Leo JK ameteua Wakuu wa Wilaya 15 new DCs,  7 wamestaafishwa na  54  wamehamishwa vituo, ili kuongeza chachu ya  uwajibikaji katika kusimamia na kuratibu mipango mbalimbali ya maendeleo na uchumi ili kutimiza malengo ya serikali. 

Kwa mujibu wa taarifa toka Ofisi ya Waziri Mkuu, Ma-DC wawili wamepangiwa kazi zingine na wawili wengine wamepangwa kufanya kazi katika jumuiya za chama tawala - CCM.

Walioteuliwa kwa mara ya kwanza ni  Ms Mercy Sila (Arumeru - Arusha), Mr Norman Sigalla (Hai – Kilimanjaro), Col Issa Njiku (Misenyi - Kagera), Ms Angelina Mabula (Karagwe - Kagera), Dr Rehema Nchimbi (Newala - Mtwara), Francis Isaac (Mbulu - Manyara), Lt Col Benedict K Kitenga (Rorya - Mara) na Lt Col Cosmas Kayombo (Mbarali - Mbeya). 

Wengine ni  Christopher Ryoba Kangoye (Kwimba - Mwanza), Queen Mashinga Mulozi (Ukerewe - Mwanza), Fatuma Mwassa (Mvomero - Morogo), Fatma Ally (Nanyumbu - Mtwara), Juma Solomon Madaha (Tunduru - Ruvuma), Anatory Choya (Kishapu - Shinyanga) na  Erasto Sima (Korogwe - Tanga). 

Ma-DC waliostaafu ni  Elias Marugu (Misenyi - Kagera), Deusdedit Mtambalike (Muleba - Kagera), David Holela (Babati - Manyara), Hawa Ngulume (Mbarali - Mbeya), Mashiba H Mashiba (Kyela - Mbeya), Col Peter Madaha (Nyamagana - Mwanza) na  Gilbert Dololo (Kibaha - Pwani).  

Ma-DC waliopangiwa kazi zingine ni  Patrick Tsere aliyekuwa  DC (Ilala – Dar es Salaam), na  Doreen Kisamo (Uyui - Tabora). Mr Martin Shigela ambaye alikuwa DC (Lindi - Lindi) sasa ni Katibu Mkuu wa UVCCM ambapo  Husna Mwilima (Hai - Kilimanjaro) sasa ni Katibu Mkuu wa UWT.

Waliobadilishwa vituo ni pamoja na Elias W. Lali kutoka Arusha – Arumeru kwenda  Ngorongoro, Evans Balama toka Arusha – Arusha kwenda  Ilala, Jowiko W Kasunga  kutoka Arusha – Ngorongoro kwenda Monduli, Col Fabian I Massawe toka  Dar es Salaam – Kinondoni kwenda  Muleba, Abdallah A Kihato toka Dar es Salaam –Temeke kwenda  Kyela.

Wengine ni Zainab Kwikwega toka  Dodoma – Bahi kwenda Kasulu, Dr Ian J. Langiboli toka Dodoma – Chamwino kwenda Babati, Capt Seif A. Mpembenwe toka  Dodoma – Kondoa kwenda Handeni, Halima Dendego toka Dodoma – Mpwapwa kwenda Kilosa, Lephy B Gembe toka Iringa – Makete hadi  Chamwino na  Elaston J. Mbwilo toka  Iringa – Iringa kwenda  Mtwara.

Wengine ni Darry I Rwegasira toka  Iringa – Njombe kwenda  Mpwapwa, Said M Mkumbo toka Kagera – Chato kwenda Temeke, Frank A Uhahula toka  Kagera – Karagwe kwenda  Tarime, Lt Col John Mzurikwao toka Kigoma – Kibondo kwenda  Mpanda, Saidi Bwanamdogo toka  Kigoma – Kasulu kwenda  Kondoa, Raymond H Mushi toka Kilimanjaro – Rombo kwenda  Arusha.

