Mhudumu wa Afya Shaabani Muna (kulia) akimpima urefu Esau Alex katika zoezi la kupima afya lililofanywa na Afya Club eneo la Don Bosco Dar wikiendi ilopita
Dk. Emmanuel Thaway (kulia) akimpima kisukari Consolata Amon wakati wa zoezi la kupima afya lililoandaliwa na Afya Club katika eneo la Don Bosco Dar

Dk. Johnson John (kushoto) akimpima mkazi wa Kipengi Pancras shinikizo la damu katika zoezi la kupima afya lililoendeshwa na Afya Club katika viwanja vya Don Bosco



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. MzeeKifimboChezaApril 06, 2009

    We Michuzi we.

    Huyo ESAU ALEX hapo juu anapima UREFU au anapima UZITO hapo wewe!?!

    Michuzi vipi wewe?

    ReplyDelete
  2. Wadau naomba kueleweshwa kidogo, Mtu anaposema kupima afya ina maana ya "Kupima Ukimwi" au maana ya ujumla yaani, mapigo ya moyo, figo, cancer cells, malaria, kidneys, na mwili wote kwa ujumla.

    Maana kuna watu wengi tunajua kupima afya ni kupima ukimwi na ukikutwa huna basi afya yako ni njema je kama una kisukari, cancer, TB, na magonjwa mengine haya yanaitwaje ukienda kupima????

    ReplyDelete
  3. Hawa ndo wanaopenda na kujali maisha ya wadanganyika. Na hawa ndio twawezawaita Hero or patriots sio mtu anakaa NYC anaweka kaposti kwenye blog ya mashaka oops sorry, michuzi then mnamwita hero.
    First: The post itself has nothing new or nothing to educate or help any Tanzanian in Tanzania coz it doesn't have any altenatve way out it more likely that it was copied somewhere.

    Pili mitundiko yenyewe iko kwa lugha za watu. Je ni nani mlengwa wa hizo post ni mtanzania ambae muda wa kusoma post ya kiswahili anao mdogo sana au ni watu fulani ambao wanaweza kusaidia baadae kisiasa.

    Why don't we focus on real patriots, ie. wahariri who wrote on ufisadi and tried so hard to open wadanganyikas' mind to the point of putting their carier in jeopardy, thinking of mwanahalisa walifungiwa, why? .....

    Sorry i'm not US Blogger and i don't want a debat

    ReplyDelete
  4. mi pia naungana na mchangiaji wa pili hivi kupima afya ni kupima ukimwi tu?maana imekuwa ni jambo la kawaida kusikia watu wakisema ;mfano {kabla ya maharusi kufunga ndoa wanatakiwa wakapime afya zao} je hapo watu huwa wanamaanisha nini?ni kupima magonjwa yote au ni ukimwi tu na ukiwa huna ukimwi basi we una afya njema ni bora tufahamishane maana mambo mengine yanadumaza akili!!.

    ReplyDelete
  5. Nakosoa kidogo
    Hao madaktari hawana vifaa vya kazi?

    Kwanza viatu alivyovaa havina kinga ya kiafya, hawana makoti ya kazi, hawana gloves kila kitu bure?????

    ReplyDelete
  6. Madaktari jamani hawaonekani professional hata kidogo na huyo anayechukua blood pressure anashika tena mkono huohuo anaoupima ye haoni atachanganya hiyo results maana hata pulse rate zake ziko hapo pia inabidi mtu asupport mwenyewe mkono wake na si yeye kuushika tena jamani nasikitika kuona hivyo ingawaje wahasaidia but wangekuwa professional at least inaleta changamoto mzuri zaidi

    ReplyDelete
  7. hebu toeni hizo ati hawonekani professional lakini wameokoa uhai wa mtu. unajua hapo ni watu wangapi walipata awareness ya bp, glucose na bmi index chart zao? hawafananii mnavyotaka lakini wamesave lives hao wanalook professional wao wako wapi?

    na huyo anayeuliza kuchecki afya ni nini/ sio kosa la hao wanaolitumia hilo neno na kufikiri kucheck afya ni kupima tu ukimwi. awareness hamna kabisa bongo ya annual physical check up. na wengine hawana uwezo wa kulipia kufanya physical. na govt haina vituo vya bure au clinic za bure za kufnya tu physical at least mara moja kwa mwaka or so....govt wanesaha usiziba ufa.....

    ReplyDelete
  8. Kudos Dr Lyimo na wenzako, nyie ndio watanzania tunaowategemea wenye kuvolunter muda wenu kuwasaidia wale wasio weza hata kumudu kulipa medical exam. Pia ni muhimu sana watu kujua kwamba kucheki afya yako ata mara moja kwa mwaka ni muhimu na sio kusubiri mpaka uugue. Dr fagilia.......bado tunakutafutia mke.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...