Mheshimiwa Michuzi,
Nakuomba unipe fursa ya kuzungumza na jamaa waislam. Aidha kwa ndugu wa dini mbali mbali naomba radhi.
Ujumbe wangu ni kuwa ramadhani is approaching“If Allahs servants knew what Ramadhan was, they would have wished it lasted for the whole year(Prophet pbuh}
And I would like to remind my brothers and sisters to consider fasting the six days in Shawwal ie the month immediately after Ramadhan. The reward is very great, for your fast of Ramadhan will be counted as a whole year fast.
You can fast consecutively or at intervals during the month of ShawwalI only wish your prayers are accepted and your troubles and those of the whole creation are minimal
Allah Yebarik
Wakatabahu
Mdau

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 23 mpaka sasa

  1. Jazzaka llahu khayra. Kama alivyotufundisha mtume Muhammad Sallalahu alayhi wasallam, kuma tukatazane mabaya na tukumbushane mema, Allah subhaanahu wa taala akulipe kwa hili.
    Ameeen.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 22, 2009

    huna haja ya kuomba msamaha ndg yangu sisi sote watz ndugu. hata mimi hufunga baadhi ya siku kuwaunga mkono ndg zangu waislam maana we are 1 people.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 22, 2009

    walah umeanza vizuri lakini una tuchanganya kilugha katikati sisi itabidi tufungue kamusi ili tupate ujumbe wako -shukran

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 22, 2009

    Allah ibarik to you too. Mungu atupe siha njema na atuepushe na maradhi, tuipate Ramadhan kareem na Shawwal inshaAllah. Nawatakia nyote Ramadhan Njema, Allah atujenge katika kumuabudu, atuepushe na machafu katika maisha yetu yote inshaAllah. Funga hutufanya tuwe wacha mungu na hili ni la kuzingatia sana(2:183)

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 22, 2009

    Sheikh Michuzi ikiwa umeamua kutoa nasaha za dini basi tafuta watu wenye elimu na wanye kuijua kazi yao, kila jambo lina utaalamu wake na taratibu zake.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 22, 2009

    Jazak a.k tunashukuru sana ndigu kwa kutukumbusha, na katika kukumbushana juu ya jambo lililo jema hapahitajiki utaalam umesikia anon wa 07.33

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 23, 2009

    Mdau ujumbe huu ulivyoutoa unaendana kabisa na Utanzania wetu. Mimi sio Mwislamu lakini nawatakieni heri ndugu zangu Waislamu katika kutekeleza imani yenu. Tuonane Eid el Fitri.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 23, 2009

    watu wengine bwana! sijui wanaufahamu mfupi kiasi gani? mfano ni huyu mtowa maoni wa Wed Jul 22, 07:33:00 PM. hivi wewe unadhani kila post itokayo hapa imeandikwa na michuzi? watu wanamtumia post michuzi na ni uamuzi wa michuzi kuziweka au kuzitia pakachani.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 23, 2009

    Nasaha nzuri ila ndugu hii ni copy and paste, si angalau basi ungelijaribu kuibadilisha kidogo angalau kwa kuitafsiri? ha ha ha ha ha ha!!!

    Hili ndio tatizo la mtandao, huwezi kujichukulia cha mtu na kukifanya chako kuna watakaogundua kuwa wameshaona hayo hayo sehemu nyengine.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 23, 2009

    Mdau,

    Jazakallahi hairan!

    Asante kwa kutukumbusha kwamba mgeni yuko njiani na manegine.

    Mungu akubariki.

    Amin

    Na kwa mdau unayefunga siku moja nakupa hongera kwa jitihada zako, keep it up.Funga husaidia sana kuboresha afya yako ya kimwili na kiroho.

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 23, 2009

    ASSALAM ALAYKUM WARAHMATULLAH WABARAQATU.

    NI WAZO ZURI SANA KUTUKUMBUSHA JUU YA MWEZI MTUKUFU RAMADHANIL QAREEM. KITU CHA MSINGI NI KUWA SIO TU TUFOCUS IBADA ZETU KATIKA RAMADHANI BALI INATUBIDI TUJIANDAE TOKA SASA, NI VYEMA KWA KILA MTARAJI MEMA SIKU YA KIAMA AKAANZA KUFUNGA KTK MWEZI TULIONAO WA SHABAAN WALAU KWA KILA JUMATATU NA ALHAMIS (ISHALLAH), TUFANYE IBADA SANA, WALE WAZEE WA KUGONGA MTUNGI PAMOJA NA MAOVU MENGINE NI BUSARA SANA WAKATULIA KIPINDI HIKI, TUKATOA SADAKA KWA WINGI PAMOJA NA KUJIKITA KTK KUTEKELEZA MEMA MENGINE NA KUACHA YALE YANAYOMCHUKIZA MUNGU, NA ISHALLAH MUUMBA WETU ATATUSAMEHE MADHAMBI YETU YALOPITA NA YA JAO, TULIYOYAFANYA KWA BAHATI MBAYA NA KWA MAKUSUDI MANA YEYE MUNGU AMETUHAKIKISHIA KUWA YEYETO ATAKAYE MUOMBA MAGHFIRA ATAMSAMEHE.

