Kikosi kabambe cha TASA United kabla ya gemu. Kunradhi jezi tumeagizia ila bado hazijaja
mtanange uwanjani na watani wa jadi
Stori na Taswirazzz na Jennifer Sumi
Timu ya Jumuia ya Wanafunzi wa Tanzania wanaosoma NEW DELHI India na jirani( TASA), jana katika kuungana na watanzania kwa ajili ya kuadhimisha sikukuu ya wakulima SABA SABA ilipimana nguvu na Timu ya wanafunzi wa watani wa jadi, KENYA, Katika mchezo uliofanyika kwenye kiwanja cha Chuo kikuu cha Delhi, North Campus.
Hata hivyo katika mchezo huo ambao ulichezwa kwenye mazingira magumu ya Jua na Joto KALI la INDIA hasa wakati huu wa majira ya JOTO..SUMMER),wanajumuiya watanzania walijitokeza kwa wengi wakiwemo wa Hydrabad, Jamia Hamdan, na Delhi ya kusini yote ikiwa ni kujumuika pamoja na kubadilishana machache.
Mchezo ulikuwa mgumu huku kila upande ukiwa na kiu ya kuweka rekodi, lakini hata hivyo Wakenya walifanikiwa kuondoka na ushindi wa Mabao 5 -3. Hata hivyo, japo walitufunga chenga tuliwala ile mbaya!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 10, 2009

    Huu ni uwanja wa soccer au mbio za farasi?

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 10, 2009

    Nimeamini hivi sasa bongo nguvu mpya hali mpya kandanda mpya sabasaba mpya jezi mpya. kawaida kandanda ilikuwa inachezwa na wachezaji 11 kwa kila timu lkn hali mpya wachezaji ni 9. s/kukuu ya wakulima huwa tarehe 8/8 kila mwaka lkn hali mpya ni tarehe 9/6. jezi za timu huwa sare lkn hali mpya ni papa na nguru
    mdau
    kisiju pwani

    ReplyDelete
  3. Duh walevi tangu lini mkaweza kucheza soka?.Mmejitahidi ndani ya 45°C na bado mkala 5-3 lazima niwape heko.

    Wakati mwingine muombe msaada toka mitaa ya huku Kashmir kuna kamati ya ufundi ya uhakika.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 10, 2009

    Kisiju ndio unachanganya watu kwama uji wa kihindi...8/8 ni siku ya wakulima au ya peasants?, na sabasaba (7/7) ni siku ya wakulima au wafanyakazi, full mixing hapa, au mimi sijui hebu nielezee uzuri weye Kijusi cha Pwani.

    by mdau,

    Ashkmatiti

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 10, 2009

    sikukuu ya WAKULIMA, SABASABA tar 9/6/2009??????????????????????????

    au "watanzania" wa india mnatoka nchi gani?

    labda sielewi elewi...

    nsaidieni

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 10, 2009

    wee jennifer sumi

    izo sikukuu za nchi gani???

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 10, 2009

    SMAHANI ETI NI iringa au india????mbona kama kumefanana au ni mimi tu mijicho yangu?

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 10, 2009

    kaka 2licheza na timu ya hostel kwanguhapa.kama walikwambia ni kenya walikudanganya walikuwa na mchezaji mmoja 2 sasa wangechezaje....

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 10, 2009

    Aaah!! KIZITO baada ya kudisco UDSM kumbe ulikimbilia elimu ya kina kuchi kuchi otahe? Dah sie tupo bongo kama kawaida yetu tunaendelea kukomaa kuliokoa taifa letu. Kimsingi DARUSO bado ipo na mwendo ni uleule ingawae sasa hivi tuna mamluki kibao. We miss you sana brother, we remember your patriotic and ativist movement. we loved you alot big up sana brazaa ila wadau wanasema we mtoto wa fisadi mkuu wa wilaya ya nanilii because when tulipokuwa pamoja UDSM, you claim alot kwamaba we mtoto wa mkulima but leo uko NEW DELHI? tunadoubt upignaji wako. Sie tupo tunaendelea na slab kama kawaida yetu.

    Mdau Nyagonde

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 11, 2009

    mh!! na hao ndo wasomi tunaowatemea warudi nyumabni na kubadilisha hali halisi iliyopo sasa!! msomi wa chuo kikuu INDIA hajui hata tarehe ya sikukuu ya nanenane!!!!
    Sasa naamini maneno ya wengi, kuwa kila kilaza anakimbilia kusoma india!! ninamfano wa watu 2 mabongolala ila cha kushangaza wapo sasa hivi huko wanakula nondo!! mmoja ya sheria mwingine ya comp science!
    Kama wahindi elimu yao nzuri mbona wenyewe wanakimbilia nje kusoma hizo comp science na IT!!! hapa nilipo kuna wahindi kibao, kama darasa la IT wamejaa wenyewe!!, sasa sisi wa TZ kwanini tukimbilie kusoma kwao ilhali wao wenyewe wanakimbia kusoma hizo kozi nchini mwao!!

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 11, 2009

    Hey Jenifer,waaooo can't beleive it,whats ya contacts its me an old friend frm Tabata.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...