sehemu ya tatu ya intavyuu ya kocha wa taifa stars marcio maximo
Home
Unlabelled
maximo aongea (sehemu ya tatu)
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Most read Swahili blog on earth
Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.
Mimi huyu Maximo nimekuwa nikimsikia kwa muda mrefu zaidi ya miaka miwili sasa.
ReplyDeleteSwali langu je waTanzania ambao wana weza kuwa ni viongozi wa timu tem mbalimbali hapo nyumbani wanafaidika nae?
Tangu kuwepo kwake amesaidia kiasigani na nani ana weza kuniambia uwezo wake katika swala zima la mpira wa miguu?
Kwa kumaliza Tanzania kuna wachezaji wazuri na wenye vipaji swala la lugha kuwasiliana kati ya maximo na wachezaji sio moja ya vigezo vya kutokuwa na mafanikio ya haraka?{MDAU}.
He gots points. Wakuchonga endeleeni...
ReplyDeleteHONGERA MAXIMO
ReplyDeleteNakubaliana nawe ktk masuala ya kocha kuwa na program endelevu, sio mambo ya zima moto ya mashindano tu.Utaona kabisa Maximo analenga nini hapo baadaye kuwa na timu imara.Hatua hii wapo wachache wanaopingana naye kwa mtazamo tofauti, ni kama vile Scolari alivyopinga na wengi kwao Brazil kumtema Romario na kumchukua Ronadinho 2002.Hivyo kuwatema baadhi ya vijeba kiumri ni suala la msingi kuangalia tunaandaa timu ya 2012 na kuendelea ambao hao vijeba wengi watakua wastaafu.Cha msingi vijeba ni kutoa uzoefu kwa vijana kibao.
Endeleza program yako Maximo ili miaka ijayo nasi tupete.
MAKULILO, Jr.
Jamaa anachekesha, Michuzi unampatia huyu kocha anaongea kama kasuku. Ukimwambia tu, umeongezewa contract unasemaje, anaanza ku rap ma verse kibao, yanayohusika na yasiyohusika...
ReplyDeleteFor the first time in the history of tanzanian soccer, our players are been called for trials in the top europeans club like west ham, tottenham. huyu jamaa alipomuita ngassa kwenye nation timu kwa mara ya kwanza watu walipiga kelele oooh anatuletea vitoto. frankly speaking this guy know what he is doing. watanzania kuweni wavumilivu maendeleo hayaji haraka haraka ila kwa programs nzuri. sasa hivi mnataka mziray au kayuni yarudi mambo yaleyale yakina ndolanga angalieni mbele, nyamb... fu nyie.
ReplyDeletethats along time you use already,blaaah,blaaaaaaaaaaaah,blaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.
ReplyDeleteMdau Kamongo
ReplyDeleteHuyu mjuba anaesema kua kwa mara ya kwanza wachezaji WETU wameitwa kwa ajili ya TRIAL anaongea no sense kabisa. Ama ndio washabiki baada raisi kwenda mpirani na nyinyi mmo!!!
Walipoitwa akina Nteze, Lunyamila, Masha na Masatu Ureno ile haiku Trial?? AMa mpaka iwe Uingereza?? Na Athumani China Nae Huko uingereza?? Kama fani huijui usilazimeshae hata netboli pia unaweza shabikia.
Halafu adabu ziro uwezi kuita wadau wenzio nyamb... fu. Ama malezi ya baba huna? Heshima mdau ni kitu cha bure. Jiheshimu.
Mdau lazima uelewe kuwa hakuna asimwelewa Maximo Lakini Swali vitu hivi kwa nini miaka mitatu ndio ayatilie mkazo?? Anazungumzia kua alipata tabu kwa ajili ya utovu wa nidhamu, hivi amesahau kua huko anakotoka kulikua na wachezaji ambao utovu wao bora ya wa kwetu?? Socrates, Rai, Edmundo, Romario, Leornado. Mbona hawakutengwa?? Rai hadi na ukapteni alipewa. Mjuba huyu anachuki binafsi. Anataka awe star yeye. Peke yake ndio maana Tinoco pia katimua. Infact Tinoko mkali zaidi kwa taarifa yenu wadau.
maximo alimkataa Ngassa kiasi cha wadau wa soka kuja juu ndio akamchukua.
ReplyDeletetrials sio mafanikio ya maximo sababu kuna maagenti wa fifa watanzania wanataka kuweka rekodi zao sawa.kwani wako kwenye biashara mwaka huu watakwenda sana trials vijana zaidi ya watano sio nguvu ya maximo.
mdau kisiju.
Mdau wa kwanza ameuliza maswali kadhaa ambayo hayajajibiwa. Kuna mwenye majibu?
ReplyDeleteKwenye hilo la msaada gani ametoa kwa timu, kwa kweli kwa wale tunaokumbuka Taifa Stars Ndolanga, ametoa mchango mkubwa sana. Kwa wale waliosahau, Taifa Stars Ndolanga walipigwa mechi tano kati ya sita. Mechi ya sita tuliingia mitini. Kila mtu alikuwa anakuja anatwanga. Naikumbuka huzuni niliyokuwa natoka nayo uwanjani baada ya mechi, tusirudi kule. Siku hizi walau hata nikisikia mechi dhidi ya Cameroon ya kina Song naenda uwanjani na matumaini makubwa ya ushindi. Hiyo ni hatua kadhaa mbele.
Kwa upande wa suala la lugha kwenye michezo sio tatizo kama mchezaji yuko fluent katika lugha ya mchezo anaocheza. Wachezaji wote wanafahamu offside, cross, wing, pass, one-two nk. Ukichanganya na demonstration somo linaeleweka.