    ISHALLAH TUJIBIDIISHE BASI.

    MAASALAM,

    MWANNAZANZIBAR.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 23, 2009

    Ramadhan kareem. Nimefarijika na ndugu waliopost comments zao za kuungana nasi au kututakia heri katika kutimiza ibada hii muhimu. Mungu atujaalie hii harmony iambukize kila mtu. Watanzania wote tukiweza kuvumiliana na kuheshimu dini za wengine kweli itakuwa heri.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 23, 2009

    Assalaam Alaykum Jamia,
    Shukran kwa ujumbe mzuri toka kwa mjumbe wa kwanza pamoja na wachangiaji.
    ninachotaka kuengezea ni kuhusu manufaa/madhumuni ya Ramadhani.Jamani mwezi huu ni darasa la kutufundisha kuacha tabia mbaya. tutafanya mazoezi ya kujizuia kutenda mambo mengi yasiyo na faida kwa mwezi mzima (Mfano;matusi, kusengenya,uongo,zinaa,ulevi nk) INSHAALLAH BASI IWE MWANZO WA KUYAACHA MOJA KWA MOJA.

    Wabillah Tawfiq.
    Kyk.

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 23, 2009

    Assalaam Alaykum Jamia,
    Shukran kwa ujumbe mzuri toka kwa mjumbe wa kwanza pamoja na wachangiaji.
    ninachotaka kuengezea ni kuhusu manufaa/madhumuni ya Ramadhani.Jamani mwezi huu ni darasa la kutufundisha kuacha tabia mbaya. tutafanya mazoezi ya kujizuia kutenda mambo mengi yasiyo na faida kwa mwezi mzima (Mfano;matusi, kusengenya,uongo,zinaa,ulevi nk) INSHAALLAH BASI IWE MWANZO WA KUYAACHA MOJA KWA MOJA.

    Wabillah Tawfiq.
    Kyk.

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 23, 2009

    Nakushukuru sana Mja wa Allah kwa kutukumbsha, Insh-Allah tutafunga.

    ReplyDelete
  16. AnonymousJuly 23, 2009

    Nawatakia kila la kheli ya mfungo wa, Ramadhani ndugu zangu wote, mfungo mwema

    ReplyDelete
  17. AnonymousJuly 23, 2009

    inshallah tunamuomba mola atuwafikishe kufanya mema na kuacha mabaya, uwe mwezi wa kuvuna kheri na kupata mafanikio kwa Allah Subhana Wataala, Tunashkuru kwa kutukumbusha wajibu wetu.
    Nawatakia waislam wote Ramadhan Kareem, waliotangulia mbele ya haki Mola awasameh makosa yao.
    Ameen.

    ReplyDelete
  18. AnonymousJuly 23, 2009

    Nielewesheni jamani, wakati wa ramadhani itakuwa sawa kupost na kushiriki mambo ya anasa kama 'the sexiest man in Tz', nk? Je baada ya Ramadhani? Mimi naona waumini wanaomcha Mungu wanatakiwa kufuata mafundisho yake mwaka mzima!

    ReplyDelete
  19. AnonymousJuly 24, 2009

    Naomba msaada kidogo kwa wadau wenye ufahamu wa hili jambo.Kwa sasa sehem nyingi Marekani jua linachelewa kuzama,inafika mpaka saa 3 usiku lakini bado kweupe.Je kuna namna ya kupata muda wa kufungulia au inabidi kusubiri mpaka jua linapozama??naomba msaada wenu wadau..

    ReplyDelete
  20. AnonymousJuly 24, 2009

    Asalaam aleykum mdau wa friday 0546
    Hakika ni matatizo makubwa suala hili la jua kugoma kutua mpaka usiku mwingi. Nafikiri hapana jibu rahisi bora zungumza na mashekhe walio kwenye misikiti yenu.Jana hapa UK baadhi yetu tulifunga kwa kuwa ni siku ya mwisho ya mwezi Rajjab na pia ni alhamisi, magharib ilikuwa saa tatu na dakika ishirini na moja usiku. Yote ni rehma zake Subhana.
    Wakatabahu

    ReplyDelete
  21. AnonymousJuly 24, 2009

    Mimi si muislamu ila nafahamu kwamba kama jua likizama ndipo unaweza ku-break the fast. So mdau, kama likizama saa tatu utakula saa 3. Ramadhan karim

    ReplyDelete
  22. AnonymousJuly 24, 2009

    Ewe mheshimiwa wa Jul 02.14 PM
    Wasema hakuna ku-break the fast mpaka jua likizama, jee unafahamu kuwa within the arctic circle around June 21st jua halizami abadan kwa masaa ishirini na nne. Part of extreme USA Canada etc are within the circle
    Wakatabahu

    ReplyDelete
  23. AnonymousJuly 25, 2009

    Assalaam Aleykum mdau was friday 0546 ukienda kwenye islamicfinder.org unaweza kupata muda wa kufungulia na pia ratiba ya swala zote.Natumaini hii itakusaidia. Assalaam Aleykum.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...