Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Rais - Mazingira, Mh. Dkt Batilda Salha Burian, Akifuatilia Hotuba ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban ki - Moon, katika ufunguzi wa Kongamano la ulimwengu la Mazingria linalofanyika katika ukumbi wa Convencia, jijini Incheon, Korea ya Kusini. Picha na habari na mdau Evelyn Mkokoi

BAN KI –MOON AFUNGUA KONGAMANO LA MAZINGIRA

Dunia inaweza kukabiliana na Matatizo yanayoikumba kama vile umaskini katika nchi zinazoendelea, njaa na magonjwa bila kuharibu Mazingira
Hayo yameelezwa leo na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki-Moon wakati akifungua kongamano la kimataifa la mazingira Nchini Korea ya Kusini.
Bwana Moon ameeleza kuwa uharibifu wa mazingira unapelekea Upungufu wa Maji ambao unaathiri idadi kubwa ya watu na kuleta madhara ya magonjwa kama vile utapiamlo.

Pamoja na kuipongeza Korea ya Kusini kwa kuwa Mfano bora kwa utunzaji wa mazingira, ameiasa pia kuongeza jitihada zaidi katika kukabiliana na mabadiliko ya Tabia nchi.

Katibu Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa, aliongea kwa kusema kuwa nguvu za pamoja zinahitajika kutoka katika sekta zote za jamii, ili kukabiliana na suala zima la uharibifu wa Mazingira.

“Nitaalika Viongozi wote wa Dunia ili kujadili tatizo la Mbadiliko ya Tabia Nchi.” Alisema.

Bwana Moon alisisitiza kuwa , Nchi zinazoendelea ni lazima ziwe na mipango na matendo ambayo ni lazima yapimike na kuripotiwa ili kufikia malengo ya kukabiliana na suala zima la uharibifu wa Mazingira.

Kongamano hilo la siki mbili la Mazingira litajadili pia suala la sera mchanganyiko zitakazoweza kutumika kushughulikia suala zima la matumizi ya Nishati na usimamizi wa mazingira kwa ujumla.

Kongamano hilo linahururiwa na wataalam mbali mbali wa masuala ya mazingira na Mawaziri wa Mazingira kutoka nchi mbali mbali Duniani ikiwemo Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. hongera mama kwa kuchapa kazi, nyinyi ndio wanawake tunaowahitaji katika Tanzania tulionayo, sio mafisadi wanaoiangamiza nchi.
    kila la kheri mama.

    ReplyDelete
  2. Wee Anonymous 05:09:00

    Wacha kusema mambo usiyo yajua na kumwaga misifa ispostahili- Angalikuwa ni Waziri MAKINI tena mwenye dhamana ya Mazingira asingesubiri Watanzania na mifugo yao wafe na wengine kuathirika vibaya kule kwenye Mgodi wa Barrick Northern Mara - bado mpaka leo anajikanyaga kuwachukulia hatua wachafuzi hao wa Mazingira. Look "No research No right to speak" Good Day!

    ReplyDelete
  3. tatizo lenu mwosha kinywa unasubiri hatua zichukuliwe kwa mkono, kiongozi hakurupuki tu. busara lazima, hata hivyo utunzaji wa mazingira unaanzia kwa wananchi wenyewe........kua na busara wewe.

    ReplyDelete
  4. DADA BATILDA UNANIVUTIA SANA KWA HIJAB YAKO SAFI.UNAPENDEKEZA NA INAKUPENDEZA.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...