Mkuu wa mkoa wa naniii.. pole kwa kazi. Kwa mara ya kwanza nami nashiriki katika kujulisha jamii kuhusu inchi yale yatendekayo nje ya nchi yetu. Naomba niwatumie watanzania wenzangu picha mbili hizo kati ya nilizozinasa katika jumba la makumbusho la Taifa hapa London. Nilifurahi sana kukuta moja ya maonyesho ya africa, nchi yetu ilikuwa imetengewa ka sehemu kwenye vitu mbalimbali na wazungu wengi kutembelea na kupiga picha. Kwa upande mwingine kulikuwa na film fupi inayoonyesha jinsi gani kina mama watumiavyo kanga, kama uonavyo huyo mama nilimnasa akiwa anapiga vigegele huku akikimbia huko na kule. Kwa kweli ilikuwa furaha na ningependa bwana Michuzi niwashirikishe na watanzania wenzangu kuwa hata sisi tupo katika mataifa. Mzee mpya wa libeneke



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ni jambo zuri sana kuwepo na makumbusho ya namna haya kwani hata unaweza kukumbukia tulipotoka lakini ningependa zaidi kuwepo na vitu mbali mbali tulivyotumia wakati huo kwa mfano hapo naona khanga mbali mbali na vitenge lakini sijaona kitenge cha mawingu ambacho ndio kilitamba sana wakati huo...mdau uholanzi

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...