WADAU WAPENDWA,
KUNRADHI KWA KUINGIA HAPA SAA HIZI. HII NI KUTAKA KUTAMKA KWAMBA MDAU WA MILIONI 6 ANANUKIA MAPEMA KULIKO NILIVYOTARAJIA. YAANI ENDAPO MAMBO YATAKUWA MSWANO NA MOLA AKIJAALIA, TUTAMPATA MDAU WA MILIONI 6 HATA KABLA YA MWEZI WA SABA A.K.A JULAI. NA PIGA UA LAZIMA AONDOKE NA KITITA KINONO.
TAYARI NIKO MBIONI KUSAKA MFADHILI ATAYETOA DONGE NONO ZAIDI YA AWALI KWA MDAU ATAYEBAHATIKA KUWA WA MILIONI 6, KWANI ILE ZAWADI YA DOLA 500 NAONA KAMA HAITOSHI VILE. HIVYO WADAU KAENI MKAO WA KULA, NA TUOMBE MOLA MFADHILI APATIKANE HARAKA. LA, KAMA AKIKOSEKANA ITABIDI NIJIPIGEPIGE MIE MWENYEWE ILI ANGALAU SAFARI HII MDAU WA MILIONI 6 AONDOKE NA DOLA 1000. AU VIPI?
MDAU USIPATE SHIDA. KUTAKA KUJUA NAMNA LIBENEKE LINAVOKWENDA, ANGALIA CHINI YA GLOBU YA JAMII UPANDE WA KUSHOTO CHINI NA SOMA TARAKAMU ZINAKUELEZA NINI.
NAOMBA KUWASILISHA
-MICHUZI
Najua Michuzi utashinda wewe au mwanao mnyamwezi buku?
ReplyDeleteMjomba acha kubania breaking News za Stanford Brigde!
ReplyDeleteMimi nimesahau wadau, inatakiwa iweje ili niweze kuwa mshindi wa hizo milions
ReplyDeleteTukumbushane jinsi ya kula hizo million za michuzi sizizo na mwenyewe
ReplyDeleteAchakubana wewe Michuzi vipi? elekeza watu jinsi ya kushiriki,,sasa unaposema tuende chini mbona na kule hakuna hata maelekezo,,au hili shindano ni watu maalumu,,weka wazi haraka
ReplyDeleteKAKA, BALOZI WA NANIHII, TAFADHALI SANA, NAOMBA GLOBU YA JAMII INIPIGIE KAMPENI ILI KUUTWAA UKUU WA WILAYA YOMBO VITUKA ILI NIPAMBANE NA MAFISADI KAMA US-GLOBBER NA FISADI ALUMNI MA MUZUMBE UNIVERSITY ECONIMCS PETER NALITOLELA
ReplyDeleteANGALIA WASOMI BANDIA WANAOJILETA KWENYE GLOBU YA JAMII NA KUJIITA WATAKATIFU; US BLOGGER NA PETER NALITOLELA AMBAO WANAKASHIFU SHULE ZENYE HADHI ZA OKSFODI NA MUZUMBE. WASIJE KUAMBUKIZA UGONJWA WAO KWA GLOBU YA JAMII.
HII TUZO ITALIWA NA MAFISADI AMBAO KAZI ZAO NI KUTANGAZA CHUKI. SIYO KAMA DR. SHAYO NA MT. YOHAANA MASHAKA AMBAO WANATANGAZA UPENDO NA UZALENDO.
KWA HIYO MIMI KAMA MZALENDO NATOA TAMKO KWAMBA HAWA WASALITI WALAANIWE
MIMI KAMA MKEREKETWA NA MPINGA UFISADI NA USENENE NAMBA WANI, BADO NAWAPIGIA DEBE MWANAHRAKATI GENIUS, RAIS MTAJARIWA 2015 MT. YHANNA MASHAKA NA WAZIRI MUKUU DR. HILDEBAND SHAYO WA KULE RONDONI NA MACHO YA MUNENE JK JANUARY MAKAMBA
LICHA YA KUSAKAMWA NA WAOSHA VINYWA KUTOKANA NA LUGHA YAO, NIMEPENDEZWA JINSI UNAVYOCHAMBUA MAMBO HASA KUHUSU MAENDELEO YA TAIFA LETU.
