warembo watakaopanda jukwaani leo usiku kwa ajili ya kinyang'anyiro cha kumsaka malkia wa Miss Morogoro 2009 kwenye ukumbi wa Hoteli ya Masuka ya Mjini Morogoro.
WAREMBO 11 wanatarajia kupanda jukwaani leo usiku kwenye ukumbi wa Hoteli ya Masuka village ya kwa ajili ya kinyang’anyiro cha kumpata malkia wa Miss Morogoro 2009.
Mkurugenzi wa Kampuni ya FG arts Promotion, Frank Kikambako , ambao ni waandaaji wa shindano hilo , alisema jana mjini hapa kuwa maandalizi yote muhimu yamekamilika.
Alisema kutokana na ubora wa warembo waliojitokeza mwaka huu ana imani Mkoa wa Morogoro utafanya vizuri katika kinyang’anyiro cha kumsaka Miss Tanzania kitakachofanyika baadaye mwaka huu.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, aliwataka warembo wanaotarajia kupanda jukwani kwenye kinyang’anyiro hicho ni Shekha Washokera ( 23) Upendo Paul ( 18),J oyce Peter ( 20), Tory Oscar (21), Frola Florence ( 19) na Lorna George (18.
Wengine katika kinyang’anyiro hicho ni Nicole Denis (19) Jacquline Laizer (21), Upendo Damian ( 19) , Mariam Didi (21) pamoja na mlemavu wa kiziwi Carolyn Emmanuel (21).
Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, shindano hilo limedhaminiwa kwa pamoja na Kampuni ya simu za mkononi ya VodaCom, Ze Club, B one Lodge na Masuka Village na litasindikizwa kwa burdani za wasanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka kwa Tunda Man, Spark na Madee pamoja na muziki waTaarabu.
Kwa upande wao warembo hao wakizungumzia kwa nyakati tofauti wakiwa kambini kuhusu kinyang’anyiro hicho, walisema shindano hilo ni ngumu kubashiri mshindi kwa kuwa kila mshiriki ana vigezo vinavyojitosheleza kuibua mshindi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 11, 2009

    uncle michuzi mbona miss dodoma hatuwaoni..........?????????tuwekee mapicha hayo basiiiii

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 11, 2009

    hayo mambo ya miss miss inaboa kweli, hao wadhamini kama wanauwezo wa kuandaa mambo kama hayo kila siku kwa nini hizo hela wasisaidie mahospitali hasa za wazazi hii imeshakuwa too much

    anyway na jua waosha vinywa mtasema sana, nchi umeme wa mgao maji maeneo mengine hamna usalama mdogo kwa wananchi ajira kwa vijana nichache then misssssssss every where around the country

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 11, 2009

    Mwenye nywele natural anyoshe mkono.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 11, 2009

    duh...mbona hata mmoja hana nywele za kiasili...au kuona aibu wa uswahili!!!

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 11, 2009

    Old McDonald had a farm, e i e i o
    And on the farm he had a Miss, e i e i o
    Like Miss, Miss, Miss
    Miss here, Miss there, everywhere Miss ...

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 11, 2009

    mwaka huu morogoro ikipata hata mmoja kwenye kumi bora nitashangaa sana.!!! utadhani wanapulizia moto!!!
    haya mtaalam wa pajazzz uko wapi au hujainasa hii bado!!!

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 12, 2009

    mbona sijaona anayefaa hapo.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 12, 2009

    waruguru typical!!! miguuni viazi ka' mkude au mogela!! morogoro mmeanza ubaguzi wa kikabila?? si mnge-consida na makabila mengine wajameni???

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 12, 2009

    mh nisiinase!!!! nimeinasa sana tu,. mi nisipoingia michuzi globu usingizi ntaupata???? sema morogoro wamekuwa biased kidogo!!! wameshindwa kuniteka kabsaaaa!! bado nina hang-over ya miss EU. ule mdatisho kwakweli utachukuwa muda kunitoka kichwani. still in mission incomplete!!!
    mdau wa pajazzzzzzz!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...