Kitendawili kilichotegwa takriban miaka mitatu iliyopita na aliyekuwa mkuu wa upelelezi wa jeshi la polisi,Mkoa wa dar es salaam (ACP) Abdallah Zombe na wenzake wanane wameachiwa huru sasa hivi katika mahakama kuu ya Tanzania.
Kwa habari na picha zaidi zinakuja

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 78 mpaka sasa

  1. Tunaheshimu maamuzi ya Mahakama kwa hatua hii, nini tunajifunza au ni kipi kinafuata baada ya kesi hii?

    ReplyDelete
  2. Mama yangu!! Natamani Mwalimu Nyerere angefufuka leo. Haya ndo mambo ya sheria za bongo. Bongo mambo tambarare babake!!!!!

    ReplyDelete
  3. Aiaseee hongera sana baba.......................................

    ReplyDelete
  4. Wacha tuone reactions za Watanzania sasa!!!

    ReplyDelete
  5. hiyo sio breaking news sababu aliachiwa ditopile mzuzuri, na sasa yuko wapi?

    ReplyDelete
  6. Duh?!!!

    Leo kweli tutakuwa wengi tunajikuta tukiiiga lile tangazo la Tigo kwa jinsi hukumu hii inavyoshangaza...

    ReplyDelete
  7. nilisema, nitalia na sasa wacheni nilie. nikimaliza nifute machozi na kushukuru 'wasomi' wa sheria.

    ReplyDelete
  8. Du karibu uswazi mwanangu. akabidhiwe tena ofisi yake

    ReplyDelete
  9. bongo tambarare, bado mramba na wadau wa epa. kweli wabongo kwa kutoa hukumu nje ya mahakama...sisemi

    ReplyDelete
  10. AMAAAA KWELI TANZANIA HATUNA SHERIA

    MTU AMEUA,ANAACHIWA HURU, BASI HAINA HAJA YA KUWA NA SHERIA.

    TUNA MLAAUMU SANA RAISI

    WATANZANIA HATUJA KUBALI KABISA NA HILO SWALA

    LAKINI MTU AIBE KUKU TU ATAFUGWA MIAKA KIBAO, KAMA HIVYO HAKUNA SABABU YA YULE MTOTO RAMA KUKA GEREZANI

    NA YEYE AACHIWE HURU

    ReplyDelete
  11. Hii haijatulia; lazima wanategwa kama Liyumba; kaka tutafutie full transcript ya hii judgement.

    ReplyDelete
  12. Huu Mfumo wa kulindana... Mwisho wake utakuwa mbaya!!!

    Arobaini zikifika, kila mwenye duku duku atalitolea kwenye makoo na mali za viongozi.

    Mifano ipo Ghana, Gabon, Guinea.. na nchi likuki zilizo shuhudia mapinduzi na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe.

    ReplyDelete
  13. ilikuwa changa la macho hilo. poleni wafiwa.

    ReplyDelete
  14. Hii ndiyo serikali ya Tanzania Bwana watu wanazuga zuga tu Dereva wa Mohamed Trans hata mwezi haukuisha kafungwa ilihali ajali huyu jamaa kwa kukusudia huru hureeeeeeeeeeeeeeee na Kikwete weweeeeeeeeeeeeeee ...

    ReplyDelete
  15. This is why our judicial system sucks. We have no hope and it is very embarrassing. Shame on us.

    ReplyDelete
  16. MMM KILA SIKU NASEMA HII NDIO TANZANIA ZAIDI UIJUAVYO HAYA SASA KIDUME KATINGA URAIANI

    ReplyDelete
  17. bro michuzi naona bongo tunapoelekea pabaya kama kweli hawa wakina zombe na wenzake wameachiliwa huru na sheria imewekwa kwa watu maskini Tanzania na ndio maana majambazi yanazidi kuendelea.

    ReplyDelete
  18. Duuuuuuuuuuuuuuh,Sasa muda wote walikua wanangoja nini kuwaachiaaaa???

    Aaaaangh!!!

