ganda la mdau wa maputo



Mambo Issa,
Nimekutana na huyu mjamaa
Kioma Siyanga Timu Ngayega
Maputo Mozambique wiki iliopita ni mfanya biashara, yeye anasema baba yake alikua Mtanzania mwanafunzi huko Maputo na alimtelekeza na kurudi Dar baada ya yeye kuzaliwa na kuwa registered huko na baba yake kwa majina hayo.


Anaomba Globu ya Jamii imsaidie kutangaza ilu kumtafuta mzazi wake au familia ya karibu.


Mdau Dar

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. mdau wa maputo mbona umeacha mambo muhimu kyataja? ilikuwa useme jina la jamaa na la baba yake ili iwe rahisi ketu kama tunamjua kuunganisha. pia mwaka ambao baba yake alikuwa maputo ni muhimu.kutaja tu kuwa mdau wa maputo anamtafuta baba yake haitoshi. toa maelezo zaidi.

    ReplyDelete
  2. NAJISIKIA HUZUNI NYINGI NILIPOSOMA HII MESSAGE,

    tabia hii ya wanaume kutokuwa na utu na ubinadamu, baadhi wameuvua ubinadamu sijui niwaite nini ??????
    hii imekuwa ni tabia ambayo wanaume wengine huwafanyia wanawake na watoto wao ila akiona ana future (mwelekeo wa kimaisha mzuri hasa!! FINANCIAL ) utamsikia na sii huyu tu kuna wanachuo wengi huingia mitaani na kujiita majina kama economics, surve, save, na mengine mengi, anapomaliza chuo anamwacha mama wa mtaani na mtoto anapokuja chuo basi kuuliza inakuwa kaziiiii kweliiii,

    tuwasaidie wakina mama, pia jifikirie je ingekuwa wewe humjui baba au leo hii umesoma unamuuliza mama, baba yangu anaitwa nani na akakujibu economics how do you feel!!! jamani ubinadamu !! huo ni uchungu na simanzi kubwa usipomjua BABABABABA!!
    mimi nina Baba na Mama ni watu wazima nami ni mtu zima but najikuta nadeka hata kama hawana pesa.

    TUKEMEE TABIA HII
    KAKA POLE SANA. I HOPE BABA YAKO HAKUITWA LECTURE ROOM. KARIBU BONGO

    ReplyDelete
  3. Ni vizuri ukiweka majina yake pamoja na ya mama yake. Na hata chuo alichosemea baba yake

    ReplyDelete
  4. jina au majina?

    ReplyDelete
  5. sasa huyu jamaa jina lake nani? na baba yake mtafutwa anaitwa nani? alisoma maputo chuo gani?? alirudi bongo mwaka gani? tupe dataz tukupe baba yake....

    ReplyDelete
  6. Kama mimi ni huyo Baba...nikisoma hapa mtoto wangu amenitoa kwenye Michuzi kuwa "nilitelekeza" naweza nikajikausha kabisa...wala nisijulikane.

    Ujumbe wangu; hii habari imetolewa vibaya kwa kila kitu.

    ReplyDelete
  7. Kwa kufuata majita ya mdau, ni dhahiri kuwa yana asili ya Mtwara, Lindi, Msasani-DSM na Tanga ambako wenyeji wa Mtwara alihamia.

    Kwa vile mwaka wa kuzaliwa unaonekana wazi ktk kitambulisho, na majina yanaonekana 'Kioma Si-Yanga Taimu Ngayenga' ni sawa na ya watanzania wenzetu wa kusini, lazima kuna ndugu, jamaa na marafiki wa baba wa huyu kijana watajitokeza kumfahamisha kuwa kijana wake anamtafuta.

    Kumbuka vita vya RENAMO-FRELIMO Tanzania ilipeleka askari wengi na 'wanausalama a.k.a wanafunzi' kusaidia Frelimo isiondolewe madarakani Mozambique.

    Mdau
    Chakumwenda Chibiriti
    Mahuta-Shimoni
    Mtwara.

    ReplyDelete
  8. Duh hilo jina limekaa kimpira mpira "SIYANGA TIMU" bali NI SIMBA YA MSIMBAZI.(jamani utani tu wadau msimind)

    ReplyDelete
  9. lakini mbona umeweka ID yake humu. Kesho utakumta Mnigeria naye anayo hiyo license.

    Back to the topic hayo tutayaona mwaka 2012 na kuendelea vijana wa OH,MD and TX. Wengi wao wakishajua child support inanukia wanahama State

    ReplyDelete
  10. unasema mwaka baba yake alikua huko si ungalie huyu anamiaka mingapi tu jamani. Leseni inasema 26/5/81 huyu baba yake alikua miaka ya 80

    ReplyDelete
  11. anafananafanana na bambo!!!

    ReplyDelete
  12. SINA MAKOSAAugust 13, 2009

    LAKINI KAMA VILE ANAFANANA NA PHILIPO MANGULA! SIJUI NYIE MNAONAJE WADAU.

    ReplyDelete
  13. Naungana na mdau hapo juu kulingana na aina ya majina ya huyu kijana inaonekana kabisa kuwa huyo baba, atakuwa, kati ya makabila ya kusini. ni mmakonde ama mmakua ama mwiyao. Ninaomba kati ya makabila haya kama kuna ukoo wa majina hayo ya kijana, basi mjiulize mara mbili ni nani alikwenda uko na mtapata jibu. mchukueni kijana wenu,kwanza anaonekana shupavu na ana kibarua chake si mnaona lesseni ya gani?

    ReplyDelete
  14. Lamuhimu nikusaidiwa huyo kijana kama kuna watu wanamuelewa baba yake binafsi imeningia huzuni kwa huyo kijana kutomjuwa baba yake isitoshe wakuu hilo jina ni miongoni mwa majina ya Tanzania ?kwani kwa upande wetu huku zanzibar naweza kumwambia jamaa hatuna mtu mwenye jina kama hili na badala yake atafute upande wa wapili pia mnaweza kumsaidia kueleza ni jina la kabila gani .

    ReplyDelete
  15. Kaka yake ni Kaijage wa TFF asikwambie mtu

    ReplyDelete
  16. Atakuwa ni mwanangu kwa sababu amefanana na mimi na pia nilisoma Mozambique na nilikuwa na 'vishindo' wakati niko skuli.

    ReplyDelete
  17. Kama kweli baba wa huyu kijana alikuwa mwanafunzi huko Mozambique basi ubalozi wa Tanzania nchini Mozambique unaweza kuwa na kumbukumbu na kujua alitokea mji gani kabla ya kwenda huko na kama alikuwa mfanyakazi watajua alitokea ofisi gani.
    Nampa pole sana. Asikate tamaa hata mie baba angu alitenekeza nikiwa mchanga... aliniacha na mama na kurudi kwao Zimbabwe lakini juzi juzi kaja kunitafuta baada ya miaka 43 kupita. Iko siku Mungu atamkutanisha na baba yake

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...