Kampuni ya PSI inayosambaza mipira ya  kiume ya Salama Kondom wiki ijayo itazindua uuzaji wa kondomu hizo kwa  njia ya ATM kama hii ionekanayo pichani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 20 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 14, 2009

    RUKSA KWA MAANA UCHANGU DOA
    KIMTINO PIA RUKSA MAANA CONDOM
    SI ZIPO BWELELEEE

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 14, 2009

    Kaka si vibaya kukosoana hiyo sio ATM inaitwa condom vending machine labda kama ulikuwa unatumia lugha zako za siku zote za utani kama badala ya blog unasema glob ni hayo tu

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 15, 2009

    Sawa ila kuweka na kuangalia ili zisiwekwe ambazo hata muda wa matumizi umekwisha, maana tunaongoza kwa kuweka mambo ila hatuna uangalizi wowote

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 15, 2009

    Waafrica haswa Watanzania sijui mtajua kujiheshimu lini.huwa mnajifanya kutangaza sana hizi condom nyie wenyewe hamtumii na mnasambaza magonjwa mnategemea wenzenu ndio watumie.
    Kujitangaza kwenye vyombo vya habari kuwa mmeathirika sana kama vile ni sifa unatuharibia jina sana duniani.Mbona ulaya watu wana kufa kwa HIV/AIDS lakini huwezikuta wanajitangaza kuwa wao wanaongoza.Elimisheni watu wa hapo nchini sio kwa kujitangaza watu tunaogopeka duniani.{MDAU}

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 15, 2009

    Kama tukiwa na fikra kama za mchangiaji wa mwanzo sidhani kama Watanzania tutakuja endelea, angalia ndugu yangu kwa wenzetu hizo vending machine ziko toilets especially za kike na kuna condom za aina zote, sasa wewe unaposema eti ooh ukimwi hautaisha, kwani sababu ya kuwekwa hizo machine ili watu waambukizane ukimwi? Tupo kwa ajili ya kuambiana ukweli kama mtu anatoa maoni ambayo hayana msingi wowote. Hebu fikiria hivi kwanza: Kuna watu wanashindwa kununua condom kwa aibu na wengine wanashindwa kutumia condom kwa sababu maduka yanakuwa yamefungwa, sasa kukiwa na hizo machines hopeful zitakuwa sehemu nzuri na ambayo mtu anaweza pata huduma anapohitaji. Tuangalie vya kuchangia jamani manake sasa imezidi!

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 15, 2009

    Tanzanians we are geting lost, even in America where I lives, I never seen such a vending machines. this is gona catalize fonication to many include young kids. Guys we better do some moves to stop that. lazima kuna mafisadi wanakula cha ju hapo.
    mkereketwa

    ReplyDelete
  7. Kaka hizo ATM zako labda waweke ndani ya vyoo vya mahoteli, lakini wakiweka sehemu za wazi hawampati mtu.

    Nani anaependa kuwangiwa?
    We imajin ndo hiyo ATM iko pale NBC Posta au pale Posta Mpya!

    Khaa!

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 15, 2009

    This is keeeewwwlllll!!!i just need to know hizi vending machines i hope ziko toilet and not just any coridors eyyy!!ARE THEY flavoured??naomba kwa msisitizo waziweke sana hapo kempinski dar!

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 15, 2009

    We anonymous wa 2:49 AM si lazima uandike Kingereza ilhal grammatically uko ICU, maana duh! Even in America where I LIVES, I never seen such A VENDING MACHINES! wacha weeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 15, 2009

    Kwendeni zenu msilete mambo ya itikadi kali hapa, wengi wetu tunaona aibu kununua kondomu pharmacy au supermarket hasa panapokuwa na mwanamama wa makamo kama cashier this is a gd thing tena ziwekwe vyooni kwenye mabaa na pubs!

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 15, 2009

    ooooh mwenyezi ooooh tuepushe na huu ufilauni

    mtaziweka wapi???

    watu kwanza hawazipendi/hawatumii

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 15, 2009

    heeeeeeeee!!!

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 15, 2009

    upupu...shenzy

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 15, 2009

    WANAPOTEZA MUDA..how can you eat a sweet with its cover,its not a raining season so i dont need a raincoat watsoever.lol

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 15, 2009

    Anony 2:49 AM, May 15th

    Kama unataka kuwadanganya watu, jaribu kutumia lugha unayoijua. Hupo Marekani bali Gongo la Mboto, Dar. kwa kuwa siku hizi Internet cafe ziko kila kona ya Mji, usijitie kuw a umepanchi. Wewe bado mchovu, na sisi huku Ulaya bado tutatesa sana.

    Kama unahitaji kusaidiwa na Kiingereza, uliza waliosoma au utaibika.

    ReplyDelete
  16. AnonymousMay 15, 2009

    Ni msaada mzuri kwa wanojali afya zao. Ni vizuri machine ziwekwe vyooni kwa ajili ya privacy.

