Rais Mstaafu Mh. Benjamin William Mkapa akimfariji Balozi Mohamed Maharage Juma baada ya mazishi ya bintiye katika makaburi ya Kisutu jijini Dar. Kati ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh Bernard Membe
Baadhi ya waombolezaji waliofika katika mazishi hayo
Rais Mstaafu Mh. Benjamin Mkapa akijiandaa kuweka udongo kaburini
Wakati wa mazishi
Marehemu Fatuai binti Mohamed
FAMILIA YA BALOZI MOHAMED MAHARAGE JUMA INACHUKUA FURSA HII KUWASHUKURU WOTE AMBAO WALIOWEZA KUSHIRIKI KATIKA MAZISHI NA KUIFARIJI FAMILIA KWA KUFIWA NA BINTI YAO MPENDWA FATUAI BINTI MOHAMED ALYEFARIKI JULAI 08, 2009 NA KUZIKWA SIKU HIYO HIYO.

FAMILIA INATHAMINI FADHILA HII KUBWA YA UPENDO KATIKA KIPINDI HIKI KIGUMU NA INAWAOMBEA NYOTE KHERI NA AMANI NA FAMILIA ZENU.

INA LILAHI WA INA ILAHI RAJOOON

MOHAMED MAHARAGE JUMA




















Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 20 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 13, 2009

    jamani mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi amina..jamani dada mzuri huyuuu!!halafu mdogo mungu wangu eheeeee poleni jamani wafiwa

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 13, 2009

    Inna lillahi wa inna ilayhir rajiun, Poleni sana wafiwa.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 13, 2009

    Inna Lilah wa Inna Ilaihi raajiuun.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 14, 2009

    mungu amlaze roho yake mahala pema peponi,imekuaje jamani ajali ama ni nini mbona mapema sana jamani kifo hichiiiiii yesu wanguuuuu

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 14, 2009

    Hili janga jamani lipo na linaua kwelikweli tujihadharini. ni janga la dunia na halijapata ufumbuzi bado

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 14, 2009

    Pole mno na familia yako yote MMJ.
    Tulimpenda lakini muumba alimpenda zaidi. Tunaamini yuko kwenye maisha mema uko aliko. Amin Mdau Ottawa. CA

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 14, 2009

    Pole sana ndugu yangu kwa kuondokewa na binti yako, Mwenyezi Mungu alilaze roho yake mahala pema peponi. bll

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 14, 2009

    Si vyema kabisa anapofariki mtu kumsema kwa ubaya kadhalika kumtajia siri zake au kumvumizia usiokuwa na uhakika nayo, ndugu yetu mtowa maoni wa tano nakukusudia wewe hasa, si uungwana na sio mila zetu hizo, utanufaika na nini na uliyosema zaidi ya kuwazidishia maumivu wafiwa hata kama usemayo ni kweli kulikuwa na haja ya ulimwengu kujua hususan sasa ameshaondoka ulimwenguni? jamani na tuwe wastaarabu:

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 14, 2009

    Salaam wote napenda kuweka bayana kwamba marehemu alipata food poisoning baada ya kula nyama choma (sehemu jina nalihifadhi kwa kuzingatia sheria) akiwa na nduguze na marafiki vijana zaidi ya kumi katika birthday party 14Juni 2009,yeye na wengine zaidi ya sita walitapika na kuharisha kwa zaidi ya siku tano,wenzake hali ilirejea kawaida ila yeye utumbo ulijipinda na kujaa nyongo tumboni na kutoboka hali iliyosababisha operesheni tatu Hindu Mandal na Muhimbili za kukata na kuunga utumbo mdogo na mkubwa, aidha maini na mafigo yake yaliharibika sana kwa sumu. Wataalamu wanasema kilicho sabisha mauti ni SEPTIC SHOCK kutokana na majeraha ya ndani na nje. Mohamed Maharage Juma, Mzazi wa marehemu ahsante

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 14, 2009

    wewe unajijua utaondoka vipi ama, ni kunyamaza tu naokuomba khatima yako iwe ya salama, na tuendako five second ijayo hujui nini kitakutokea,

