Chef Issa akiwa na tuzo ya kichwa cha ngombe na majani baada ya kuonyesha uwezo ktk utengenezaji wa chocolate.
chocolate special order ya mechi kati ya arsenal na ac roma kwa wageni waalikwa wakati wa champions league aliyotengeneza Chef Issa

Chef Issa akichanganya chocolate ganache na chef mkongwe na mtaalamu wa chocolate kutoka Suter Bakery ya Luzern, Switzerland

Chef Issa akipata lunch na machef wenzie kabla ya mashindano

Chef Issa anashukuru kwani tayari ameshafungua blog ya 'Culinary Chamber' na kwa sasa anaandaa articles pamoja na taswira. Anasema amesoma maoni ya wapenzi wa Globu ya Jamii na anayakubali kuwa ni changamoto.
Chef Issa anasisitiza HACCP ni moja ya taaluma muhimu kuliko maelezo ila aliyopata yeye ya main course ni art in european culinary management ( bingwa wa chakula cha kimagharibi) ambapo ukitembele ktk site no 1 duniani kwa kazi za hotel duniani inaitwa www.catererglobal.com na pia utakuta kazi zote za ma chef zinazotangazwa. Hapo ni lazima uwe HACCP certified bila hivyo hata kama una uzoefu wa miaka 20 hakuna atakae kukabidhi jiko umsababshie jiko lake kufungwa.
Anasema Tz bado hajasikia hata siku moja hotel au mgahawa umeshitakiwa au kufungwa kwa sababau za afya, na kwamba majiko mengi ni machafu kweli kweli na usalama wa vyakula ni mdogo na haufanyiki, anasema ni hatari.
Katika kuendeleza libeneke, Chef Issa amebahatika kupata nafasi ya kutengeneza chocolate ambazo zilitumika katika mechi ya Arsenal na Ac Roma mwaka huu mwezi wa 3 kwenye champions league wakati wa mafunzo yake ya utengenezaji chocolate na cheese ktk jiji la Luzern, switzerland.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 47 mpaka sasa

  1. Tumezoea kuwabeba ma miss na wacheza mpira je wizara ya maliasiri na utalii mmemuona kijana huyo kapeperusha bendera ya Taifa kwa juhudi zake binasfi nyie kama wawakilishi wa sekta ya utalii mnajivunia nini ikiwa mtaalamu huyo yupo na ajira nyingi bado zipo mikononi mwa wageni mantuvunja moyo wa kurudi nyumbani tukimaliza elimu tunabaki kujenga mataifa ya watu kwakua hatukubaliki nyumbani mdau Ireland

    ReplyDelete
  2. Duh kaka mi ni mshabiki wa the gunners duh kumbe zile chocolate ulitengeneza ndugu yangu aisee tulizila kwa macho tu ni kweli zilikua special kwa VIP tu duh aiseeee chef Issa uko juu hazijabaki hata 1 jamani tukutumie viza utupitishie London jamani tuweke kumbukumbu Tanzania oyeeee sasa watu wanasoma mpaka raha Hongera kwako na familia yako yote Mdau London

    ReplyDelete
  3. KTK HOTEL STAFF WA KWANZA ANAETHAMINIKA KAMA JICHO NI CHEF AKIKOHOA TU KILA MTU LAZIMA NETWORK IKATIKE NA MACHEF WENGI NI WAKALI SANA NA EXECUTIVE ANAMSHAHARA SAWA NA GENERAL MANAGER MDOGO WANGU ISSA UNANAFASI NZURI FANYA MAAMUZI YA BUSARA USIJUTIE TAALUMA YAKO NI ALMASI KUA BINGWA WA EUROPEAN DISHES SIO MCHEZO WATANZANIA TUNAKUPONGEZA Hotelier Istanbul

    ReplyDelete
  4. Uingereza inafahamika kwa mtaala bora wa elimu na swiss inafahamika kwa standard pia ndio inaaminika kua ubora wa mambo ya hotel unaanzia swiss kaka naimani umepikwa na umeiva cheti chako kitengenezee safe watu wasijetia husda watu wengi wanafeli sana sana fani hii na gharama ya masomo ni kubwa kuliko kusomea urubani au udoctor ulijipinda usingefaulu ingekua hasara kubwa ktk familia yako Hongera sana fanya makubwa zaidi tunakuunga mkono sana tu mdau Switzerland

