anko nanihii akiwa uhuru park ya jijini nairobi sehemu maalumu ya kupigia pafu.
huko kwa watani wa jadi si mchezo. huruhusiwi kupiga fegi sehemu yoyote
anko nanihii akikumbukia vekesheni yake ya kwa watani wa jadi. hapa ni kajisehemu tu ka gaden ya uhuru park ambako walipa kodi wa jiji la nairobi hufaidi kwa kupimzika na vivutio kadhaa. sijui wazee wa jiji la dar ambao wanaonekana kuwa na mtindio wa ubunifu wanasemaje?

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 12 mpaka sasa

  1. Bongo wanauza mapa maeneo ya shule au beach mpaka baharini! na unafanya mchezo..na fisadi's!!

    ReplyDelete
  2. Mambo mengine Afrika tunaigiza mpaka tunapitiliza.

    Jiji london kuna bonge la park - Hyde Park, kitu kama hicho cha kuzuia wapiga fegi hakuna, maana ni sehemu ya wazi, labda kwa ustaarabu una hakikisha hakuna watu waliokuzunguka kwa karibu.

    Basi hapo Nairobi wawapige stop wavuta sigara katika barabara zenye wingi wa watu pia.

    Tukiiga mambo, basi tuige mambo mpaka miundo mbinu ya kisasa, umeme saa 24 kwa siku, kilimo kwanza n.k

    Mdau
    MpigaFegi1

    ReplyDelete
  3. we michu endelea tu sijui huwa vidole vyako vina kwi kwi?! huwa unabofoaga sana NAIROBU ni kuzuri sana kuliko nairobi
    miss michuzi

    ReplyDelete
  4. Michuzi Haiwezekani Tena sababy Sehemu zilizotakiwa kuwa Park na Park za watoto Kucheza Serikali wameziuza Kujengwe Nyumba Miti Imekatwa katwa ovyo Basi joto tu linazidi. Inshallah tutafika ila Kunavitu muhimu zaidi ya hivyo Bw Michuzi vya kufanywa kuliko hayo hapa Tanzania. Tuanze kusomesha Watoto wa Barabarani na kuwatafutia makao mazuri. kuliko kuangaika na Miss Tanzania.

    ReplyDelete
  5. We anon wa pili, si kila kitu ugeze ulaya, vitu vingine unatakiwa uwe creative mwenyewe,acha ulimbukeni. " Kuku mkubwa wa kizungu, mbona mende au inzi mkubwa hamuwaiti wa kizungu"

    ReplyDelete
  6. MpigaFegi1,

    Kwanza kabisa ujue kuwa the number one killer katika hii dunia ni hiyo sigara unayoitetea.Siyo tu unaongea ongea ili mradi na wewe u-post hapa kwa Michu.Sigara hiyo ujue kuwa inaua hata wale ambao sio wavutaji.Unadhani uvutaji wa sigara ndio ubingwa?Watu wanakufa na wanawafanya wengine pia wafe kwa ajili ya starehe zao za kifo.Ni sahihi kabisa kuweka smoking zone na sio kupuliza moshi tu kama train ya makaa ya mawe.Bongo hakuna usimamizi na ndio maana unaona kama wanaiga-TEMBEA UONE!

    Mdau.

    ReplyDelete
  7. DAR iige mfano wa Nairobi, na miji mingine misafi ya nchi zilizotuzunguka.
    Tuache kujilinganisha na Tokyo bila sababu za msingi. Tujue uhalisi ili tuweze kutatua tatizo.

    ReplyDelete
  8. huyo mwenye kufananisha afrika na ulaya na kukashifu africa ni mwafrica kweli. kuna watu wengi ambao sio waafrica ambao wanajua kiswahili na hawataki kusikia jambo lolote la maana juu ya africa kwasababu ya wivu wao. china ilidharauliwa na watu wa west mpaka hivi majuzi lakini angalia sasa wana washinda nchi nyingi za ulaya kwa maendeleo. michuzi mji wa nairobi ni mzuri sana.

    ReplyDelete
  9. Dk Shein tumemuona anashuka na first Lady wake, Akaja Mzee Pinda nae na first Lady wake mara Mzee Sinde kwenye besidei First lady kwa mbele na keki yake...huyu kaka michu yeye kila vekesheni, mtoko hadi besidei peke yake mmmmh kuna usalama kweli hapa??!!
    Mzawa

    ReplyDelete
  10. Hala hala hao wanapiga roba hao kama kufuli la mjapani usitembee peke yako. Silaha za kukodi huko bwelele dola 600 tu unakuja kuifanyia kazi ogpa sana nairobi hiyo

    ReplyDelete
  11. Nakuona kaka Michu unakumbukia enzi zako pale kijiweni petu....jani hilo!

    ReplyDelete
  12. OOOOH! SIGARA ZINAUA, OOOOOH! SIGARA NI HATARI KWA AFYA YAKO MBONA MICHUZI HAFI?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...