KWA MBELE
KWA NDANI
KWA NYUMA
mdau mwenye kulitaka aje alinunue. Limetoka japan. lina mwezi mmoja Bongo. ni aina ya Hino. Halina tatizo lolote. Limetembea 245,000km tu. Lina engine nyuma, 9880CC. Ni cylinder 6 straight. Lina kiyoyozi, mikanda na milango miwili ya umeme. linauwezo wa kubeba abiria 95. ni maalum kwa usafiri wa mijini (City Bus).

mwenye kuweza kulisimamia kama daladala litamlipa vizuri sana. liko katika hali nzuri sana. Limeshasajiliwa na kodi zote zimelipwa T 451 BAR.
Linauzwa 53M/- Tsh.
maelewano kidogo yapo.
mwenye kulitaka anipigie
0713 60 28 00
au
0784 60 28 00.
Asante
JB

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. Hicho kitu kinapanda mlima ile mbaya ila Mil. 53 kweli mimi sijui.

    ReplyDelete
  2. kaka mwambie mwenye hilo basi akaliuze ulaya! hayo mahela mengi sansana! labda kama ataliuza sh. mil kumi hivi! si mtumba? au? alafu tena litakuwa la kichina! alama yake kubwa kelele kama simu zao

    ReplyDelete
  3. we acha kutuingiza mjini kaka, hii dunia ndogo sana siku hizi. nipe dola 25,000 nikuletee gari kama hilo. acha wizzi

    ReplyDelete
  4. Dola elf 25 ni sawa na Tsh ngapi?

    Bro Michu, tangazo kama hilo ni kiasi gani kwenye blog ya jamii? Maana na mimi nina uza Bajaj, Vipanya na gari ndogo nyingiiiiiiiiii

    ReplyDelete
  5. Milango wa umeme ni hatari sana hiyo.

    ReplyDelete
  6. Baba UbayaAugust 26, 2009

    hilo bac na baraX2 za hapa bongo,foleni plus hiyo bei naona kama unaumiza saana.
    kuwa city bus ni hasara kwani itakuchukua hadi miaka 30 kuweza kukaribia kurejesha hiyo 53M.
    ila Mola akujaalie upate mteja na ikishindikana bac fanyia kazi wewe mwenyewe.teh teh

    ReplyDelete
  7. Abiria 95? mbona kazi? straphangers rider kufa hatufi cha moto tunakiona

    ReplyDelete
  8. Abiria 95? Embu anaglia seat arrangement yake then utakubali 95, yaani 20 wa kukaa afu 75 wakusimama, si bisbis hzo na pick poket

    ReplyDelete
  9. michu umebana comment yangu, dongo nini? powa kuhusu milango ya umeme sio tatizo ila sisi wabongo ndio washamba....

    ReplyDelete
  10. mdau uwanja fisiAugust 27, 2009

    kwa siku hesabu alfu 40 hadi 60..!!? hapo halijaharibika kwa bei ya milioni 53 ni sawa na kupaka rangi upepo!!!

    ReplyDelete
  11. Mmmh, Shughuli! Haya yetu macho!

    ReplyDelete
  12. Tutaendelea kufa tu kwa ajali zisizokuwa na sababu. Hii basi in uwezo wa kubeba abiria 20 hivi. Ndo sababu ina seats kumi upande mmoja na kumi au nane au tisa upande mwingine. Sasa hao wengine wanakaa wapi? au kuna seat zingine kwenye keria, na keria yenyewe siioni. Kudadeki Bongo. Yaani jamaa anataka kututapeli na picha ipo, jee kama angelikuwa anauza mbuzi kwenye gunia ingelikuwaje?

    Exagerated price, exagerated features, si ajabu ukaenda kuliona ukaambiwa gesi imeisha hivyo AC haifanyi kazi kwa sasa tumemtuma mtu afuate gesi town.

    Hapo nimekoma. Wananchi kuweni makini na hizi biashara za bongo, duuuh.

    ReplyDelete
  13. Waugwana, hilo basi lina sifa zote zilizotajwa na nyingine hazijatajwa, hakuna exaggeration hata kidogo. Hino ni kampuni kubwa sana ya magari Japan hususan magari makubwa. kwa bei ya $25,000 uweke na kodi ya TRA (takribani 40% ya hizo $25,000) weka na port charges, gharama za clearing agent, shipping line then utajua kama bei iliyotajwa ni ya kawaida au iko exaggerated! hili ni basi la kusafiri mijini hivyo nafasi kubwa ni ya kusimama sio kukaa. idadi ya abiria (95) ni kwa mujibu wa Japan Export Certificate. manake ni kuwa likiwa japan basi hili linaweza kubeba mpaka abiria 95. nasikia kwa wenye kuyasimamia vizuri hesabu ya kutwa ni kati ya 120,000-160,000 kutegemea na bei za mafuta na shurba nyingine za barabrani...JB

    ReplyDelete
  14. Acha kudanganya wananchi ww Anon wa01:30 nipo Japan kwa muda sasa sijaona msongamano wa abiria kwenye mabasi wa kufikia angalau watu 50. Sasa hili basi la kubeba watu 95 sijui lipo wapi katika Japan pengine kwenye makumbusho!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...