Wataalamu wa Iran katika kituo cha utafiti wa kisayansi cha Royan mjini Esfahan, wiki hii wamefanikiwa kuzalisha mbuzi wa kwanza kwa njia ya Cloning katika kituo hicho. 

Kuzaliwa kwa mbuzi huyo kwa njia ya cloning kunafuatia silsila ya utafiti wenye mafanikio wa wanasayansi wa Kiirani wa kituo cha Royan, na ni baada ya huko nyuma,  kuzaliwa kondoo kwa njia hiyo hiyo ya cloning ambaye alipewa jina la Royana. 

Mkuu wa kituo hicho, Dr. Mohammed Hossein Nasr Esfahani, amesema kuwa mbuzi huyo wa kike alizaliwa mapema siku ya Jumatano  na amepewa jina la Hana.

     Lengo la utafiti huo wa ku-clon wanyama limetajwa kuwa ni kuiwezesha Iran kupiga hatua katika utafiti wa kitiba, likiwepo suala la kuwatumia wanyama waliozaliwa kwa njia hiyo katika kutengeneza antibodies dhidi ya magonjwa mbalimbali. 

Mkuu wa kitengo hicho aidha amesema lengo kubwa lililowapelekea kufanya cloning ya mbuzi huyo ni kumtumia katika kutibu wagonjwa wa mshituko wa moyo au stroke. 

   Hadi sasa ni nchi chache tu duniani ambazo zimefanikiwa kuzalisha mbuzi kwa njia wa cloning . Nchi hizo ni Marekani, Uingereza, Canada, China pamoja na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. 

Kwa maelezo zaidi ponyeza … 
http://www.google.com/
Shukran,
Mdau Tehran.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. Mbona ana makengeza mbuzi mwenyewe! LOL

    ReplyDelete
  2. Da! Ebwana ndioooooo, Mbuzi anapozi la kufa mtu.

    Mdau Davey

    ReplyDelete
  3. wametoa mbuzi gay

    ReplyDelete
  4. NA DUBAI PIA AMEZALIWA CLONED NGAMIA ANAITWA INJAZ, TUWEKEE NA HIYO PIA BASI.

    ReplyDelete
  5. hilo ni jini la kiiran sio mbuzi

    ReplyDelete
  6. Mhhh, huyu mbuzi niaje? Mbona jicho lake linaita kinamna!!!

    ReplyDelete
  7. CLONING NDO NINI JAMANI??
    TUELIMISHANE UMU

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...