    Kisoda2

    "Masikini haishiwi NDOTO"

    ReplyDelete
  19. MUNGU WANGU! TUMEKWISHA, YAANI MIJAMBIZI INARUDISHWA KITAANI. KAZI KWELIX2

    ReplyDelete
  20. SAFI KABISA, WALA MSIJIDANGANYE KULAUMU HII NDIO SYSTEM YA TANZANIA NI NZURI NA YA HAKI, KWA MAFISADI TUUUU hongera JK

    ReplyDelete
  21. Nilijua kitu kama hicho kitatokea tu

    ReplyDelete
  22. Hao waende wakajichimbie mahala, manake hapo nje ya mahakama watu tele wanawasubiri watolewe, sijui wanataka kuwatoa macho au ndio roho zao.

    ReplyDelete
  23. wanajamii wa blog mie kama cjaamini vile.duu thats life.

    carlos M

    ReplyDelete
  24. kaka michu ya kweli haya kaka, duh kama ndo hivi maafande watumaliza mtaani hakianani

    ReplyDelete
  25. HABARI NDO HIYO....WATANZANIA TUJUE ANGALAU SHERIA KIDOGO..KUA JUKUMU LA KUTHIBITISHA KOSA SIO LA MAHAKAMA NI UPANDE WA MSHTAKA IN THIS CASE POLISI...MAHAKAMA KAZI YAKE NI KWA KUTUMIA USHAIDI HUO (WA POLISI)KUTHIBITISHA "BILA SHAKA YEYOTE" KAMA WATUHUMIWA WALISHIRIKI..NA SIO USHAHIDI WA KIMAZINGIRA (TUME,MAGAZETI ,MA STORY ZA VIJIWENI NK...NK)..TUJIFUNZE WA TZ KUTOKANA NA HILI NA KITU HIKIHIKI TUNAKOSEA KWENYE ISHU ZA UFISADI
    NAWAKILISHA MDARESELAMA

    ReplyDelete
  26. MIMI SIKUBALII WALA NINI , SIKUBALIIII BWANA MIMI SIKU SIKUBALII HATA KIDOGO, A-A-A-AA MIMI HATAAA SIKUBALII KWANINI HIVI, MMM MIMI SIKUBALI AAAH WAPI SIKUBALIII

    ReplyDelete
  27. Hii nchi sasa tuwaachie wenyewe! Yaani hapo ni kiinimacho tu! So dissappointing!

    ReplyDelete
  28. Hivi ni kweliii au naota jamani, naomba mtu aniamshe pls!!!!!

    ReplyDelete
  29. Duu!!!!!!!! this is tooooo much!! What a shame!!!!

    ReplyDelete
  30. sorry to say " siipendi nchi yangu. thanx

    ReplyDelete
  31. Mwisho wa siku Mungu mwenyewe atashuka kuja kutoa hukumu ya haki, Hakuna mamlaka yoyoduniani inayoweza kutoa hukumu kama ya Mungu, Mimi sishangazwi na hukumu hiyo, kama umeau au haujaua wewe ni nani katika nchi hii? Mungu aaangaliwe wee ni nani bali anaangalia binadamu kwa usawa ule ule bila kuweka Classes. Haya tutayaona zaidi na zaidi hap hap ndani ya bongo. Wadau wenzangu mtakubaliana nami kwamba binadamu wachache wanaoweza kutoa angalau haki kidogo hata kama ni ndogo kama punje ya ulezi. Watanzania mnaiyona hukumu hii? kila mtu atakuwa na dukuduku lake juu ya hili. Napenda mimi mwenyewe Michael J.L niwakilishe

    ReplyDelete
  32. ndio maana wabongo humaliza biashara mapeemaaa wanachukua sheria mkononi basi shughuli nyingine zinaendelea!!!

    ReplyDelete
  33. Tanzania, Tanzania
    Nakupenda kwa moyo wote
    Nchi yangu Tanzania
    Jina lako ni tamu sana
    Nilalapo nakuota wewe ... Read More
    Niamkapo ni heri mama wee
    Tanzania, Tanzania
    Nakupenda kwa moyo wote

    ReplyDelete
  34. wallah kwa niaba ya Wananchi wa Kilombero tunasema hivi HUYU ZOMBE HATUMSAMEHI NA TUTAMCHUKULIA HATUA MIKONONI MWETU LABDA AKAISHI MBINGUNI, SATU!!