Wengine ni Jordan Rugimbana toka  Kilimanjaro – Mwanga hadi  Kinondoni, Rashid M Ndaile toka  Lindi – Nachingwea kwenda Chunya, Anna Magowa toka  Lindi – Liwale kwenda  Hanang, Elias Goroi toka Manyara – Mbulu kwenda  Nachingwea, Capt Geoffrey Ngatuni toka  Manyara – Hanang kwenda Musoma.

Walohamishwa wengine ni Saveli Maketta toka  Mara – Musoma hadi Namtumbo, Stanley Kolimba toka  Mara – Tarime kwenda  Uyui, Ms Miriam L Lugaila toka  Mbeya – Rungwe hadi  Misungwi, Halima Kihemba toka  Mbeya – Mbozi kwenda  Kibaha, Fatuma L Kimario toka  Mbeya – Chunya kwenda  Igunga. 

Wengine ni  Athuman H Mdoe toka  Morogoro – Kilosa kwenda  Mwanga, Hawa Ng’humbi toka Morogoro – Mvomero hadi  Makete, Gishuli M Charles toka  Mtwara – Mtwara kwenda  Njombe, Jackson W Msome kutoka  Mtwara – Newala kwenda  Rungwe, Capt Assary Geofrey Msangi toka  Mtwara – Nanyumbu kwenda  Iringa.

Wengine ni Samwel Kamote toka Mwanza – Ilemela hadi Bukoba, Danhi Makanga toka  Mwanza – Kwimba kwenda Kibondo, Magalula S Magalula toka  Mwanza – Misungwi hadi  Lindi, Paul Chiwile toka Mwanza – Ukerewe kwenda Liwale, Mathew K Nasei toka  Mwanza – Magu kwenda Muheza, Lt Col Serenge M.  Mrengo kutoka Pwani – Bagamoyo hadi  Ilemela, Ali N Rufunga toka  Pwani – Rufiji kwenda  Manyoni.

Wengine ni Major Bahati Matala toka  Rukwa – Sumbawanga kwenda Kahama, Thobias Mazanzala toka Rukwa – Mpanda kwenda Sumbawanga, Gabriel Kimolo toka  Ruvuma – Namtumbo kwenda  Mbozi, Peter Toima Kiroya toka  Ruvuma – Tunduru kwenda  Rombo, Amina Masenza toka  Ruvuma – Mbinga kwenda Shinyanga.

Waliohamishwa vituo wengine ni Khadija R R Nyembo toka  Shinyanga – Kishapu kwenda  Chato, Col (rtd) Edmund Mjengwa toka  Shinyanga – Shinyanga kwenda  Mbinga, Magesa Mulongo toka Shinyanga – Bukombe kwenda Bagamoyo, Florence A Horombe toka  Singida – Singida kwenda  Bukombe, Pascal Mabiti toka  Singida – Manyoni kwenda  Singida, Cleophas Rugarabamu toka  Tabora – Igunga kwenda Nyamagana.

Wengine ni Kassim Majaliwa Majaliwa toka Tabora – Urambo kwenda  Rufiji, Lt Winfrid F Ligubi toka Tanga – Handeni kwenda  Urambo, Elizabeth Mkwasa toka Tanga – Korogwe kwenda  Bahi na Zainab Kondo toka  Tanga – Muheza kwenda Magu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 23 mpaka sasa

  1. Mwanamtandao Norman Sigalla naona wamekupa kitengo. Kila la heri

    ReplyDelete
  2. NDUGU ZETU JAMANI NATANGAZA UPENDO UTAWALE KATI YA MLIOKO BONGO NA UGAIBUNI HASA KWA AKINA DADA,

    SISI TULIOKO UGAIBUNI TUNAWAPENDA SANA NATUNAWAOMBEA MEMA KILA SIKU ILI SIKU MOJA BONGO IWE KAMA UGAIBUNI
    MSIKAZANIE KUSEMA BONGO TAMBARARE BADO HAPAJAWA TAMBARARE ILA TUNAOMBA SIKU MOJA IWE TAMBARARE KWANI NI KWETU.