    ReplyDelete
  5. Alichokisema chef issa ni kweli kabisa kuna baadhi ya hotel kibao tu hapa nyumbani ni chafu sana na ni hotel kubwa kweli kiasi cha kuhatarisha usalama wa chakula watu wanaugua sana tu na sumu zitokanazo na chakula lakini sijui kwakua matumbo yamekua sugu lakini ipo siku itakua ni balaa kweli tusiwapigie magoti wageni tu sasa tunawazawa waliofuzu wapewe nafasi walijenge taifa kwa uchungu sio wazungu au wakenya waliokuja kuchuma na kutunyanyasa chef Mwanza

    ReplyDelete
  6. Kaka Issa unarudi home lini tuje airport tukupokee kwa shangwe kweli utakua chef mdogo kuliko wote tanzania kwa mafanikio uliyoyapata ukipita hoteli zote hapa bongo machef ni wazee na wanafanya kazi kwa uzoefu wala hawana hata cheti wengi wana vyeti vya kufoji tu ukiangalia hata vyuo vyetu bado wanababaisha tu hakuna elimu bora bado ktk fanii hii angalu forodhani wanajitaidi Mdau Zanzibar

    ReplyDelete
  7. Jk mtanzania huyo anautaalamu wa chakula cha magharibi atakufaa sana kwa state banqueting wanapokuja wageni wa nchi mbalimbali, wizara ya elimu mtumieni mtaalamu huyo kuchangia mitaala ya mambo ya mapishi veta, wizara ya maliasiri mtaalamu huyo awasaidie kukagua viwango vya mahotel na majiko feki mboreshe sekta ya utalii, kufanya kazi third world inataka moyo nakushauri usirudi home tafuta kazi popote ulipo ule bata kiulaini Mdau German

    ReplyDelete
  8. Mdogo wangu Issa umepiga bao la kisigino mi binafsi nipo ulaya miaka kibao ktk fanii hiyo ila nakuvulia kofia wasiss ndio wanaongoza kwa chocolate duniani ingawa kakao inatoka ghana hahahahaaaaaaaaa kaza buti utafika mbali zaidi juu juu daima kwetu bongo majungu mengi ziba masikio chapa kazi ndio siri ya mafanikio upo wapi kwasasa? njoo mwaka mpya tujimwage chef Malik Williams Venice Italy

    ReplyDelete
  9. Ni kweli chef Issa.

    Every operation serving or selling food needs to have a food safety system in place that is designed specifically to guarantee the food being served is safe to eat. This specific food safety system is called HACCP for Hazard Analysis and Critical Control Point. HACCP is a system comprised of 7 principles that are to be applied to a written food safety program focusing on the food in your operation. This course aims to teach you the importance and use of all 7 principles in order to make you a safer, more effective food service employee.

    Course is a Four Hour Seat Time and Meets the Regulatory Requirement of Compliance with the 2005 FDA Code and the USDA Requirements for School District HACCP Plan Implementation.

    Mdau.
    USA

    ReplyDelete
  10. weweeee, utakuja rogwa bule huku bongo.eti una cheti cha Nyota tano? unataka kuchuka kazi ya nani? eti umesomea upishi, watu wamekuwa wana pika tangu enzi ya mkoloni bila cheti na wewe unawaambia eti wachafu weweweeeeeee, utarogwa na hicho cheti chako kitaungua moto na wewe utakuwa huoni.shauri yako.

    ReplyDelete
  11. Chef Issa, hiyo special order ya mechi, Mashallah.

    ReplyDelete
  12. Horns /Horny Head, jumulisha Chokolada/ chocolate is equal to Kujiraaambaaaa.

    Au sio, Chef? Hapo vipi?