    ReplyDelete
  35. Kama mambo ndio hivi basi elimu ndio jawabu: (http://wachumi.blogspot.com/).

    ReplyDelete
  36. Duh..hii ilikuwa bonge ya tamthilia..And they lived happily ever after..

    ReplyDelete
  37. TANZANIA HIYO, SISHANGAI KABISA. NAKOSA HATA AMANI. HIYO NCHI BORA NIFIE HUKUHUKU NILIKO. NAMSHUKURU MUNGU KUZALIWA HAPO, LAKINI SITAREJEA NCHI ISIYO NA HAKI, IMEJAA RUSHWA, KUJUANA, WAKUBWA WANA SHERIA MKONONI NK.

    Mwananchi.

    ReplyDelete
  38. ............imekaa vizuri hii ndio bongo bwana darisalamu. kudadadeki bonge ya chenga.........
    Kwishneyiii...
    Kama kawaida changanya madawa.
    Imekaa vipi hii

    ReplyDelete
  39. Hiyo ndio tofauti ya sheria na haki, wameachiwa kwa mujibu wa sheria!!!

    ReplyDelete
  40. Kiroboto, Mikanjuni, TangaAugust 17, 2009

    Kila mmoja alijua kuwa mnyonge hana haki tokea siku ya kwanza ya kesi hii. Ufisadi na rushwa vimetawala kila kona ya nchi yetu hata kwenye vyombo vya sheria ambavyo vinawasaidia mafisadi zaidi kuliko wanyonge wenye haki zao na kuishia kudhulumiwa.
    Hongera mahakama kwa kuidhinisha dhuluma dhidi ya wanyonge

    ReplyDelete
  41. NAAAAM!
    MBINGU NA JESHI LAKE LOTE VIKAMALIZIKA NA HUKUMU PIA IKATOLEWA!
    IKAWA ASUBUHI IKAWA JIONI SIKU YA HUKUMU:

    ReplyDelete
  42. ÙˆَÙ…َÙ† ÙŠَعۡÙ…َÙ„ۡ Ù…ِØ«ۡÙ‚َالَ Ø°َرَّØ©ٍ۬ Ø´َرًّ۬ا ÙŠَرَÙ‡ُ

    The way I look at it is that the real courtroom is before Him where you will be rewarded for everything you did no matter how small or big
    Wakatabahu

    Û¥

    ReplyDelete
  43. ndugu zangu , subirini hatima ya albino kanda ya ziwa muone ... ikifuatiwa na baba wa pacha mbili ufukweni alafu muone uwiano

    kang`aaa!!!!Tanzania zaidi uijuavyo !!!

    Tufunge safari uchaguzi 2010 hureeeee...

    ReplyDelete
  44. Sikuamini macho yangu hii inauma sana kuachiwa wauwaji wa wazi wazi kabisa. Kwa hilo sidhani kama tutakaa salama. Tume iliyounda ya Jaji Kipenka ilionekana kwamba hao watu waliuwawa na nani sasa kama hao wameachiwa?????????Lakini MUNGU YUPO NA YEYE NDIYE ATATOA HUKUMU YA MWISHO. Poleni sana wafiwa.

    ReplyDelete
  45. jamani 2010 kweli CCM wabaki? kama mambo ndo haya...katika utaratibu huu napendekeza alex masawe awe raisi,zombe makamu wa raisi waziri mkuu rostam aziz, lowassa akajenge chama imekaaje hii???

    ReplyDelete
  46. TATIZO WA TA TUMEZOEA KUWA NA HABARI ZA MAGAZETI NA VIJIWE, Tupate hiyo judgement ndo tuamue, me binafsi namkubali sana judge Masati na ni judge of court of appeal, tuone reasoning ya judge ndo tuamue kama kachemka au la.....kumbukeni pia criminal charges u have to prove beyond reasonab;e doubt.....so watanzania tuache habari za kijiweni na za magazeti, tukome kutuhumu watu wana hatia wakati hawana...shame on you all ambao mnafwatilia habari za vijiweni na hamna data zozote hasa nyie wa TZ mnaojifanya mpo nje ya nchi mnajifanya mnajua wakati hamna LOLOTE


    MDAU TZ

    ReplyDelete
  47. Next to be free is Liyumba, hii ndo bongo bwana. Wenye nazo wapo juu ya sheria wakati wote

    ReplyDelete
  48. aghhhrrrr!!!!