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 14, 2009

    huyu msichana amefariki baada ya kula samaki pale kawe club inahofiwa alikuwa na poison either alivuliwa kwa njia isiyohalali au alikuwa ameharibika; wenzie waliharisha na kutapika yeye hakutapika wala kuharisha after few days akaumwa tumbo kumbe kaoza utumbo akafanyiwa operation pale hindumandal akakatwa kipande cha utumbo kilicho haribika after few days tumbo likavimba tena so they had to rush her muhimbili haikuwa rizki mungu akachukua kiumbe wake, so hapo aliyepelekea kifo chake ni kawe club na samaki wao au hindu mandal walikomkosea operation? i t doesnt matter now ndio tumeshampoteza masikini.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 14, 2009

    ...mh

    mbona watu mmeanza kuleta stori umu mara samaki,mara janga la dunia

    nini sasa?ametangulia mbele ya hukumu na kila mtu atafika tu,swala ni kujiandaa wakati wote tengeneza na Muumba wako

    ni hayo tu

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 14, 2009

    Poleni sana family ya Balozi Maharage. Hawa mahayawani wanaoandika upuuzi huu na hakika hawajazaa bado, na hawajui uchungu wa kizika mtoto! Kwa wale wanazuoni iliyobaki ni kumwombea mwanetu huko alikopumzika na siyo kuanza kuandika pumba. Wote tumetoka kwa Allah na kwake ndiko tutarejea! Inshaalah Mwenyezi mungu awape tahafif na uvumilivu katika wakati huu mgumu. Sote tuko nanyi.

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 14, 2009

    Pole Balozi wetu kwa statment hiyo uliyoitoa .. naomba hatua za kisheria zichukuliwe kwa wahusika..

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 14, 2009

    POLENI SANA NDUGU WAFIWA HIYO NDIO KAZI YA MWENYEZI HAINA MAKOSA
    NAOMBA MSIJIBU HAYA YA UMU KWANI UMU KUNA VICHWA VINGI NA SIO TIMAMU ZAIDI NI KUJIPA UCHUNGU NA MAWAZO YA MPENDWA WETUU
    TUNASHUKURU KWA TAARIFA HII YA MSIBA INNA LILLAH WAINNA ILAH RRAJIYN
    MWANA KIJIJI FOTO BARAZA BLOG MAKINI

    ReplyDelete
  16. AnonymousJuly 14, 2009

    poleni sana wafiwa, ama hakika kwake tutarejea. Kisomo lini(40)

    ReplyDelete
  17. AnonymousJuly 15, 2009

    Hakuna marehemu asiyeacha hadithi. Nawapa pole sana familia ya mahemu. Ninachomba tuu kama imesha thibitishwa marehemu alikula sumu katika chakula basi inabidi serikali ifuatilie hilo ili wengine tusije dhurika. Hapa ndio unatakiwa uonyeshwe umuhimu wa elimu ya usafi katika chakula nchi yetu ni ya joto hivyo genetation ya bacteria katika chakula ni kubwa sana. Kwaufupi tu wa ufahamu bacterial generation kwa dakika ni mara mbili ya idadi ya hao bakteri. Yaani kama kuna bakteria kumi katika chakula baada ya dakika watakua 20 na baada ya dakika mbili 40 piga hesabu baada ya saa moja. Na vyakula vya nyama na maziwa vikiwa baridi chini nyuzi joto 65 chini masaa matatu huwahavistahili kuliwa tena. Salmonera au coli bacteria wanaweza kutekteza jiji kwa muda mchache sana. Serikali inabidi iweke mkakati kwenye hilo. Balozi hili limeanzia kwako basi fanyakazi ili wengine wasije dhurika pole sana mungu atakuafu na machungu hayo wewe pamja na familia yako

    ReplyDelete
  18. AnonymousJuly 16, 2009

    This is such a shock!!! I went to school with Fatuai at Academic International school, she was a lovely girl, young and beautiful. My heart goes to the whole family!! Inna lillahi wainna ilaihi rajiuun...I shall include her in my prayers always, being a friend and a fellow muslim.

    ReplyDelete
  19. AnonymousJuly 16, 2009

    This is shocking news!! Fatuai was a lovely girl, young, good hearted and beautiful...I went to school with her at Academic International School. My heart goes out to the family!! Inna lillahi wa Inna ilaihi rajiuun...I shall include her in my prayers always, being a friend and a fellow muslim. Poleni sana Fatuai's family!!

    ReplyDelete
  20. toothpickJuly 17, 2009

    i loved u Fatu..but God loved you more..
    il never forget our big brother moments....
    My heart goes out to your whole family especially ur mum, Teddy bear and ur dad..
    Inna illahi wah inna irrajiun

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...