RAIS Jakaya Kikwete amebadilisha vituo vya kazi kwa Wakuu wa mikoa 11 ambapo mkuu wa mkoa wa Dodoma William Lukuvi atakuwa Mkuu mpya wa Mkoa wa Dar es Salaam na Abbas Kandoro anakwenda Mwanza.
Taarifa iliyotolewa leo na Ofisi ya Waziri Mkuu ikiwa imesainiwa na Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Aggrey Mwanri, lengo la mabadiliko hayo ni kutoa msukumo zaidi wa shughuli za serikali.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dk. James Msekela anahamia Dodoma.Wakuu wa mikoa wengine waliobadilishwa ni Enos Mfuru kutoka Kagera kwenda Mara, Issa Machibya kutoka Mara kwenda Morogoro, Said Kalembo kutoka Morogoro kwenda Tanga, Mohamed Abdulaziz kutoka Tanga kwenda Iringa na Amina Mrisho kutoka Iringa kwenda Pwani.
Wengine ni Dk. Christine Ishengoma kutoka Pwani kwenda Ruvuma, Monica Mbega kutoka Ruvuma kwenda Kilimanjaro na Mohamed Babu kutoka Kilimanjaro kwenda Kagera.
Mabadiliko hayo ya wakuu wa mikoa yamefanyika wiki tatu tangu Rais Kikwete afanye uteuzi wa wakuu wa wilaya kwa kuteua wapya 15

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Let the Musical Chairs begin...

    ReplyDelete
  2. LANGU MOJA MABADILIKO HAYA KWA SABABU YA UTENDAJI MZURI KTK MIKOA YAO AU MBAYA? KWA MTAZAMO WANGU NAONA SERIKALI YETU INA KAZI YA KUBANDIKA NA KUBANDUA NIA HAYO TU.
    JE WANAJUA NI NINI KAZI ZAO HUKO WAENDAKO? mdau.

    ReplyDelete
  3. mwanza mbona tunaonewa hivi anayetoka na anayeingia wote sawa. Mwanza anatakiwa arudishwe yule ambaye yuko Rukwa. OLE NJOOLAY

    ReplyDelete
  4. ANGEWAHAMISHA WAKUU WA MAHAKAMA,LABDA TUNGEONA HUKUMU YA UFISADI.

    ReplyDelete
  5. Ikiwa 1+2=4 ninauakika ata 2+1 Jibu litakua 4 tu.Siasa za mwaka47,tunaendelea nazo.

    ReplyDelete
  6. Mbeya?????!!!!!

    ReplyDelete
  7. WIZI MTUPU.

    ReplyDelete
  8. MliakuvanaApril 16, 2009

    Hivi hakuna RC anayeiweza Iringa? Nadhani huyu anayekuja ni wa tano tangu 2006 - maRC watano katika miaka mitatu!

    Tui nalio, veyaa!

    ReplyDelete
  9. Yaani katika mabadiliko yote haya mbeya hajaibadilisha? kweli kuna mpango wa kuuharibu mkoa wa mbeya. najua michu huwezi kuiweka hii ila habari ndio hiyo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...