NADHANI MIMI NITAIPELEKA HII MAKALA KWA WABUNGE WETU KULE DODOMA
MHESHIMWA RAIS MTARAJIWA, TUNAKUUNGA MKONO, NA TUTAZIDI KUKUOMBEA DUA, ILI MUNGU AKULINDE DHIDI YA MAADUI AMBAO PIA UMEONYESHA UNA UPENDO NAO KAMA VILE US- BLOGGER
MZEE WA PAMBA, JAKAYA MRISHO KIKWETE TUNAMPA KURA TENA, 2010 KWA MASHARTI KWAMBA LAZIMA ATUPE MIBARAKA YAKE KWA AJILI YA 2015.
MZEE MZIMA, MZEE WA BAGAMOYO, MZEE MTANASHATI, MZEE WA PAMBA, TUNAOMBA UWABARIKI WANAO.
MBARIKI MT. YOHANNA MASHAKA AMABYE PETER NALITOLELA NA US-BLOGGER WA OKSFODI ANAMUWANGIA, MBARIKI, SHAYO, MBARIKI JANUARY PAMOJA NA RIDHWANI
Mh. MT. Mashaka, January, Dr. Shayo na Ridhwani. Kwa hiyo naomba msinisahau ifikapo 2015 HAMNA MSHABIKI MWINGINE NCHINI TANZANIA ZAIDI YANGU .
ZIDUMU FIKRA ZA MZEE WA PAMBA JK
ZIDUMU
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
KIDUMU
KIDUMU FIRKA ZA LAIS MTARAJIWA 2015
ZIDUMU
ZIDUMU FIKRA ZA MAKAMU 2015
ZIDUMU
USGLOBBER NA PETER NALITOLELA WALAANIWE
WALAANIWE
MKEREKETWA, YOMBO VITUKA !!!!
-----------------------------------
Dakika 30 za Internet Café Zimekwisha
Naomba kama unaweza ufafanue zaidi jinsi libeneke linavyokwenda.
ReplyDeleteNikiwa naangalia kompyuta chini upande wa kushoto kwangu sioni namba za watumaji habari zinavyoongezeka. Naona Michuzi, siku,tarehe...na mwisho kabisa kulia namba za maoni zinavyoongezeka. Au unamaanisha mtoa maoni wa milioni sita? Na kama ni hivyo mtoa maoni kwenye habari ipi, hii au zingine, maana kuna zaidi ya moja.
Bro Michuzi wewe miyeyusho. Kifuta jasho changu cha mshindi wa tatu mpaka leo hujanitumia wakati mwenyewe ulitangaza nikutumie ushahidi. Safari hii mwe! sikeshi tena kusubiri hiyo zawadi.
ReplyDeleteMdau
Cardiff
Kuhusu hizo namba, ni idadi ya watu wanaofungua mtandao wako. au let us say those who browse your website. for now is 5595330
ReplyDeleteDaah... mi nahisi kuchanganyikiwa sasa, mwenye blog yake anasema tarakimu ziko upande wa "kushoto", mi kwangu hapa inanionyesha ziko upande wa "kulia" ndo nahangaika hapa kuzitafuta manake nahisi za upande wa kushoto zimekuwa transparent.
ReplyDeletePole Bro Mithupu, halafu nilitaka kukurekebisha namba ipo kulia na sio kushoto ya blog yako kama ulivyosema
ReplyDeleteITAKUWA INAFURAHISHA KAMA
ReplyDeleteMDAU WA MILLION 6 APEWE MILLIONI 6
MDAU WA MILLION 7 APEWE MILLIONI 7
TUENDELEE HIVYO HIVYO MPAKA COUNTER ISIMAME.