    ReplyDelete
  13. Hongera bwana issa,manake watu wamekuwa wanaheshimu fani za udakitari na uchumi na wanalipa mahela mengi kwenye mavyuo ya nje kusomea hivyo vitu lakini hata hawaenjoy kufanya mambo yao.wewe inaonekana unapenda unachokifanya ambacho ni cha kupikapika.Waonyeshe watu mambo ya kujipikilisha ndo yenyewe.
    Mhangaza wa kanazi
    http://duniayetukubwa.blogspot.com/

    ReplyDelete
  14. 2010 iko mlangoni hadi leo kuna imani ya uchawi.Wake up ndugu zangu train imekwisha tuacha wenzetu wamefika mbali sana.

    ReplyDelete
  15. hongera saana kaka issa yaelekea ulikuwa makini na mwelewa ndo mana sasa hivi na wewe ni chef bab kubwa kwani wao waweze wana nini hata wewe ushindwe kuna nini?? uko juu umeweza kama wao hongera sana chef issa michu.. oops chef issa
    mdau canada

    ReplyDelete
  16. Ndugu Issa mimi kama mdau mmoja wa sekta hiyo ningependa kukupa hongera kwa level uliyofikia. kaza buti mkuu rudi nyumbani uwaonyeshe jeuri wazungu walio jaa kwenye mahoteli yetu bongo. pili wewe ndio ungefaa hasa kuitwa Issa Michuzi sio huyu Michuzi tuliyemzoea . huyu angeitwa Muhidin Masnap au Mablog.
    mdau Leicester Uk.

    ReplyDelete
  17. Food production is Art and scicnce Scince applies on how you mix you ingedients and transform raw material to the right done of cooking with reasonable test to eat, Art is how you decorate and arange the dish on plate to impres the consumer ohhh my god to be Executive chef lazima uwe na kichwa kama cha Issa kaka umefaulu halali ulaya elimu sio ya kuhonga hasa swiss. Veta wanafungua chuo Arusha wewe unafaa kua mwalimu pale pls nenda kawape utaalamu watanzania wenzako mungu atakulipa mdau Canada

    ReplyDelete
  18. Kaka michuzi niliona ktk blog yako hapa VETA wanafungua chuo cha mambo ya hotel na utalii sasa ni muda muafaka wamepata mtaalamu huyo mzawa wamuheshimu na wamtumie asaidie kutoa elimu kwa moyo mmoja kwa ndugu zake watanzania inapendeza sana jamani tujivunie kijana huyo na tumuenzi hiyo tusimuachie hiyo ni lulu ya taifa jamani JK pls pls tupia macho hapo Mdau Antwep Belgium

    ReplyDelete
  19. Issa umewafariji sana wazazi wako, watanzania na familia yako kwa ujumla ni ujasiri najua umepata shida sana kufikia hapo kwa ubaguzi uliopo ulaya utakua ulipambana sana kwani hata wao hawafurahi kuona weusi tunafanikiwa umepita pagumu mapaka kufanikiwa mungu akujalie sasa ulie kivulini kwa raha zako. muximum respect Mdau Russia

    ReplyDelete
  20. Wapishi wengi sana tunao hapa home lakini wanapikia uzoefu tu sio wataalamu kama alivyosomea chef Issa ni muhimu sana ili uwe tofauti ktk ushindani wa biashara ya hotel chef akifahamu vizuri chakula histori na ubora wake hasa mgeni anapotaka maelezo zaidi mashefu wetu wengi ni kina kanumba uwiiiiiiiiii hahahahaha kazi ipo mmatumbi issa njoo ujenge nchi ziba masikio mengi yatasemwa sisi watanzania milioni 38 tunakukubali

    Mdau korea

    ReplyDelete
  21. Tunamadereva kibao Hapo Tz lakini sio wote wamekwenda diving school ila waliokwenda driving school wanapata wasahaa wakujua zaidi usalama na alama za barabarabi so tanzania tuna cooks kibao na chakula chao ni chahali ya juu wangepata washa wa kusoma ingekua safi zaidi kua qualified and certified executive chef hata picha yako tu inaonyesha kweli unaumri mdogo peney nia pana njia umejikwamua ktk taaluma sasa Tamba unatambulika kokote duniani Mungu akupe uzima na maisha marefu ufanye makubwa zaidi