    ReplyDelete
  3. Naona kuna mada ndani ya mada!,Nirudi kwenye mada, heko JK!, endelea kutembeza fagio!, fukuza wote wasiowajibika!

    ReplyDelete
  4. JAMANI NYUMBANI VIPI MBONA KILA SIKU MABADILIKO LAKINI MAENDELEO HAKUNA! WATU WALE WALE NATHANI CHA MUHIMU NI SERA TU! MBARIKIWE NDUGU ZETU BONGO

    ReplyDelete
  5. NIMESOMA WAKUU WOTE WALIVYOPIGWA MAPANGA HUMU NA JK. AJABU MKUU WA WILAYA YA NANIHII (TEGETA), AMENUSURIKA! MHH HII WILAYA INA WALAKINI...TUTAONA YETU MACHO

    ReplyDelete
  6. Hongera Bro. Lt Col Cosmas Kayombo. Mtu safi sana na huo ni mwanzo najua utafika mbali sana. Kaza uzi!!

    ReplyDelete
  7. Mkuu wa wilaya ya nanihii mbona sioni jina lake hapa? Au anaendelea na kazi katika wilaya yake ya nanihii. JK hongera ila watanzania nadhani wana kiu ya maendeleo na si mabadiliko ya mara kwa mara yasiyoleta tija.

    ReplyDelete
  8. Massoud Massoud, Chillicote, OhioMarch 28, 2009

    Jamani yule jamaa yangu Ibrahim Marwa bado anapeta na ukuu wa wilaya?? Yuko wilaya gani siku hizi maana simuoni katika list hii au yeye mabadiliko hayakumgusa??
    Ni mchapa kazi na mtafutaji mzuri kwa njia halali, namfagilia wa wa waaaa.

    ReplyDelete
  9. Mkuu wa wilaya ya nanihii balozi nanihii hajaguswa na mabadiliko haya...Duh ze fulanazzzzzz ina fanya vitu vyake!! au labda ni utendaji mzuri tu ...tusimsingizie!! Hajawahi hata kutishia kuchapa mtu viboko atahamishwa vipi? Najuuuuuuuta kukufaham!!!

    ReplyDelete
  10. AFANDE MIDAKOMarch 28, 2009

    Dr Rehema Nchimbi(MPYA) HIRI JINA SIJARIELEWA VIZURI. MHESHIMIWA TUNASHUKURU KWA KUTUTANGAZIA MA DC, SASA MHESISHIMIWA TUTANGAZIE BASI NA MAJINA MATATU YA WANAOAJIRIWA NA TRA NA BOT PAMOJA NA QUALIFICATION ZAO

    ReplyDelete
  11. NI MAONI TU, INAWEZEKANA KULIKUWA NA ULAZIMA WA KUTEUA WAKUU WAPYA KWA SABABU YA WACHACHE WANAOSTAAFU.
    ILA WANAOHAMISHWA DU, MBONA WENGI HIVYO..SASA HIVI RAIS WETU AMEDECLARE KUWA HALI YA KUYUMBA KWA UCHUMI IMEINGIA TZ NA ITATUAFFECT SANA. NINAVYOELEWA SERIKALI, UHAMISHAJI MAMILION YA SH. YATATUMIKA...MAANA WENGINE KUNA KUHAMISHA MIFUGO, NA WENGINE WATASINGIZIA MIFUGO WASIYOKUWA NAYO ILI MRADI TU WAJIPATIE VISENTI N.K.
    HIVI UHAMISHAJI WA AINA HII INA MAANA UTENDAJI KAZI UMEKUWAJE?
    ILA NAONA MKUU WA WILAYA WA NANIHII YEYE HAJAGUSWA

    ReplyDelete
  12. Naona mjomba Tsere kawekwa kando, sijui atakuwa Balozi nchi gani!!

