Miss Redds Ilala 2009 Sylvia Frank Shally (pichani chini) ambaye pia ameibuka kuwa Miss Redds-Michuziblog Photogenic. Sylvia kajishindia shilingi laki 5 ambazo zimetolewa na Redds Premium lager

mgeni rasmi alikuwa waziri wa nishati na madini mh. william ngeleja (wa pili shoto) akila pozi na redds miss ilala 2009 pamoja na mabosi wa masomo wa TBL david minja (shoto) na wa vodacom ephraim mafuru
mama wa mitindo asia idarous akila pozi na evelyne (pili kulia) ambae kaibuka balozi wa fabak fashions 2009
anko nanihii akitangaza mshindi wa Miss Redds-MichuziBlog photogenic 2009. Chini anko nanihii akiwa na Sylvia pamoja na Mwenyekiti wa kamati ya miss Ilala Jackson Kalikumtima (shoto) na meneja wa Redds Da Kabula (kulia) wakati wa kumzawadia Miss photogenic shilingi laki 5 wakimkabidhi smshindi hundi ya mfano wa pesa hiyo
tatu bora

Zena Rashid Mbasha mshindi wa shindano la vipaji akivishwa taji
Miss Ilala 2008 akiaga
juu ni tatu bora na chini tano bora
anko nanihii pamoja na kudhamini miss photogenic libeneke lilikuwa kama kawa wakati wa mchuano
mshiriki namba 4 margareth akiondolewa jukwaani baada ya kuzirai alipokosa nafasi kwenye 10 bora
washiriki wote wa redds miss ilala 2009
(Picha zote na Moiz Husein)




























Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 21 mpaka sasa

  1. Huyu bouncer ndio vipi tena hapo?! mbona kama anapata denda vile au ndio
    mouth to mouth resuscitation kujaribu kuoko!! mshindi kapendeza hopeful she is smart pia maana sura anayo.

    Ni mtazamo wangu.

    Mdau wa Juu

    ReplyDelete
  2. Hao warembo ubinadamu upo wapi? mwenzao ameanguka na kuzirai badala ya kumsaidia na kumpa huduma ya kwanza ndio wanazidi kuweka mapozi na kupunga mikono.Kweli aliesema wanawake hawapendani hajakosea.

    ReplyDelete
  3. Hongera Sylivia, hata Bongo Pix alishakupitisha zamani mbon ailikuwa yangojea utangazwe tu. Brazo!!! na karibu ktk ulimwengu wa ulimbwende ambao marafiki zako wa karibu ni wapiga snap ka BP or Mzee wa Libeneke hapo.

    ReplyDelete
  4. Viongozi wetu kwa mambo kama hayo uwaambii kitu ingekuwa kwenye kutatua shida za watu tungekua mbaaaliiiii!

    ReplyDelete
  5. mgeni rasmi mheshimiwa .... shoto bosi wa..... kulia bosi wa....namba mbaya hizo haponi mtu hapo.

    ReplyDelete
  6. - namba 2 evelyne, sijui, atafika mbali..watch this space!!..hao wengine 'utamu wa sukari' waonjwa na ncha ya ulimi!..

    ReplyDelete
  7. Nimefurahi kura yangu imejibu maana anabamba mno 8000 jupu juuuuuuuu

    ReplyDelete
  8. Miss kakaa kimama mama huyu. Mwangalie mikono, tumbo na hips. Kwa vigezo vya Kiafrika anaweza hata kuwa miss Tz. Lkn kwenye vigezo vya miss world haingii hata kwenye top 150. Ana umbo la kimama mama, anafaaa sana kuwa mke wa mtu na kuzaa watoto na si kuwa miss.

    ReplyDelete
  9. Michuzi mkeo kazi anayo.

    ReplyDelete
  10. ANKO NANIHII ULIKUMBUKA KUMTWANGA SWALI HUYO BINTI NI KWANINI ALIKUITA MICHUZI MAHARAGE??? KAMA HUKUULIZA BASI ULICHEMSHA, NINGEKUWA MI NDO WEWE PALE ULIPOPEWA NAFASI YA KUSEMA MAWILI MATATU PALEPALE NDO NINGEIBUKA KIVYANGUVYANGU NINGETOKA KAMA HIVI, "Ndugu mabibi na mabwana nashukuru kwa nafasi hii mliyonipa ya kutoa mawili matatu. Kwanza kabisa naomba nitoe dukuduku langu manake mi huwa sipendi unafki, nataka kuwauliza swali moja tu hawa washiriki wa miss Ilala walioko mbele yenu usiku huu, je nyie mamiss mlioko mbele yetu mimi sitaki matatizo na nyie, naomba tu muwaeleze watanzania walioko mbele yenu hapa, Ni KWANINI siku ile ya utambulisho mlinikejeli kwa kuniita MICHUZI MAHARAGE???, swali langu ni hilo tu, naomba muileze hii kadamnasi LA SIVYO NITA-WITHDRAW SPONSORSHIP yangu nataka jibu sasa hivi ahsanteni".
    hivi ndivyo ulitakiwa kuongea bwana Issa Muhidin Michuzi.
    Langu ni hilo tu
    Francis,IL.

