
Akizungumza na glob ya jamii kwa njia ya simu, muandaaji wa sherehe hizo, Shekale Bwana Kelly ambaye ni mkurugenzi wa kampuni inayoshughulika na burudani na vyakula, PAPA AFRICA, amesema kuwa sherehe hizo zitafanyika siku ya Jumamosi ya tarehe 18 mwezi Julai, ambapo watakaofanyikiwa kununua tiketi wataingia ndani saa moja mjini Dusseldorf hadi siku ya pili yake, ambapo meli hiyo itakwenda katika miji mingine kama vile Cologne, Bonn na Koblenz.
Ndani ya meli hiyo kutakuwa na sehemu mbili za burudani, moja kwa ajili ya vijana na nyingine ambayo ni chini ni kwa wale wazee wa zamani yaani old skull, hapo kutapigwa zile nyimbo za enzi hizo.Pia kutakuwa na bendi itakayokuwa ikitumbuiza usiku kucha, huku watu wakila raha na pia kutavukizwa udi ili kupata ladha halisi ya pwani.
Mbali ya hivyo Kelly pia amesema kutakuwa na burudani ya chakacha itakayooneshwa na mabinti kutoka Mombasa, pamoja na Samba itakayooneshwa na wasichana kutoka Brazil.
Amesema watu wote watatakiwa kuvaa nguo nyeupe, ikiwa ni ishara ya amani, kuionesha dunia hususani watu wa Ulaya kuwa Afrika na haswa Afrika Mashariki ni watu wa amani.
Kelly ambaye ni maarufu nchini Ujerumani kwa kuandaa matamasha makali, amesema kuwa kiingilio kwa maana tiketi ya kuingia ndani ya meli hiyo ya kifahari ni euro 20 na kwamba chakula ambacho kitakuwa ni cha pwani kitauzwa.
Tayari sherehe hiyo ya ndani ya meli ambayo itakuwa na ladha ya kimwambao imekwishakuwa gumzo katika eneo hilo la Ujerumani.
Hii kitu mbona inafanyika kila mwaka hapo Minnesota
ReplyDeletetaratibuni hayo maudi na maharufu ya pombe katikati ya bahari,
ReplyDeletemsije rudi nusu kiroba!
kila la kheir!
dj nani????mbona ujasema au kade wa kade....haaaaaaaaaa..sawa ujerumani.
ReplyDeleteKutakua na Heineken?Lazima mtu aokotwe kwenye maji.Wabongo na Heineken check yangu macho
ReplyDeletenawapa hi sana masela wote kule munich, kiel, magdeburg, konstanz karibu na uswisi, dussedolf, frankfurt,hohenheim, achen nakazalika, bigup wakubwa hasa mnaosoma hapo ujerumani manake shule ya mabwana hao si masihara iko juu kishenzi ingawa dunia haitaki kutambua ukisoma kwa mfano economics au econometrics ujerumani kama si mzembe basi utakuwa aluwatani wa uchumi au econometrics na unaweza kufundisha popote duniani. c ya
ReplyDeletechakacha na mabinti wa"jirani zetu"
ReplyDeletemabinti wa samba ya brazil
afu iweje??