'JUISI YA MUWA GHALI'
Bahati niliipata, Unguja hatembelea,
Hajionea sakata, sepatapo kablia,
Muwa tabu waipata, wanywaji kuwaridhia,
Juisi ya muwa ghali, si tunavyofikiria.
Hajionea sakata, sepatapo kablia,
Muwa tabu waipata, wanywaji kuwaridhia,
Juisi ya muwa ghali, si tunavyofikiria.
Muwa wao huushika, mezani ‘kautandaza,
Huanza kwa kuukosha, muwa upate pendeza,
Kisha maji hukaushwa, tayari kutumikizwa,
,Juisi ya muwa ghali, si kama tunavyodhani.
Huanza kwa kuukosha, muwa upate pendeza,
Kisha maji hukaushwa, tayari kutumikizwa,
,Juisi ya muwa ghali, si kama tunavyodhani.
Kisu hwisha andaliwa, kupara miwa kuanza,
Kwa makali kilotiwa, chapara na kuparuza,
Kwa hamu wasubiriwa, muwa upate maliza,
Beiye haifanani juisi ya muwa ghali.
Kwa makali kilotiwa, chapara na kuparuza,
Kwa hamu wasubiriwa, muwa upate maliza,
Beiye haifanani juisi ya muwa ghali.
Baada kuhakikisha, nywele zote metolewa,
Muwa huusimamisha, mashineni ukatiwa,
Kwa nyuma huupitisha, na mbele kuutolea,
Katu haifananipo, juisi ya muwa ghali.
Muwa huusimamisha, mashineni ukatiwa,
Kwa nyuma huupitisha, na mbele kuutolea,
Katu haifananipo, juisi ya muwa ghali.
Mara kadha’ hurudisa, ili juisi itoke,
Tena huubiringisha, kusudi ulainike,
Kwa nguvu pumzi kushusha, maji yapate yatoke,
Adhulumiwa muuza, juisiye bei ghali.
Tena huubiringisha, kusudi ulainike,
Kwa nguvu pumzi kushusha, maji yapate yatoke,
Adhulumiwa muuza, juisiye bei ghali.
Mashine nazo hubana, hasa zile za asili,
Cha moto muwa huona, hadi badilika hali,
Hapo muwa huungama, haliye I tadhilili,
Madhulumu muuzaji, aongezewe beiye.
Muwa sasa ‘chopolewe, kwa mbwembwe na kwa madaha,
Hali ya utokajiwe, wengi huona karaha,
Maana siyo haliye, lipongia kwa furaha,
Jamani tukubalini, juisi ya muwa ghali.
Siri moja negundua, forodhani ‘lipokwenda,
Mashine si zote sawa, ziko nene na nyembamba,
Kuna zinazooshewa, ukatamani ziramba,
Ujira aogezewe, si rahisi kukamua.
Kuna zinazopuuzwa, holela zikatumiwa.
Viambazani hubanzwa, kazi zikishafanyiwa,
Hazikumbukwi kutunzwa, hata kwa maji kutiwa,
Huyu yuastahiki, bei ya chini kupewa.
Binafsi napata hoja, na haja ya kuuliza,
Muwa, mashine pamoja, na anaesukumiza,
Ni kipi kivikwe koja, kwa kazi kuitimiza?
Malenga saidiani, jibu hapa kupatiza.
Beti ihida ’ashara, zakifu kusimulia,
Kuelezea tijara, ya wanao para miwa,
Ombi kwao mshahara, nivyema kuongezewa,
Tusifanye masihara, kazi yao kazi ngumu.
Wakatabahu,
H. Hamad
MSc. Development & International Relations
Aalborg University
Denmark
zanzibaricon@hotmail.com
H. Hamad
MSc. Development & International Relations
Aalborg University
Denmark
zanzibaricon@hotmail.com
mzee wa libeneke kule kwa michuzi jr na haki kuna stori ya fitina za itv na radio one, mbona wewe huitoi? watu wana hamu nayo sana itoke kwenye ukumbi mpana kama huu waijadili aaah!