    Mmatumbi Norway

    ReplyDelete
  22. kua chef sio kupika tu unatakiwa shule iwe yakutosha kichwani hesabu kwasana! marketing knowledge lazima! HACCP lazima ili uweze pamaba na soko la ushindani wa chakula Executive chef hapiki tena yeye anakua anatunga menu na kufundisha staff wake kufatilia ubora wa production, usafi na kutoa idea za marketing kwa staff wanouza product yake kwa wageni kwani mgeni anafarijika zaidi ikiwa atapata maelezo zaidi ya anachotaka kukilipia so shule muhimu mdogo wangu Issa wazazi wako wanastaili sifa kwa support ya kukusomesha fani adimu na adhimi wathamini sana upate maisha marefu yenye mafanikio mdau Dubai

    ReplyDelete
  23. Kaka Michu tunampa Hongera huyu kijana.
    Lakini trend ya ushabiki inaelekea kuwa kama ya ile ya John Mashaka ambaye aliishia mitini hata katika mwaliko wa kongamano la wanataaluma (Dar)na hawezi kuchaguliwa hata kuwa diwani tu popote Tz maana alianza kuvimbishwa kichwa eti yeye ni nabii na ndiye rais mtarajiwa na kwamba kiingereza chake ni babu kubwa na bla bla kibao..

    Dogo umepata elimu nzuri lakini huwezi kamwe kujifikiria kuwa wewe ndio namba moja au bora zaidi kuliko Watz wote maana kuna watu kibao wako ndani na nje na hawajitangazi kihivyo lakini mambo yao huwezi amini.
    Yaani siku moja utashangaa kukutana na Mtz ambaye yuko Chuo kimoja kimya kimya na siye mwanafunzi bali ni Mkufunzi mwandamizi wa mipangilio ya majiko, uandaaji wa meza, menu na vyakula mara dufu kuliko ulichokipata.

    Work smart with a low profile!

    Hii haiwezi kuminywa maana ni mawazo yangu!

    ReplyDelete
  24. Hongera kaka Issa, wadau wengi wanakushauri urudi nyumbani ukajenge nchi, lakini ukiangalia wanavyosaini hapo chini ni Mdau, Uk, mdau Russia, mdau US na mdau sijui wapi na wapi. Kwanini ni wewe tu ndie urudi ukajenge nchi wao kwanini wasirudi wa kwanza, kinachowaweka huko ni nini? Kama ni madaktari tuna shida nao sana, kama ni walimu wa vyuo vikuu ndio usiseme, na wataalamu wa aina mbali mbali wanahitajika lakini mbona hawarudi wao.

    Sikiliza kaka yangu, ukipata kazi ya maana huko uliko, fanya, jiendeleze zaidi kimasomo, kwani elimu haina mwisho, taifa linaweza kujengwa popote ulipo sio lazima uwepo Tanzania. Pesa utakazopata huko uliko utaendeleza familia yako Tanzania, kwa njia ya Remittances, kuna nchi hapa duniani zinawasaidia vijana wao kwenda kufanya kazi nje ya nchi ili kuingiza pato loa taifa kwa njia ya remittances. Usisikie mwayago baki huko huko ujenge taifa letu kwa njia ya michuzi utakayoileta nyumbani kama remittances, kama ni suala la kufundisha utakuwa unawafundisha kwa njia ya mtandao inatosha, kumenyeka kote huko eti ukaishie kufundisha VETA ntakushangaa!

    ReplyDelete
  25. We mdau uliempa hongera issa na kumfananisha kama john mashaka umekosea sana kwani yeye sio mwanasiasa yeye ni hotelia mdogo sana aliepata mafanikio makubwa sawa kama kuna huyo muandamizi wa maswala ya chakula kokote duniani na ni mtanzania ajitokeze basi agawe ujuzi wake kwa watanzania akijificha na taaluma yake inafaida gani ketu kijana kajitokeza ili asaidiane na watanzania wenzake kwa kubadilishana ujuzi then tunaanza kumvunja moyo huu ni ushamba wa hali ya juu nawala hajasema kama yeye ni bora kuliko wa tanzania wote ila nimmoja ya chef mdogo kuliko wote Tanzania amabae kafuzu kielimu na hii ni kweli tuache majungu tujenge nchi Mdau CRDB DAR

