Kwanza nawapa pole kwa msiba mzito wa mzee wetu reggie Mhando wengi tutamlilia na mwenyezi mungu amsamehe makosa yake.


Pili ningependa kushea na wadauzzzz kwenye kilaji iki cha Tanzania hapa ughaibuni kinazidi kulipenyeza jina la injii yetu Tanzania ikiwa Akon kaipeperusha bendera yetu kwenye ule mwimbo wake mpya wa soka kwa Madiba,kwa ubishi nasi tuna hii kitu kwa wapenzi wa chocolate a.k.a kashata.japo ramani ya inaonyesha ya Ethiopia katika kuwapiga tafu dugu zetu.japo waosha vinywa watalipinga hili.

MVH MDAU WA ICELAND

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 18 mpaka sasa

  1. SI KWELI HIYO NI COMPUTER PRODUCED OBJECT HAMNA KILAJI KAMA HICHO DUNIANI MBONA HAPA BONGO HAKIPO? USITUFANYE SISI MAFALA.

    ReplyDelete
  2. Mtoa maoni hapo juu unakumbuke ule usemi tembea ujionee mimi nilipokuwepo kule London nilishawahi kuiona hii kashata na nzuri sana sijui wewe uko wapi na sio lazima kilichopo bongo kiwepo ulaya au cha ulaya kiwepo kila kona japo jina la kwenu
    Mdau kisumu

    ReplyDelete
  3. Jina la chocolate ni Tanzania halafu ramani iliyoko kwenye ganda inaonyesha Ethiopia-It doesn't make sense kwenye ulimwengu wa kibiashara.
    Tunawapiga tafu gani wakati wao ni matajiri kuliko sisi.
    My take,Hiyo kashata imetokea Ethiopia na hilo jina halina uhusiano wowote na Tanzania

    ReplyDelete
  4. Hahaha hii imetulia afadhali nasi tujitutumue,Swali wizara husika wanajua hili au ndio wako ndani ya usingizi mzito.watafuniwe wao wale faida kama wataipata

    ReplyDelete
  5. labda kiwanda cha china kinatengeneza hicho kilaji lakini sio Tz................

    ReplyDelete
  6. Hongereni kwa hilo lakini tunaomba jina ni kampuni gani ina produce hiyo kitu hapo juu tupe jina ili to google tupate ukweli zaidi.

    ReplyDelete
  7. Tanzania ni nini katika hiyo brand? Ni kinapotengenezwa hicho kinywaji? Ethiopia inakujaje? Sidhani kama Tanzania au ethiopia zina inapatikana kakao. Kwa ujumla, hiyo lebo/kabrasha ni maswali mengi kuliko majibu, hivyo kunyewa ni mashaka!

    ReplyDelete
  8. We anonymouos wa kwanza acha uchizi. Kwa hiyo kama product haipo huko bongon ndio dunia nzima haipo? Kwa taarifa yako hiyo siyo computer generated image wala nini.

    Ni chocolate inayotengenezwa kwa kutumia "organic" products hivyo wanatumia sukari na kakao toka Tanzania kwenye bidhaa zao nyingi. Ila pia wanatumia bidhaa za nchi nyingine za Afrika na nje ya Afrika

    Usiwe unakurupuka. Tanzania ni zaidi ya uijuavyo

    Nenda www.ceder.net/chocolate

    ReplyDelete
  9. NA HIO FLAG ALITOBEBA AKON SIO YA BONGO MKUU ILE NI YA SAUZI IKIJIKUNJA INAONEKANA KAMA YA BONGO NA MIMACHO YAKO MIKUBWA HUJAJUA TU LOL NDELA YA KABURUR ILE

    ReplyDelete
  10. wewe Anonymous wa tarehe fri feb 19,03:07:00PM hiyo ipo kwa maelezo zaidi nenda ktk site hii http://www.decigifts.com/chocolates/chocolate-bars/tanzania-75/265.htm

    mdau toka mbele.

    ReplyDelete
  11. Nyie ndo mnatutakaga maneno. afu unajihami ati 'waosha vinywa' Tanzania na ramani ya ethiopia wapi na wapi. Kama unatakaga kutukanwa tafuta njia mbadala. Pusi we!!! Hivi jamani watu wengine huwashwa kubongewa mbovu??? Nimetoka Box na nimechoka ila next time watu kanyie hunisaidia kuondoa uchovu kwa kusukutua kinywa. Nasema koma na ukomage.