ReplyDeleteBw. Hamad, hiyo dawa yake ndogo. Huku bara miwa bei ndogo tu. Unanunua muwa wako unatafuna na kutema fundo. Ndivyo wengi twafanya huku Bara, yakhe.
ReplyDeleteHH shairi lako zuri. ni kweli juisi ya muwa aghali na hususan wakati kama huu wa mwezi mtukufu. lakini uaghali wake hauna budi kuangaliwa katika mchakato wa kanuni za utashi na ugavi. kwa mfano, wakati kama huu wa mwezi mtukufu mashine nyingi hufungwa na hivyo utashi huwa mkubwa kuliko ugavi, na hivyo kusababisha bei ghali zaidi!!!! kwa kifupi, ndivyo kanuni za uchumi zinavyoelekeza!!!
ReplyDeleteAnon wa sep 07, 10.59PM Unayosema ni kweli kabisa kwa kipindi hiki cha ramadhani juisi ya miwa inakuwa ghali sana kutokana na mashine nyingi kufungwa .na nilipata kuongea na wapara miwa wa visiwani (Zanzibar)wanasema wao wanapendelea sana juisi ya miwa kutoka Bara zinakuwa nzito na sukari nyingi kuliko za zanzibar nyingi zinatengenezwa na mabua . mie ushauri wangu kwa wale wapara miwa wangetumia zile mashine za kisasa zenye matundu madogo pale wangejua hasa ladha ya sukari (utamu ) iliyoko kwenye miwa na biashara yao ingetoka kwa sana na faida mara dufu .
ReplyDeletemdau maalim Kifundo Uk.
"Juisi ya muwa ghali-Jawabu"
ReplyDeleteBismillah naanza
Ubeti huu wa kwanza
Nami nipate jifunza
Utamu wa huo muwa
Ila nataka kujuwa
Vyereje wasifu muwa
Ukaicha mashine
Inayojuwa kamuwa
Nisawa kusifu jino
Ukauacha ufizi
Au kusifu mlezi
Ukasahau mzazi
Bila mashine kubana
Muwa hauna maana
Utazimaliza zana
Juisi kuikamuwa
Sifa zende kwa mashine
Isiyojuwa chaguwa
Uwe Mnene, mwemba
Yenyewe inakamuwa
Uwe kutoka mahonda
Mtibwa au kilosa
Juisi hutokikosa
Mashine ikiamuwa
Asili ya shengejuu
Au kutoka majuu
Pumzi takwenda juu
Muwa unapoutia
Tena huminya vifundo
Vilivyo vishinda nyundo
Kwa madaha na maringo
Juisi huikamuwa
Ajabu ya rahmani
Tena isiokifani
Muwa huwa watamani
Mashineni kuingia
Mengine ya toka bara
Lindi pia mtwara
Hata ile isoparwa
Mashineni yaingia
Mashine na uchafuwe
Si muwa na utamuwe
Muhimu ni ikamuwe
Juisi tujipatie
Tamati nna maliza
Kama sijakutatiza
Lengo langu kuuliza
Mashine waipuuza?
Mahadhy!
Kaka Hamadi kama kweli unaongelea muwa basi hamna neno, ila kama huu muwa ni tafsida tu itakuwa balaa!
ReplyDeletemashine ndio jawabu
ReplyDeletemalenga ameshajibu
asili ya muwa ugumu
mashine kuziharibu
........
Nawakilisha
Mdau
Trondheim - Norway
Kaka Hamadi, wastahil pongezi. Kwa mtazamo wangu wa haraka ni TAFSIDA nzito uloitumia kutoa ujumbe wako.Ama kwa hakika ujumbe umefika kwa wenye kuelewa maana.
ReplyDeleteAhh Bableee nawe wamo????
ReplyDeleteKeep it up
Kakio
wajameni hiyo mi-verse mimi chali.
ReplyDeletemuwa+machine=juice???????
baghosha