    ReplyDelete
  26. Ama kweli nchi hii imejaa chuki watu mpaka mnaanzan kumuapizia kijana wa watu kua atakutana na mtaalam siku moja ashangae duh kazi ipo! watu wengi wachoyo wa elimu dogo kasoma kwa mamilioni ya pesa anajiolea kufundisha kwa njia ya mtandao bure mnaanza majungu kua work smart with low profile inamaana ajifiche kama nyie mlivyokalia ujuzi wenu? acheni rohombaya haubiri siasa ila itasaidia sana hata kwa wake zenu kujifunza kuwabadilishi misosi yenye akili majumbani kwenu hahahahah uwiiiiiiiiiii kudadadeki Issa usirudi home haya mazee yatakuparua bure Mdau YANGA

    ReplyDelete
  27. mtu anapofanya vizuri lazima apongezwe swala la work smart with low profile huo ni ujima wa enzi nzenu we sijui ulisoma rasia? mbona untaka kuleta ukomunism kwenye nondo za watu kimbia huko acha vijana tufanye mapinduzi weweeeeeeeeee nahasira kweli na haya majitu yenye majungu duh tutafika kweli? kaka issa usirudi kabisa kula kona tena speed 120 mdau Mwenge

    ReplyDelete
  28. unaona unaona unaona jamani duh majungu hayo bila chef Issa kututaarifu maendeleo yake tungejuaje kama tunawataalamu wa sekta hiyo tena ktk umri mdogo hivyo? hapa sio swala la kujisifia ni ukombozi na mapinduzi ktk sekta hii hotel zote zimeshikwa na wazungu na wakenya tunahitaji mabingwa kama yeye waje washike nafasi hizo hii ni issue tofauti na john mashaka hata kama sawa na john mashaka we inakuhusu nini mwacheni kijana wa watu ale good time kijapan hulalalalala Mdau DHL

    ReplyDelete
  29. Chef issa wewe ni mzalendo halisi umeamua kutuelezea mafanikio yako pamoja na malengo yako ya kushea elimu yako na watanzania wenzako ni busara ya hali ya juu na moyo wa kipekee ktk umri wako maana wengi ni wachoyo wa kugawa ujuzi ziba masikio work smart with high profile unaweza bwana ila baki kokote kule nje home bado hali si shwari utapoteza muda wako kama unavyoona majungu by nature ohhh my God kazi ipo Mdau Dar

    ReplyDelete
  30. Hcef issa hureeeeeeeeeeeeeeeeeee hureeeeeeeeeeeeeeee kudadeki mapaka mate yananidondoka kijana ulivyofanya mambo ya ajabu kama watu wangekua wanajifich vipaji vyao basi GUINESS WORLD RECORD isingekuwepo issa ni mtu wa watu nakukumbuka ulipokua Executive chef five star hotel kule Arusha iliyofunguliwa na Dr shein makamo wa Raisi ulikua unajulikna kama mzee wa sumu haaahahah yaani full sumu kwa misosi yakufa mtu uliokua unaporomosha hasa wakati wa Sulivan wakuu wote walikua wankula hotelini kwako kijana always uko juu juu zaidi Mdau Arusha

    ReplyDelete
  31. Tunasubiri blog ya Culinary chember kwa hamu sana naimani itakua yakufa mtu Good job kijana welldone pongezo sana kaka michizi aka misupu kwa kutuletea huyu kijana online we ni mwanmapinduzi ktk blog super sana kaka michuzi huna husda na mtu basi tu ila unatufaa sana yaani we acha tu hujafulia kabisa uko juu theteheteheee uwe juu zaidi milele amini mdau mtwara

    ReplyDelete
  32. Karibu home chef mzalendo na blog yako tutaipa supot sana tu pamoja ila ujifunze kua mzalendo kama kaka michuzi wa jina lako maoni ya watu usibanie ili kukuza na kuendeleza blog yako ukubali yote hakuna wazuri tu hata wale wabaya changamoto yao inasaidia wewe kua bora zaidi big up big up mzee unatisha hasa ilo lichocolate la arsenal duh full shangwe mzee