    ReplyDelete
  49. ALIYESEMA MAJAMBAZI WAMERUDISHWA MITAANI NI KWELI KABISA. KUMBE JAMBAZI MAFIA MKUBWA ANAACHIWA KUJA KUZIDI KUFANYA UFISADI WA UUWAJI. ILA TUSIMUHUKUMU MTU HATUWEZI KUJUWA MOLA NDIO ANAJUWA. KAMA KAFANYA BASI ATALIPWA HAPAPA. PAZI.

    ReplyDelete
  50. Bwana ametoa na Bwana ametwa,jina la Mungu na lishukuliwe kwa kila jambo.HUKUMU YA MWISHO MTOAJI NI MUNGU PEKE YAKE JAMANI.

    ReplyDelete
  51. duuuu jamani kweli serikali inapoelekea pabaya sana na sheria imewekwa kwa watu maskini, babu seya na wanaye wanahatia kifungo cha maisha jela,dereva wa mohamed trans anahatia miaka 30 jela na zombe na wenzake wameuwa kwa makusudi eti hawana hatia na wameachiliwa huru! ivi tunaelekea wapi jamani?ccm inajiwekea wakati mgumu huko mbeleni kwani inaoneana aibu sana na kuongoza nchi wamechoka.

    ReplyDelete
  52. Ze komedi waliwahi kuigiza hii kesi ya kina Zombe ina mazingaombwe nakumbuka yule mpoki alisema "mi nina mdogo wangu hakufanya mtihani wa form 4 akaenda kwa babu ukatumwa mzinga NECTA mbona matokeo yake yametoka amefaulu kwenda form 5"

    ReplyDelete
  53. TUNAPOTEZA MUDA KUFIRI KUNA FISADI ATAONJA JELA TANZANIA,JELA KWA SISI WANYONGE TENA HUKUMU UTOLEWA KATIKA MWEZI MMOJA TU.

    ReplyDelete
  54. sheria na haki vitu viwili tofauti.
    wewe ulitegemea afungwe yeye alitegemea atoke sasa hapo jipime uko sahihi au?

    mimi najionea sawa tu kwakuwa sikuwa naye nilalamike kuwa alikosa, au tunahukumu kwa kukasirishwa na mashtaka? angalia upande A pia angalia upande B yote yawezekana tujenge nchi yetu tusifuate ya mtu mmoja kuna watu milioni 40 wanatutegemea.

    ReplyDelete
  55. WASIOPENDA HAKI WAKO HASI HATA KOMENTI.

    HIVI HAIFAI ZOMBE ASHINDE?

    ReplyDelete
  56. It’s not hard to see the frustrations of my fellow countrymen/women! And no one can blame them for that because it has been too long and lots of cases have been judged under the same ‘kangaroo court’ and nobody appeared to change something. It's just business as usual!

    Is it our legal system or people who implement it (or all of them) to be blamed for this? Or maybe our politicians?

    This judgment, apart from other things, it clearly shows inconsistency in our legal framework which is allowing some ‘potential criminals’ to slip off the net.

    Of course, they say; “you are innocent until proven guilty” but how many times we have seen 'people without power' (normal citizens) became “guilty until proven innocent”?

    In my memory of following these ‘high profile cases’ (cases involve big hogs) in Tanzania, the verdict of these cases are always known even before the case started!


    Tanzania of today is not the one of 40 years ago! We have lots of so called ‘intellectuals’ in different areas. Most of our today's MPs are graduates and some with the highest level of education qualification, PhD degrees but still we can’t move on in anything! WHY? What's the point of being over proud of a first class degree while you can't make any change to help your suffering people? Something’s wrong somewhere!


