Mkurugenzi wa Masoko wa Vodacom Tanzania Ephraim Mafuru (shoto) na Mkuu wa Idara ya Huduma kwa Wateja wa rejareja wa KCB Felix Mlaki (kulia) wakimkabidhi Tuzo Milionea 2009 Renatus Mkinga na mai waifu wake Kiticha chake cha shilingi milioni 100 mchana huu katika hoteli ya Kempinski Dar.
shilingi milioni 100 keshi alizoshinda Tuzo Milionea 2009 Renatus Mkinga zikoneshwa baada ya kukabidhiwa rasmi kwa mwenyewe mchana huu


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 16, 2009

    Mpeni hongera zake, lakini mimi bado siafiki mtindo wenu huo wa kutoa zawadi, na sio kwamba nalalamika kwasababu sijaipata hiyo zawadi, la khasha. Mimi ningeona badala ya kumpa mtu milioni 100, hiyo ingeweza ikagawiwa katika zawadi ndogo ndogo ambazo zingewasaidia wateja wenu wengi, badala ya kumpa mtu mmoja tu.
    Hilo ni wazo langu tu
    M3

    ReplyDelete
  2. Huyu mzee amekuwa mkombozi wa jamii kubwa sana ya watanzania.....MUNGU kaiona kazi yake kaamua kumtunuku.
    MBIJE,A-Kafanabo

    ReplyDelete
  3. Wagagagigikoko bwana si mungemuandikia checki tu mpaka mumpe makaratasi yote hayo.Halafu eti wanamwita milionea.
    Millionaire definition:A millionaire (originally and sometimes still millionnaire[1]) is an individual whose net worth or wealth exceeds one million units of currency in USD

    Mdau
    USA1
    Columbus

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 16, 2009

    huo mtindo sio mzuri kabisa wa kutangaza kumpa mtu kiasi hicho cha pesa,ameshinda mmemtangaza mwekeeni kwenye account yake kwisha.namna nyingine mnamtia kwenye matatizo makubwa kwenye jamii.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 16, 2009

    Hongera. Hivi wadau hizo pesa huwa zinakatwa kodi?

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 16, 2009

    TULIKOTOKA NI MBALI!!
    LEO NAWALETEA MASWALI KATIKA SOMO LA SIASA.
    MASWALI YA LEO!!!
    Chagua jibu sahihi kwa kuzungushia herufi husika.
    1. Raisi wa kwanza wa jamhuri ya muungano wa Tanzania anaitwa Julius Kambarage ________
    (a)Kawawa (b) Moringe (c)Sokoine (d) Mandela (e) Nyerere (Maksi 30)
    2. Chama cha kisiasa cha kwanza kutawala Tanzania kinaitwa Chama Cha _________
    (a) Mapinduzi (b)Mafisadi (c) Chadema (d) Maendeleo (e) a na c (Maksi 30)
    3. Raisi wa awamu ya pili Tanzania anaitwa Ali Hassani Mwi____
    (a)Nyimvua (b)ke (c)nyu (d)ko
    (e) Hakuna Jibu
    (f) Majibu yote Sahihi (Maksi 40)
    MWISHO WA MTIHANI
    Ahsanteni.

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 16, 2009

    Huyo mai waifu wake ni Anganile au?? Kafanana nae.....

    ReplyDelete
  8. Hasira hasaraJuly 17, 2009

    Daah! Nimekumbuka mbali sana, Mkinga ulikuwa unafuatilia malipo yako pale Home Affairs, kama sikosei uko au ulikuwa Uhamiaji, God bless you more and more, umeanza kuhangaika siku nyingi.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 17, 2009

    100 MILLIONS ZINAKAA KWENYE HILI BOX, KUMBE NI CHACHE HIVYO, AU KWA VULE MNA DENOMINATIONS ZA PESA KUBWA KUBWA, ZINGEKUWA 100 MILLIONS ZA DOLLAR NI MAGUNIA, HATA HIVYO SINA UHAKIKA KAMA HIZO KWENYE BOX NI 100 MILLIONS AU HIZO NI SAMPLE ZA KUTUONYESHA KWENYE LUNINGA?

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 17, 2009

    Jamani nielewesheni. Hivi hapa watu kusifia dollars, USD n.k. na kuponda hela za madafu ni watumwa? Mi siwaelewi. heri umasikini wa fedha kuliko wa mawazo!

    ReplyDelete
  11. Kweli maisha ni kama mchezo wa soka, usikate tamaa kama dk 90 hazijaisha. Mzee Mkinga bila kwenda SA kwenye BBA amekula Bingo ya kufa mtu...kwa ufupi hakuna lisilo wezekana.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 17, 2009

    Hongera kwa aliyepata hizo pesa. Usemakweli, kama alikuwa anamatatizo mbalimbali ambayo yalikuwa yanahitaji kutumia pesa kuyatatua, basi Mungu kamwona.

    Tatizo ni kwamba ukitoa, hata shilingi miatano katika hiyo milioni miamoja basi sio milionea wa miamoja tena.

    Subiria watu watakuja wengi kuomba msaada, kwani sasa hivi wanajua una milioni miamoja, halafu watakuwa wanasema, hata ukinipa laki tisa sio mbaya hela yote hiyo.

    Wengine watakuja kujitambulisha kwako kama: Mimi ni binamu wa shangaziyako aliyekuwa jirani na mjomba wako aliyekuwa mdogo wake wa baba yako na alikuwa rafiki sana tena rafiki wa kweli, sasa bwana naomba unisaidie hata elfu kumi tu.

    P.E.D

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 18, 2009

    Hongera sana mshindi.

    Nina mtazamo tofauti kuhusu hii: Kwa kampuni kama Vodacom inayofanya biashara "Tanzania", kumpa mtu mmoja zawadi ya Milioni 100, sithani kama ni busara.

    Mdau
    Reading, UK.

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 18, 2009

    Duh huyu jamaa si yule anakuaga kipindi cha sema usikike ITV anatoa michanganuo na mawazo mbalimbali kuhusu mustakabali wa nchi.
    Duh jamaa mjua mengi sana.Ana data za ishu zote political,social.economical.
    Kama sio maswala ya voda kupanga ushindi.basi jamaa mungu amemlipa kwa michango yake.Japo mwishoni MWA MADA ZAKE huwa ana malizia kwa kuonesha kua ni kada wa chama tawala.Hongera usiache tena kuwakilisha sauti zetu wanyonge.endelea sema usikike

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 20, 2009

    NDUGU Zangu mnaojidai mmestaarabika acheni ushamba.. kwanza katika dunia hii kweli unaweza ukapewa hata Tsh 10m/- in cash? Nasema TSH kwa kumaanisha shilingi ya Kitanzania. Na kama mmetoka Tanzania siku nyingi, siku hizi BoT policy ni kwamba any payment above Tsh 10m/- hata cheki huandikiwi, it is paid direct to your bank akaunt via TT. mpe hapo wasomi wetu wabeba maboksi? Ok, na pia I believe mnafahamu maana ya Prize giving ceremony and an action for the press. That brief case full of makaratasi was for the press action, ili kupata action picture Watanzania tuliobaki nyumbani tuweze ona.

    Waaleykum Assalaam

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...