    ReplyDelete
  33. SASA UMESOMA CHUO GANI NA LEVEL GANI? KUNA WATU PIA WANATAKA KUOMBA NAO WASOME. NI KAZI NZURI LAKINI PIA BAHATI INATAKIWA, KUNA MACHEF KIBAO HAWAJASOMEA LAKINI WANA BAHATI NA WAKO MBALI SANA KWA MFANO HAPA U.K. KUNA JAMMY OLIVER, GORDON RAMSAY HAWAJAENDA SHULE YA KUPIKA LAKINI NI WATU WENYE PESA KAMA MVUA INAVYONYESHA SO BAHATI PIA INA-PLAY PART KATIKA MAISHA. MWISHO TUNATAKA KUJUWA UMESOMEA CHUO GANI NA WAPI HAITOSHI KUTUAMBIA CHETI CHAKO KINATAMBULIKA NA MMU NA CHUO GANI SIJUWI USWISS, KWANI ZIKO KOZI KIBAO ZA UCHEF NDOGONDGO AM,BAZO UTAMBULIWA NA VYUO VINGI DUNIANI PAMOJA NA HIVYO ULIVYOTAJA, HAPA UK KUNA NVQ PIA UKIFIKA NGAZI FULANI UTAMBULIKA NA VYUO VIKUU.

    ReplyDelete
  34. kama unamjua jamy oliver na goldon ramsey hawajasoma na wanahela chafu na kupatia maisha ni play party jamani machefu Tanzania msisome muendelee kubahatisha kama huyo mdau feki wa UK kama unaleta majungu mpaka ulaya kazi ipo we ndio mbeba mabox halisi

    ReplyDelete
  35. Goldon ramsey hajasomea culinary we jamaa umerogwa nini? vitabu vyote hivyo alivyoandika visingetumika mashule kufundishia kama angekua mbumbumbu kama wewe mwenye mawazo finyu sawa kila kitu bahati ila shule muhimu sana usilalie bahati ya mwenzio mlango wazi kama unavijua vyuo kibao vya culinary waambie hao watu wako waende huko na ndio maana mdau nadhani hakutaka kuweka wazi dogo anaakili kama mchwa UK nini bwana? majungu tu.

    ReplyDelete
  36. Inapendeza sana likikuuma ulitapike sasa unaona chef issa nae atakua na hela mbaya ndio unataka utume ndugu zako wakasomee huko alikosoma yeye? kama ulivyosema mafanikio ktk maisha yanaambatana na bahati kaa kimya acha kuvunja watu moyo sema na wewe nani na unamafanikio gani sio kukosoa wenzako kwa point za kijinga kabisa tena pumba mzamiajai wa Uk wewe! Big up Issa Mdau Kawe

    ReplyDelete
  37. Tunarudi pale pale nabii hakubaliki kwao mdogo wangu ziba masikio tena inaonyesha unabusara sana anzisha blog yako fundisha ndugu zako kama ulivyoahidi hayo ndio mafanikio ktk fani yako husda na chuki za watu tupilia mabli fanya kama huoni au hujasikia kila lakheli ktk mapambano. Shule shule tu ukiwa hujasoma hujasoma tu hongera usiishie hapo nenda juu zaidi

    ReplyDelete
  38. WE MTZ MZAMIAJI WA UK UNAKAA KUSIFIA GOLDON RAMSEY NA JAMMY OLIVER KWAKUA HAWAJASOMA BADALA YA KUSIFIA CHEF MWENZIO MZALENDO ALIEKULA NONDO YAKE WIVU USIO NA MSINGI, MTAAACHA LINI MAJUNGU YASIYO NA MSINGI? CHUKI BINAFSI? BANZA ALIMALIZA ELIMU YA MJINGA MAJUNGU NA ALLY CHOKI ALISIMBA CHUKI BINAFSI HAIFAI ENDELEA KUBEBA MABOXI MKUU URUDI HOME MGONGO UMEPINDA. ACHA WATU WAPETE NA NONDO ZAO BWANA.