    I think it’s time for our politicians and intellectuals to do something in our legal framework in order to save it from being perceived 'BIAS' i.e. "it’s only there to serve a ruling class", as it's for the case NOW.
    ______________________________

    Mzee Wauyagauyaga

    ReplyDelete
  57. Huo ndio utawala bora lakini yana mwisho hayo ni damu ya mtu na kama hayana mwisho everythings goes around will comes around leo judge katoa hiyo hukumu kama ni haki hawakuua basi kheri yake na kama wametenda basi malipo kwa mungu.wafiwa sala zenu ni muhimu na mungu ndio anajibu lenu inshaallaah kama hukumu si hapa dunia hata akhera wataikuta huko hakuna wakili mjema wala mjeuri!

    ReplyDelete
  58. Michuzi, my experience so far, this is the post that will have fetched more comments than any other ever!! the number of comments will be record breaking, keep a close eye and observe this!!
    sidhani kama huwa michuzi una kawaida ya kurecord topics zinazovunja record kwa kupata responses nyingi kuliko nyingine. ni vizuri ungekuwa unafanya hivyo ni vizuri kwa historia ya blog yako pia. na pia itakuwa vema topic itakayovunja record ya kupata comments nyingi zaidi katika mwaka husika uwe unairusha mwisho wa mwaka na kuwafahamisha wadau kuwa hii ndo topic iliyovunja record kwa kupata maoni mengi zaidi ya topic yoyote katika mwaka husika. inavutia.

    ReplyDelete
  59. HAPO BADO..

    NASIKIA KK ANATAKA KUMTEUA ZOMBE MKUU WA MKOA.. AU KUMPANDISHA CHEO KWENYE UPOLISI...
    BONGO SYSTEM

    ReplyDelete
  60. Wamesamehwa duniani,lakini hukumu ya kweli inawangoja!

    ReplyDelete
  61. Liyumba, Chenge na wengineo nanyi mtaachiwa tu wala msiwe na presha....bongoland wanaofungwa ni wale wachovu tu...wenye pesa kutesa si kwa zamu bali ni daima. Wahenga hawakukosea waliposema PENYE UDHIA PENYEZA RUPIA

    ReplyDelete
  62. OK. Marehemu walikamatwa Sinza na hilo kundi la Zombe (polisi), wakiwa mikononi mwao na pingu wamefungwa wakakutwa wameuwawa kwa risasi huko msitu wa Pande. Chini ya ulinzi wa Polisi Zombe na kundi lake, hawa ndo watu wa mwisho kuwaona marehemu wakiwa hai tena chini ya ulinzi wao, wanaachiwa huru, hawana hatia.

    Jaji ameamua vipi? Yaani sioni maelezo waliyotoa yanayoeleweka kukana kosa hili. Imekuwaje? Au tuseme kuwa marehemu wakiwa chini ya ulinzi wao, muujiza ukatokea, wakakutwa msituni wamepigwa risasi. Zombe na wenzake wakasema hao ni majambazi.

    I mean, how come? Mtu yupo chini ya ulinzi wako, hajiwezi kwa kuwa umemfunga pingu, unapaswa kumpeleka kituoni, kesho anakutwa kauwawa msituni, jaji ana onaje kuwa Zombe na wenzake hawana hatia? Wamepigwaje risasi? I am pissed off!!!!

    Hii ni kesi wala haikuhitaji kutumia miaka mitatu wala siku nne.
    We Tanzanians are so fucking stupid.

    ReplyDelete
  63. Imekaa vibaya, hii bado haijatulia. Kali P upo wapi?

    ReplyDelete
  64. Jaji na wazee wa baraza, hivi hawa wazee wa baraza elimu yao ikpo vipi?

