu Zenj kukataa kuwekewa Baa kwenye makazi ya watu!! HONGERENI YAKHEEEEE!

    ReplyDelete
  5. oo yees - haya ndio mambo...e bwana pametoka pina kisawa. ambaye hajawahi fika hapa aende for the w/end

    ReplyDelete
  6. Yangu mengine lakini yanafanana na haya. Hapa Dar kuna Bustani nzuuri yaitwa Botanic Garden, iko mkabala na Karimjee Hall na nyuma ya Southern sun Hotel, zamani ikiitwa Holiday Inn. Bustani hiyo kwasasa imevamiwa na wanafunzi wa IFM, eti wakijidai kujisomea, cha kusikitisha pamoja na matangazo ya kuchimba mkwara watu wasichafue mazingira katika bustani hiyo, wanafunzi hao wamekuwa wakichafua mazingira saana kwa makaratasi na chupa tupu za maji, kiasi cha kwamba bustani imepoteza TASWIRA. Mamlaka ichukue hatua kuzuia hili. Nawakilisha.

    ReplyDelete
  7. kama wananchi ni wakorofi bassi tutumie staili ya mwanza maana huko baadhi ya bustani zinalindwa na kutunzwa masaa 24 kwa hiyo siku zote ni safi na zinapendeza. kwa hiyo dawa ni kuweka walinzi

    ReplyDelete
  8. Cha Muhimu hizi bustani lazima ziwekewe wasafishaji, kila asubuhi wasafishe, pia liwekwe tangazo kwa herufi kubwa kabisa "KUNYA_BUSTANINI_HAIRUHUSIWI"

    ReplyDelete
  9. mkuu nimependa taswira ya foro naomba kama unazo picha zaidi tuwekee tafadhali

    ReplyDelete
  10. Iwe mfano kwa nchi nzima. Imependeza saaaaaaana

    ReplyDelete
  11. hiyo bustani ni nzuri sana. wananchi tuwe wastaarabu tusitupe taka hapo. panatakiwa pia kuwe na vitu vya kutupia takataka. wekeni matangazo kueleza watu wasitupe takataka hapo. pongezi kwa waliotengeneza hiyo bustani.

    ReplyDelete
  12. anyway tanzania we have a long way to go.. havent seen anything fantastic.. then again HAYA NI MAWAZO YANGU NA NAOMBA YAHESHIMIWE

    ReplyDelete
  13. Bustani inahitaji maji, mimea kumwagiliwa ili iwe imenawiri. Matumizi ya mboji na kuwe na kamashine kakunyolea ukoka (mower) sio kufyeka kwa makwanja.

    Miti (shrubs, bushes and trees) inahitaji kupunguzwa (trimming)
    uwekaji bustani nayo ni fani, sio ajira kwa itikadi ya chama au Manispaa kutoa tenda kifisadi

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...