    Mpg Box

    ReplyDelete
  12. Mbavu zangu namkumbuka huy Mdau wa Iceland aliahidi kuleta kajielimu sijui ule mpango unaendeleaje?maana kama huyo mtoa maoni wa kwanzaanahitaji elimu,Pia mnajua mtu akikosa viza basi anaathirika kisaikoloji Ndio maana mdau wa Iceland akaandika japo waosha vinywa watalipinga hili
    Mdau kwa bibi

    ReplyDelete
  13. We mdau wa Tarehe Fri Feb 19, 07:02:00 PM acha ubishi hewa, nenda katizame video nzima kisha tizama picha zilizotoka ktk video hiyo, unataka ikunjuliwe zaidi kivipi? Bendera ya SA ipo na ya Tz ipo na nyinginezo, linki ya picha hii: Bendera ya Tanzania katika wimbo wa Akon (bofya hapa)

    ReplyDelete
  14. Wewe mdau nusu majununi nusu hamanazo kama huyo mwenzio hapo juu,Umedai kwenye ule mwimbo ile sio bendera ya Tanzania wacha kukurupuka ile bendera ya Tanzania na nendo kaangalie vizur Oh Africa
    au www.mtv.se kwenye mahojiano ya ule mwimbo Hyawani mkubwa
    Aahsante mdau wa iceland kutumumuzishia aka kalaji sasa kanapatika wapi kwa wingi?nasi tumung unye? michu tafadhali tuulizie Mdau wa Iceland

    ReplyDelete
  15. Kwa uzito wa boksi la leo sikutegemea kucheka Michuzi mungu akubariki mwanawani watu hata benera ya Tanzania hawaijui wanai kwenye ule mwimbo ile bendera ya South ikijikunja inaonekana ya Tanzania,bora wakoloni warudi au Nnari arudishwe kazini,
    Ni hivi Bendera ya South ina Rangi,nyekundu,nyeupe,kijani,njano,nyeusi na blue,Ya bongo Kwanza haina rangi nyekundu pili mpigie simu mwalimu wako wa akili umuulize bendera ya nchi ikoje
    Mpiga boksi Mitaa ya mbali

    ReplyDelete
  16. www.eastafrican.etFebruary 19, 2010

    Kweli ukishangaa ya musa utayaona ya waosha vinywa,Ethipia utajiri wao nini?Njooni hapa Adis ya Baba muone kibanka nazi,,japo pesa yao iko juu lakini choka mbaya wacheni hizo hiyo kampuni naijua iko Italy na inatengeneza iko kilaji kweli au mshazoe mkiona nembo za Kenya
    alafu wewe unajigamba mpiga boksi unasukutua kwa maneno machafu wenzio tunapiga boksi tunasukutua kwa ulabu

    ReplyDelete
  17. Je mnajua the best and most expensive organic cocoa in the world inatoka Kyela, Tanzania? We don't have the west African quantities kama za Ghana na Ivory Coast, lakini tunaongoza kwenye quality. Je mnajua wakati sarafu mpya ya ulaya ya Euro ilipozinduliwa zilitengenezwa chocolate zilizofungwa na foil paper ya gold mithili ya coin ya Euro- guess where the cocoa to make the chocolate coins for that great and momentous ocassion came from........Kyela Tanzania. Tatizo tumekwishazoea vyetu kuwa ni vibovu kiasi ambacho hata tukiwa na kizuri sisi wenyewe tunakuwa wa kwanza kukidharau. Tubadilike. Nahisi hiyo chocolate haitakuwa ya bei ya kawaida kama viCadbury vilivyojaa kwenye visupa market vyetu! We can make it with the right leadership, with the audacity of hope and if we dare to dream.

    ReplyDelete
  18. huh!! hizi meseji stress imeshuka yani nimecheka kweli kuna wadau humu ndani ni ze komedi manake lazima ucheke tuu ukifungua hii blogu! yani mpiga box acha tu mbavu zangu weee

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...