    ReplyDelete
  65. Ndugu zanguni hapa ndipo unapokuja ukweli wa mambo kwamba sheria zipo kwa ajiri ya kutetea na kuwalinda watawala na siyo kutetea wanyonge kama inavyonadiwa. Kiukweli hili ni suala la kisheria zaidi, according to the letter of the law watuhumiwa hawana hatia na jamhuri imeshindwa kuprove hilo over the court. But kihualisia watuhumiwa wanayakujibu, hata kama wameshindwa kujibu mbele ya mahakama, watajibu mbele ya mwenyezi mungu. Na hii inaonyesha jinsi gani serikali isiyokuwa makini, wanakurupuka kila kukicha imetumia gharama nyingi kwenye tume ya jaji Kipenka na kutoa report kwamba Zombe na wenzake wanachakujibu mbele ya mahakama. Lakini leo hii, serikali hiyohiyo kupitia mahakama inakwambia hawana hatia. It reach a point tunajiuliza umakini wa serikali yetu hatupati majibu!! Sasa umefika wakati ndugu zetu tujaribu njia nyingine ya msingi na sio serikali hii ya chi chi M.
    Asanteni

    ReplyDelete
  66. Anon wa Mon Aug 17, 05:27:00 PM

    nadhani hujui yepi yaliyojiri na kesi ya kina babu seya, ni kweli walilawiti watoto wetu na wala hawakusingiziwa. Tuache sheria ifanye kazi yake sio kuongea tu humu labda kweli kina Zombe wako innocent

    ReplyDelete
  67. Wewe unayemlilia Nyerere wacha kutaka kutuletea ujinga wako hapa.

    Nchi inaendeshwa kwa mujibu ya sheria na huo ndio uamuzi wa mahakama.

    ReplyDelete
  68. KUSEMA UKWELI KAMA MTU ANGEINGIA MOYONI MWANGU ANGEONA UCHUNGU NILIO NAO JUU YA NCHI YETU KWA KWELI HII SIO HAKI KABISA TENA KABISA,KILICHO BAKI SASA KUKAA HUKU HUKU UGHAIBUNI NISIJE NIKARUDI BONGO NIKAUA MTU BUREE.HIII.HAPANA SERIKALI IKO WAPI??CCM IKO WAPI KAMA CHAMA TAWALA.MAMBO YANAKO ELEKEA NI BURUNDI NA RWANDA 1994 WE SUBIRI MTAONA TU.NCI INANUKA UCHAFU.JAMANI JAMANI MWALIMU HEMBU FUFUKA HATA KWA DAKIKA MOJA UONE.

    ReplyDelete
  69. Nahofia kusema kuwa hili ni pigo kubwa kwa utawala wa sheria nchini. Ni wazi kuwa hukumu hii imemaliza kabisa imani ya watanzania kwa asasi za utawala na utoaji wa haki nchini. Itachukua muda mrefua na gharama kubwa kuwafanya watanzania walio wengi haswa wale wa mjini kuamini tena kuwa mahakama zetu zipo kwa ajili ya kutoa haki kwa kila mtu na sio kwa wenye nguvu tu.

    Hata hivyo naamini wa kulaumiwa hapa ni upande wa upelelezi na ushahidi (polisi na waendasha mashtaka)kuliko mahakama.

    Tusishangae kuona ule utamaduni tuliojijengea wa KUCHOMA tuwaitao vibaka ukawageukia tuwaitao MAFISADI...

    Inasikitisha kuwa kuna wengi waliokuwa wakishangilia "ushindi" ambao ni wazi ndio cheche za mwanzo za mlipuko mkuu ambao watanzania tumekuwa bize tukiuandaa.

    omarilyas

    ReplyDelete
  70. watanzania wengi hatuna utamaduniwa kujifunza, ni wavivu wa kudadisi ni waoga kupindukia,tungekua na uelewa wazaidi wa sheria tungeelewa nini kinaendelea,lakini kadri tunavyoenda elimu inazidi kuwa kubwa tutakuja kuelewa nini cha kufanya.

    kwa sababu wengi hatujui sheria ndio maana hatuna uhakika kama maamuzi ya hii kesi yako sawa au sio sawa.

    mungu ndio muamuzi wa kweli na ndio maana akaweka kifo kwa wote kuonyesha usawa.na malipo ni hapahapa duniani

    asanteni



    asante

    ReplyDelete
  71. nchi yetu mpk kesho iko chini na itaendelea hivo kwakuwa hakuan justice..marekani au nchi nyingine yoyote yenye maendeleo(sio za africa)wanafata sana haki hata uwe MP kudadekiii hata raisi ukimess up ur down! sisi huku mtu akishakuwa na madaraka bass anaambiwa tunazuga zuga tu humu baba utatoka tu usijali! mi kwakweli &*(&£%£%£&*£&£*!!!!!!(natukana sanaaaaaa)

