mhadhiri mwandamizi Profesa Cleophas Migiro akitoa maelezo kwa askari wa upelelezi wa kituo cha polisi cha chuo kikuu cha dar akiwa kwenye tundu ambalo wezi walitoboa na kuiba vitu kadhaa vya nyumbani humo. profesa ni mume wa naibu katibu mkuu wa umoja wa mataifa Dk. Asha-rose Migiro. haya mambo yametokea usiku wa mkesha wa sabasaba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 08, 2009

    pole sana profesa migiro

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 08, 2009

    Nampa pole sana lakini ukiangalia kwa makini basi ujenzi wa nyumba kama hizo kisha ukaweka vioo vya kuslide ni kukaribisha wezi. Inaonekana hao wezi hawakupata tabu yoyote walipoingia. Waliondoa vioo na wala hawakuvivunja.
    Tahadhar kabla l-athar. Kama Professor alipaswa awe mwangalifu zaidi.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 08, 2009

    Kwangu mimi hiyo eneo la tukio (scene of crime.Sijaelewa huyo askari alikuwa kwa uapnde dirisha la vioo liliotolewa kama ugauzi wa tukio ulikuwa umefanyika au la.Maana kama ni tkio la uhalifu kuna vitu vingi vya kuangalia.Mfano unaweza usione kifaa kilichotumika kuvunjia laikini unaweza kupata nyuzi,nyayo za viatu au hata alama za vidole zilizoachwa na wahalifu.

    Nasisitiza hilo ni tukio la uhalifu!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 08, 2009

    Prof pole sana...fuga mbwa, uwe na walinzi hata watatu na waombe estates wakuwekee magrill kwenye madirisha yote...kwa uzoefu wangu wa kuibiwa na ukizingatia hakuna Grill kwenye madirisha nina uhakika hiyo siyo mara ya kwanza kuibiwa , lazima tv, vcr na redio zimeshaibiwa mara kibao humo ndani, pole sana Prof.!!!

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 08, 2009

    ebu basi muwapishe wengine wakae izo nyumba

    khaaa,mmekalia nyie tuu

    jengeni

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 08, 2009

    Profesa,

    Nasikitika sana kwa hayo yaliyokukuta. Hata mimi nilivunjiwa nyumba mwezi Februari, na kuibiwa iMac, laptop, external hard disk 2, na vikorokoro vingine. Tuseme walinitia hasara kubwa.

    Mali yaweza patikana, uhai wako ukiondoka haurudi tena. Nashukuru u-mzima wa afya, hujaumizwa.

    Poke kwa matatizo ndugu yangu.

    ./aziz mongi

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 08, 2009

    pole sana mzee omba uzima watakamatwa tu polisi wakifanya kazi yao inavyotakiwa,
    hii ndo nyumba ya katibu wa UN, majambazi wanaingia bila wasi iwe ya kidampa ka mimi halafu unanambia nirudi bongo?

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 08, 2009

    Azizi na wewe kwa ushamba sasa kuna haja gani ya kututajia ulichoibiwa?

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 08, 2009

    watu wanaibiwa kila siku, hiyo wala si news kwa hapo bongo.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 08, 2009

    wewe uliyetumia lugha ya KIDAMPA Umenichekesha sana.

    Maana hapa nilikuwa na mihasira yangu, vile ninatakiwa kusoma kwa mitihani ya master's na nilikuwa sina mood ya kusoma. Aisee Ubarikiwe sana.

    Siku Njema.

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 08, 2009

    Hivi kumbe nyumba ya huyo Katibu wa Umoja wa Mataifa hailindwi? Ama walilala kama kawaida yao! Keshi ikulu sitashangaa!!Wabongo!

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 09, 2009

    Na wewe acha kujishaua mitihani ya master's ndio nini....Ushamba mtupu

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 09, 2009

    Mie nachotaka kujua siku anavunjiwa prof. alikuwa home au chobingo?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...