    ReplyDelete
  39. Unataka kujua kasoma wapi? hahahahahaaaaa kasoma ulaya si unaona mweusi peke yake yuko na machefu kibao wadhungu! kama cheti kinatambulika na vyuo hivyo bora duniani basi kasoma chuo bab kubwa sio cha kubahatisha maana vyuo vya culinary bora duniani vinahesabika ikiwemo Coldon blue, ecole, MMU, IMI ,colnel, DST na SSTH utajaza kijana kasoma kimoja wapo kati hivyo navipo ulaya mzee.Huwezi tambulika na chuo bora ikiwa umesoma chuo feki jibu unalo tayari Mdau UK

    ReplyDelete
  40. kaka misupu tumeona mambo ya chonga chonga duh kazi ipo tunasubiri kwa hamu machef wa kikenya wanatusumbua sana na hii taaluma sasa chef issa kama atatoa shule ya bure duh mbona tutamshukuru sana inapendeza kweli mdau kwalukuvi

    ReplyDelete
  41. Hureeeeeeeeeee culinary chember karibu sana tutakupa ushirikiano kaka michuzi mungu akupe maisha marefu kwa kututambulisha huyu kijana always wewe mtu wa watu Mama....Mbezi beach

    ReplyDelete
  42. Kweli bwana nimeona bendera ya Tanzania inapepea duh dogo basi umeshatufunga mdomo wenye majungu wote tunalala sasa tunakuunga mkona na blog yako karibu sana kwa kishindo suport ipo sana tu usiwe na shaka

    ReplyDelete
  43. GOLDON RAMSEY NA JIMMY OLIVER wangekua hawajasoma wasindgeweza ku develope recipe na concept ambazo wametengeneza ktk vitabu na sasa zinatumika ktk vyuo vikuu maarufu duniani sawa utundu unamata sana ktk sanaa ya chakua lakini shule ni kila kitu we mshamba wa UK mi nichef mkongwe mtanzania nipo ITALY sijisifii kwakua kiwango changu cha elimu kipo chini napia natamani sana kusoma ingawa umri umekwenda dogo kajipanga vizuri akiwa na umri mdogo CONGRATULATION Chef Tomas

    ReplyDelete
  44. CHEF ISSA JARIBU FANYA MAPINDUZI YA FANII HII NYUMBANI IPATE MWANAGA ZAIDI WATOTO WETU WAHAMASIKE WACHIPUKIE KTK FANI HII ILI WAJE WACHUKUE NAFASI ZILIZOKALIWA NA WAZUNGU TUMECHOKA MAANA MAHOTEL NDIO YAMEVAMIWA SANA NA WAGENI SEKTA ZINGINE TUMEJIKOMBOA KIASI FULANI MUNGU AKULINDE MZEE SPENCER MIKOCHENI

    ReplyDelete
  45. aisee dogo umefanya maamuzi saahihi kweli hakuana blog ya mambo ya misosi sasa duh wake zetu watafaidi kujifunza badala ya kuwapeleka mashule maana mi nawivu sana na mke wangu duh aende veta morogoro mi naishi dar mhhhh baraa hii sasa net ipo home ajifunze kufatilia tu mafunzo mdau Kimara

    ReplyDelete
  46. Goldon ramsey na Jimy oliver hawa sasa wazee chef issa ndio anaanza kuota ndevu hahahahahaaaaaaaaaaa teheteteeeeeeeeeeee nani zaidi? inshaalah mola atakujalia utafika huko tu nyota njema huonekana asubuhi mdogo wangu .DADA ANTWEP BELGIUM

    ReplyDelete
  47. machef wa kibongo sasa ni time ya kushikamana mfanye mambo safi mkimuunga mkono dogo chuki hazina mpango huu ndi wakati wenu wakuwapa machef wanaochipukia ujuzi sio muanze kuponda maneno yasio na msingi na wala hayajengi mnatakiwa mtambulike ili mthaminike mpo wengi tu ila mnajificha na pia hampendi kutoa ujuzi kwa wenzenu haya changamoto ya kufunga mwaka toka kwa dogo hiyo Chef issa you Rock kinyamwezi

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...