    ReplyDelete
  72. NIMEKASIRIKA.IM PISSED OFF.sina imani na nchi yangu! PERIOD

    ReplyDelete
  73. Haaaa,,,,, mambo gani haya jamani sasa tunaogopa kurudi nyumbani bora tutafute uraia huku tuliko make sasa Tanzania nchi ya amani sasa itakuwa nchi ya vurugu. Kweli huyu jamaa kaachiwa sasa mda wa miaka mitatu ni nini walichokuwa wakipeleleza ata mmoja wao hakuna mwenye makosa mahana wale masela walikufa kwa miujiza.. Poa tu ngoja tusubiri atima ya Tanzania

    N.B Dereva kasababisha ajari ata mwezi bado kalamba 30 jela hakuna ata investgation yoyote,,,

    Mda,,,, Malaysia

    ReplyDelete
  74. Nchi yako au yaMAFISADI? unajipa moyo,wenye nchi uwaoni,KAUWE WEWE MBUZI TU UONE KAMA NCHI YAKO!

    ReplyDelete
  75. NA ZE KOMEDI ORIGINAL YETU NDIO IMEISHIA HAPO...!WADANGANYIKA MPOOO....?!

    ReplyDelete
  76. SITAHAMA TANZANIA..NITAFIA HAPA HAPA..NAOMBA MUNGU NISHUHUDIE NA IKIBIDI NISHIRIKI KWENYE KUTAFUTA HAKI ZA WANYONGE...HAIJALISHI NI MBINU ZIPI..ZIWE ZA KUMWAGA DAMU AU VYOVYOTE VILE..HT YESU ALILAZIMIKA KUMWAGA DAMU ILI WENGI WAKOMBOLEWE!

    SASA NI HV, ZIHARAKISHWE HT HIZI ZA KINA MRAMBA, YONA, RICHMOND NA EPA..WAFUTIENI TU MASHTAKA KWANI KWA HALI ILIVYO NDIO MWELEKEO..LOWASSA ANAKULA MATUNDA YA WAZIRI MKUU MSTAAFU JAPO ALIJIUZULU KWA TUHUMA ZA UFISADI!

    LAKINI TUNAONA..HAYA YANAFANYIKA HADHARANI, KUNA HAJA YA KUANZISHA MOVEMENT ZA CHINI KWA CHINI ILI KUWEKA MAMBO SAWA KAMA WALIVYOFANYA WAMAREKANI WEUSI WAKATI WA KUDAI HAKI ZAO..

    KINACHOFUATA NI kujitoa muhanga kufanya 'kitu mbaya' tena mchana kweupeeee kila mtu akiona ili tujipeleke wenyewe polisi na tuhukumiwe on the spot! Ili ndio mahakimu waonekane wanafanya kazi kiproffessional zaidi..

    Ditopilie aliua kweupee mchana mbele ya umma, lakini MUUZA SURA JK alimpa pole na kumwambia ''tuko pamoja ndugu yangu katika hili'' na aliachiwa mchana kwa dhamana..

    Na ndivyo ilivyo, sheria inafanya kazi kwa maskini tu na wasio na watu wa kuwasemea..na ndio wamejaa magerezani, kesi za kuku vibaka wakwapuaji na wengine wa kusingiziwa! TUFANYEJE WATANZANIA?

    HAWA JAMAA WAJITAHIDI WATEMBEE FULL MITAANI TUTAKULA NAO TU NA TUTAJIPELEKA WENYEWE POLISI TUHUKUMIWE, TENA WASIUNDE TUME ZA KUPOTEZA HELA..MAKE SIYE WADOGO WADOGO, VIKARAGOSI NA MASKINI
    HATUUNDIWI TUME..sasa basssi!

    onyo: CCM MJIANDAE..TUTATAKA MAJIBU YA YOTE HAYA KABLA YA KWENDA KWENYE VITUO VYA KUPIGIA KURA MWAKA 2010!