    ReplyDelete
  11. Kwani huyu Miss Redds na Miss Phtogenic alikuwa namba ngapi kule nyumna? 300/600 au???? Michu mdogo wangu naomba kuwasilisha swali

    ReplyDelete
  12. Wewe Francis was IL, na wewe umechemsha. kwanza kabisa.......Je pili? na tatu NA mwisho???? Mbona umechemsha hata wewe. Mdogo wangu Michu...nawasilisha. Mtoa hoja (MH)

    ReplyDelete
  13. Mtanzania mmoja alianza kazi ya kuuza mboga na kila mmoja akaelekea huko. Akaja mwingine akaanza kuuza maziwa, wote haooooooo - maziwa......nk nk....na sasa ni miss ilala, miss sinza, miss maharage, ms..blog nanihiii...na miss michuzi maharage nk nk...na kesho itakuwaje? EPA??? na pia kuuza kiwanja cha mita 600 kwa dola za kimarekani 30,000!!!!!! Uchizi mtupu huku tanzania!! Huu nasema na uchizi. Hakuna mwelekeo wala direction (kama kuna tofauti ya maneno haya mawili nisaidieni).
    Mchuzi mdogo wangu nawasilisha hoja MH

    ReplyDelete
  14. Mdogo wangu Mchuzi,
    Zefulanas iko wapi? Tangu ulipoanza kuwahoji hao watoto hadi leo hii sijaiona zefulanas, nikutumie dozen moja ya zefulanas?
    Mchuzi mdogo wangu natoa tu hoja. MH (Mtoa hoja)

    ReplyDelete
  15. HAO MAMISS WALIOKUWA NEAR NA HUYO MWENZAO ALIYEANGUKA NI WAPUUZI NA HAWANA UTU. KITENDO CHA KUMUONA MWENZIO KAANGUKA INGETAKIWA WAWE NA UTU ATLEAT KABLA YA BAUNSA KUJA SIO WANAKAZANA KUPUNGA MIKONO.
    I HOPE HAKUNA ALIYESHINDA KATI YA HAO WADADA WAWILI WANAOPUNGA MKONO KARIBU NA DADA ALIYEANGUKA.
    PART YA MWANAMKE KUWA MZURI NI KUWA NA UTU NA ROHO NZURI AKA....

    ReplyDelete
  16. Jamani mlio kuwepo, kuna miss wa kwanza kuulizwa swali, siku namsikiliza ila kama vile alisita katikati nakuomba swali lirudiwe je ndio huyu aliye shinda Miss Ilala?
    Halafu kuna Miss mmoja ana dai anasoma USA ni yupi maana alisema alifaulu vizuri ningependa kujua aliambulia nini kwenye mIss Ilala

    ReplyDelete
  17. ni matoto wa wafisadi vigogo wachichini basi washapatiwa pesa majaji nani mwingine nchi zilizoendelea gym kwanza balance diet na attitude lakini watanganyika pesa kwanza wapinawapi hata kama ndiyo mimi nitaishia kburini pesa yesu alishailaani kabisa maana hata huyo aliyechaguliwa atazeeka tu sikumoja remember that people ageespecially we women we do loose alot of nutrients too

    ReplyDelete
  18. Na mie nilijua tu ama atashinda haya karibu katika umaarufu kunuka miss 8000 cjui utaanza na skendo gani tunasubiri mambo yako

    ReplyDelete
  19. Duh watoto wamependeza....tofauti na kabisa na zile picha niliziona huku

    anyway, huko camp wakiwa wanaandaliwa huwa wanaandaliwa nini? Just a catwalk? Duh...Wangetakiwa wawe wanaandaliwa kisaikologia pia. Wenzenu wanawaandaa na akili zao waelewe kuwa kuna kuwin na kuloose hapo.

    Haya mambo ya kuzirai huyaoni kwenye 1st world. Laki tano tu inamfanya mtu azirai je ingekua millioni. Si angekufa mtu hapo.


    Lakini who knows alishaongea na kibibo au alishahonga hela sehemu akajua yeye amenunua seat. mara jina halipo anashangaa imekuaje.....pole yake

    ReplyDelete
  20. Napenda kujua lini na sisi huku tutapata mwakilishi wa urembo? Maana nasikia miss Magomeni, Sinza na blaa blaa. Please naomba wanaoandaa mashindani wasisahau Miss Mchamba Wima.
    Mwanakampeni.

    ReplyDelete
  21. Do we really value human life? A contestant faints and the others are just waving. Where is first aid? The contestant needed medical attention first before being carried away. The first aid team should have rushed to the rescue. I am deeply saddened.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...