RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, ameteua Majaji Wapya Kumi (10) wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Uteuzi huo ulianza Juni 26, mwaka huu, 2009.
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo Jumatatu Ikulu, Dar es Salaam imewataja majaji hao kuwa ni Bwana Ferdinand Leons Katipwa Wambali, aliyekuwa Msajili wa Mahakama ya Rufani; Bibi Eliamnani Godfrey Mbise, aliyekuwa Msajili Mahakama Kuu na Bibi Sekela Cyril Moshi, aliyekuwa Mkurugenzi Mahakama za Wilaya hadi Rufani.
Wengine ni Bibi Fatuma Hamisi Masengi, aliyekuwa Mkurugenzi wa Mahakama za Mwanzo, Bwana Sivangilwa Mwangesi, aliyekuwa Naibu Msajili Mwandamizi, Mahakama ya Rufani; Bibi Pellagia Barnabas Khaday, aliyekuwa Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani na Bwana Moses Gunga Mzuna, aliyekuwa Msajili Wilaya Mahakama Kuu, Iringa.
Taarifa hiyo iliwataja Majaji wengine wapya wa Mahakama Kuu kuwa ni Bibi Hamisa Hamisi Kalombola, aliyekuwa Msajili Wilaya Mahakama Kuu, Mbeya; Bibi Fredrica William Mgaya, aliyekuwa Msajili Wilaya Mahakama Kuu, Mwanza na Profesa Ibrahim Hamisi Juma aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo Jumatatu Ikulu, Dar es Salaam imewataja majaji hao kuwa ni Bwana Ferdinand Leons Katipwa Wambali, aliyekuwa Msajili wa Mahakama ya Rufani; Bibi Eliamnani Godfrey Mbise, aliyekuwa Msajili Mahakama Kuu na Bibi Sekela Cyril Moshi, aliyekuwa Mkurugenzi Mahakama za Wilaya hadi Rufani.
Wengine ni Bibi Fatuma Hamisi Masengi, aliyekuwa Mkurugenzi wa Mahakama za Mwanzo, Bwana Sivangilwa Mwangesi, aliyekuwa Naibu Msajili Mwandamizi, Mahakama ya Rufani; Bibi Pellagia Barnabas Khaday, aliyekuwa Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani na Bwana Moses Gunga Mzuna, aliyekuwa Msajili Wilaya Mahakama Kuu, Iringa.
Taarifa hiyo iliwataja Majaji wengine wapya wa Mahakama Kuu kuwa ni Bibi Hamisa Hamisi Kalombola, aliyekuwa Msajili Wilaya Mahakama Kuu, Mbeya; Bibi Fredrica William Mgaya, aliyekuwa Msajili Wilaya Mahakama Kuu, Mwanza na Profesa Ibrahim Hamisi Juma aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
Mhe. Jaji Sekela nakupa pole kwa kufiwea na mmeo na hatimaye kuzikwa wend iliyopita-roho ya marehemu ipumzike kwa amani-Amina.
ReplyDeletePia hongera kwa kuteuliwa kuwa Jaji.
Kila la heri katika kazi yako.
Mwanafamilia!
Jamani naomba wale wanaofahamu tusaidiane mawazo.
ReplyDeleteHivi Rais huteua majaji kwa hulka yake tu au kuna utaratibu maalum wa kiuweledi??!
Je Kuna tume maalum ambayo hutoa mapendekezo kwa Raisi kwa kuzingatia vigezo mbalimbali ambavyo pengine Bunge limeviainisha?
Je Mahakama ya Rufaa kazi yake ni nini? Je ina idadi maalum kikatiba?
Tuelimishane jamani maana karibu tunafika 50 tumekua.
Mzawa