    ReplyDelete
  77. Mwenyezi Mungu apewe sifa, natoa salamu zangu za rambirambi kwa familia za wafia.Pia nawapongeza mawakili wa pande zote mbili kwa kutimiza wajibu wao !!!!!! Na nawaomba watanzania wote kwa ujumla kuwa makini.
    Sasa watanzania wenzangu tujifunze kwa vitendo, leo tumeone hiyo kesi ilivyo endeshwa na matokeo yake tumeyaona,. Swali langu ni je tumulaumu nani ? kama siyo sisi wenyewe,. Uongozi umekuwa wa kujuana tokea siku nyingi, kulindana ndo usiseme, hususani ukiangalia upande wa vyombo vya usalama au walinda amani kama wanavyoitwa, mara ngapi wametumia nguvu kupita kipimo au wanawapiga raia wasio na hatia au kosa lolote lile (kumbuka ile ishu ya Arusha- watu wakishushwa kwenye daladala na kupewa kibano-) hapo ndo tunaweza jiuliza haki za binadamu nini maan yake na masingi wake upo wapi kwenye sheria au kwenye ubinadamu ? na jibu nani atoe kama siyo sisi wenyewe –watanzani waipendao nchi yao.
    TUSEME HAPANA KWA WAUAJI- kwa kuondoa viongozi wazembe katika taasisi zote. Hiyo ni kazi yetu vijana wazee haooooo wanaelekea kustaafu, tuanze kazi ili watoto wetu siku moja wahukumiwe kwa haki bila kuangalia uwezo wao kiuchumi, madaraka yao au uhusiano wao ni vigogo, bali wahukumiwe kulingana na makosa yao na kwa mjibu wa sheria za nchi.

    ReplyDelete
  78. Kesi ya Nyani, kapewa nyani.
    Hivi kweli watanzania na akili zenu finyu mnadhani kuna muendesha mashtaka (Polisi) gani hapo Bongo anaweza kupeleka ushahidi mahakamani wa kumtia hatiani bosi wake (Zombe). Hawa jamaa wote wameweka mtandao wa kulindana, kuanzia IGP mpaka mshika kirungu kule chini. Huwawezi kutosana kwa kuwa wote wachafu na wanasaidiana kuficha siri zao. Washenzi watupu mbwa hawa.

    Hu si uamuzi wa mahakama, bali ni uamuzi wa jaji alieendesha hiyo kesi. Sheria wala haki havijafuatwa hapa bali pesa na kujuana kama si kuogopana.

    Tatizo la Bongo, Jaji, wazee wa baraza, muendesha mashtaka, wakili wa utetezi, watuhumiwa na serikali yao ukiangalia kwa umakini utaona kuwa wote wana uhusiano wa karibu kabisa au by reference.

    Naungana na anony hapo juu anayesema, hawa walikuwa ndo watu wa mwisho kuwaona marehemu na zaidi wakiwa chini ya ulinzi wao, motive ilikuwako ambayo ni money, muder weapons were there, the bodies were there. Inakuwaje waachwe huru? Halafu huyo jamaa wanayesema alitoroka polisi hata hawawezi sumbuka kumtafuta kwa sababu hawatakuwa na kisingizio tena, wanajua alipo.

    Hivi mali za marehemu, madini na fedha zipo wapi sasa? Au nazo ndo zimedhulumiwa kama walivyodhulumiwa haki yao?

    Uhakika ni kuwa Bongo mapinduzi hayawezi kutokea hata siku moja, wananchi wamegawanyika makundi makundi. Wengi ni waoga sana, wengine hawajui kesho wataionaje, hivyo wamekuwa tegemezi mno kwa hao wanaowakandamiza (Kumbuka mtu akikandamizwa sana, humtetea mkandamizaji daima), wengine ndo ma mbumbumbu hawajui A wala B, wengine wajuaji mno (hujifanya) lakini yote tisa kumi ni kuwa waTZ wengi ni wabishi mno tena hubisha bila kuwa na data zozote.

    Hivyo, watawala wenu wataendelea kuwakandamiza daima na hakuna lolote mtafanya kuondokana na hali hiyo, mbuzi ninyi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...