    Watanzania muwe wenye kupenda kuelimika hii ni changamoto ya kupambana na ukimwi. Kwa wenye akili timamu hawatojali mwenye kampuni anatumia kifaa au hatumii bali ataangalia uhitaji wake wa kifaa hicho.

    Hapa kuna mawili tu either kuacha uasherati au kutumia kifaa. Hizi machine zitawasaidia sana wastaarabu wanaojali afya zao.

    Hizo nchi za nje zinazosemekana kuwa hakuna machine za condom ni zipi? tuongee kwa ushahidi, kuna maeneo maalum ktk nchi hizi ambayo machine za pads za wanawake pamoja na condom zinapatika. Na isitoshe condom zinapatikana ktk kila surgery (zahanati) na hizi zahanati ziko kwenye maeneo yote ya makazi ya watu, hivyo mtu unapohitaji, ni kiasi cha kwenda dirishani kuomba na huwa zinagawiwa kwa wingi za kukutosha kwa kipindi unachotaka.

    Hakuna machine za condom kwa sababu condom ziko available na wenzetu hawana tabia za kushangaana katika vitu vya kimaendeleo.

    Naomba tuchangie hoja kimaendeleo ili tuwasaidie ndugu zetu wengine kama siss tumeshakata tamaa.

    Swala hapa ni wapi ziwekwe na si kwamba hazitapata wateja.

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 15, 2009

    Huu ni wizi mtupu.Kwanza mnachochoea uzinziiiiiiiiiiii. Kutuletea hizo ITM za kondomu kwanini msituletee ITM za kuwafichua mapapa na manyangumi.

    Alaah kumbe nimegundua aliyemuwasha mzee Mwinyi Kibao alikuwa sahihi.

    Habari ndio hiyo.

    ReplyDelete
  18. AnonymousMay 15, 2009

    BRO MICHU NAULIZA HIVI ILISUALA WAKUU WA NCHI WANALIJUA JAMANIII NAONA SASA HATA WASIOTAKA KUZINI WATAHITAJI KUZINI NA NCHI YETU SIJUI KAMA ITAENDELEA.JAMANI SIKILA WANACHO KISEMA WAZUNGU NDO KIZURİ,FIKIRI BRO MICHU KAMA HIZI MASHINE ZITAFUNGWA MPAKA VIJIJI JAMANI WATU WATAMALIKA KWA UKIMWI JAMANII,Mdau Dr

    ReplyDelete
  19. AnonymousMay 15, 2009

    MI SASA NATAKA NIMSIKIE KIONGOZI YOYOTE AROPOKE KUWA TANZANIA BILA UKIMWI INAWEZEKANA!!!
    WENZETU WAMEIGA MAMBO YA MAANA NA SASA WAMEENDELEA KIUCHUMI NA KIJAMII.
    SISI HUKO, SHOMBO TUPU, VIONGOZI NYAMAFU KABISA, KAZI TU KUIIBIA NCHI WAKISHINDWA KUISAIDIA JAMII DHIDI YA MAAFA!
    UKIMWI NI MAAFA NAMBARI MOJA HASA HUKO KATIKA ULIMWENGU WA TATU, NA UNAMALIZA WATU HASA!
    HUKU ULAYA HATA HUWASIKII TENA WAKIUZUNGUMZIA, SABABU HAWAJALI TENA NA WAMESHINDWA KUUDHIBITI!
    INABIDI KILA MTU AJICHUNGE MWENYEWE!
    HUKO SASA WANAKULETEENI BIASHARA YA MIPIRA, SASA IUZWE KIHOLELA. NANI ATAHAKIKISHA UBORA WAKE KAMA HAIPASUKI MTU AKIWA KARIBU NA KUPIGA GOLI?
    AU MMESHASAHAU JINSI BIDHAA FEKI ZILIVYOZAGAA MITAANI? NANI ATAKUHAKIKISHIENI UBORA WA KONDOMU ZITAZOUZWA?
    MAANA HAPA UK PAKITI YA MIPIRA 12 INAFIKA MPAKA £9, HUKO MTAUZIANAJE?
    SASA ZIKISHALETWA HIZO MASHINE, MHESHIMIWA RAISI TUTAMWOMBA BAADA YA MWAKA MMOJA AADHIMISHE FAIDA YAKE KITAIFA DESEMBA 1 KWA KUTOA TAKWIMU MPYA ZA UENEA KWA UKIMWI.
    JAMAA WABONGO MPAKA LINI NYINYI MTAACHA KUIGA HATA YASIYOFAA KUIGWA?
    JAMAA MSIPOKUWA MAKINI BONGO ITATEKETEZWA KWA LAANA YA NGONO SI MUDA MREFU UJAO.
    MUNGU ATULINDE, Amin.
    Mndengereko, Ukerewe

    ReplyDelete
  20. AnonymousMay 17, 2009

    Am kweli kila mtu na macho yake! nyinyi imeshikilia ATM mimi macho yangu yametua kwa huyo dada! du jamani kuna mtu ana email? michuzi vipi?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...