    ReplyDelete
  13. David VillaMarch 28, 2009

    Wewe mdau hapo juu uliyeongea kuhusu gharama za uhamisho kwenye kipindi hiki cha mtikisiko wa uchumi duniani umeongea pointi nzuri sana,umeharibu ulipoweka utani huko mwishoni.
    Serikali yetu bwana,juzi bwana Lipumba amewambia wapunguze matumizi yasiyo ya lazima lakini wapi

    ReplyDelete
  14. Masoud Masoud DC Marwa bado yuko Same. Yeye kama maDC wengine hawakuhamishwa. Marwa ni hard working na muadilifu.

    ReplyDelete
  15. hapo hakuna kitu maana watu ni wale wale hapo ni kama alivyosema jamaa ni kupoteza pesa maana watasingizia mpaka mababu zao ili pochi litune MUNGU IBARIKI TANGANYIKA SORY TANZANIA

    ReplyDelete
  16. Tusubiri siku mbili tatu hadi Aprili mosi kwa habari zinazomhusu mkuu wa wilaya ya nanihii.

    ReplyDelete
  17. Hongera sana Dr Rehema Nchimbi. Mdau uliyeuliza kuhusu Dr Rehema Nchimbi si mpya. Ni mjumbe wa NEC na ni mjumbe wa UWT. Pia ni mkufunzi UDSM idara ya Historia.

    ReplyDelete
  18. DAVID VILLA
    NAWITHDRAW SENTESI YANGU YA MWISHO KUHUSU MKUU WA WILAYA WA NANI HII ILI MAONI YABAKIE NA NGUVU....
    UKWELI INASIKITISHA KAMA KULIKUWA NA ULAZIMA WA KUHAMISHANA NAMNA HII WAKATI WANATAKIWA KUBANA MATUMIZI.
    CHEKI MAKINI NA HIZO HAMISHO, WENGINE UTAONA WANATOLEWA KASKAZINI KUPELEKWA KUSINI....
    NDO MAANA NAULIZA? KUHAMISHANA NAMNA HII KUNAHUSIANA NA NINI NI KWAMBA UTENDAJI WA KAZI UMEKUWAJE, JE KUNA ULAZIMA HIVYO KIPINDI HIKI? SI AJABU UTASIKIA WAKUU WA MIKOA NAO UHAMISHO KARIBUNI.
    WATAKAOKUWA NA DATA KUTOKA SIJUI HAZINA WAJE WATUAMBIE ZOEZI LIKIKAMILIKA TSH NGAPI ZIMETUMIKA KUHAMISHANA.
    NI HATARI LAKINI...VINGINE TUNAJITAKIA...

    ReplyDelete
  19. HII NCHI HAIHITAJI MKUU WA WILAYA HATA MMOJA. KINACHOTAKIWA NI KUWAFUTA KAZI WOTE NA SAVINGS ZITAKAZOPATIKANA ZIELEKEZWE KWENYE SHUGHULI ZA KIMAENDELEO KAMA KUJENGA BANDARI NA RELI MPYA YA KATI. ACTUALLY HATA WAKUU WA MIKOA HATUWAHITAJI TUNACHOHITAJI NI TUME ZA KITAALAMU KAMA YA "KEENJA" KUFANYA KAZI ZA KIMAENDELEO MIKOANI. HAWA WAKUU WA WILAYA NA WA MIKOA NI WANASIASA NA KIMSINGI SIASA IMESHINDWA KUTULETEA MAENDELEO NCHI HII.

    ReplyDelete
  20. WANAOSEMA JK MDINI MBONA ANACHAGUA WAKRISTU KILA SIKU.LAKINI BADO ANAAMBIWA MDINI.

    ReplyDelete
  21. Hongera kaka Norman you deserve it.Kila la kheri ila tu usijisahau kama wengine,i believe theres is more to come this is jus the beginning .Mungu akutangulie.
    Mdogo wako. Loleza.(97-99).

    ReplyDelete
  22. Kaka Michuzi tunashukuru kwa habari ila tunaomba utufanyie utafiti hili zoezi limeigharimu au litaigharimu serikali kiasi gani cha pesa.

    ReplyDelete
  23. JK ange balance kwani kwenye 15 wapya waislam ni watatu tu waliobaki wakristu.angempa balozi Michuzi ili wawe wanne.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...