Home
Unlabelled
kiongo ya maquiz du zaire
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Most read Swahili blog on earth
Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.
Asante sana kaka umenikumbusha nyumbani Mwanza, vijana wa jambo stars pale Mza hotel kila jmamosi walikuwa wanajitahidi kukidhi kiu yetu. Sijui kama bado wapo pale anayejua tafadhali anijulishe
ReplyDeleteWazee kama hawa wa kazi wana ujuzi na vyombo vya muziki.
ReplyDeleteKwa mfano, badala ya kushindana na rika la leo, yafaa wabadilishe genre ya muziki wao.
Watupigie muziki kama wa Jazz! Wangali na nfasi nzuri ya kushirikiana na wana-Jazz wa USA, Brazil, Ufaransa, Uingereza, Israel na hata Japan.
Wazee wanaweza sana kufurahia genre hii, ikiwa ni pamoja na kufanya mashindano, Sauti za Jazz (kama ya Sauti za Busara).
Wanaweza pia kuzidi kupanua wigo wa kupata pesa.
Born Again Pagan
ORCH.MAQUIS CO.LTD OMACO
ReplyDeleteKamanyola Bila Jasho
Concert hii ilikua tarehe 17.Okt.2008 Police Officers Mess Osterbay Mjini Dar-Es-Salaam.
Solo-Gitaa:Maestro Vumbi Dekula.
Rythm-Gitaa: Petit Pierre(Mangelepa)
Besi-Gitaa:Fariala Mbutu.
Keyboard:Geofrey Kumburu.
Drums:Chocho-Lee,Congas:Roy Mukuna.
Tarumbeta:Kanku Kelly.
Tenor Sax:King Maluu.
Alton Sax:Mafumu Bilali Bombenga
Waimbaji: Kasaloo Kyanga(mwenye nyekundu),Issa Nundu,Parash Mukumbule,Tshimanga Assosa pia alikuwepo Kasongo Mpinda clayton na Mwema Mujanga aka Mzee Chekecha(Rapa) enzi hizo Rap haijaingia Tanzania,kongo na Afrika.
MC ni Julius Nyaisangah wa TV &Radio One
KIONGO: ilitungwa nampiga Besi Banza Mchafu( marehenu).DVD ya Concert hii karibu itakua sokoni,wasiliana na Dekula kahanga email:dekula2@hotmail.com
Mdau Vumbi Dekula Sweden
Mdau hapa umeniweza sana kwa sababu hizi zilikuwa ndio enzi zangu, nakumbukuka nilikuwa Darasa la 4 nilikuwa ni mpenzi sana wa Makwizi, Sikinde Ngoma ya Ukae, na OSS Masantula bila Jasho. nilikuwa nikipenda vipindi vya. Chaguo la msikilizaji, Na mida ya jioni huwa nikimsubiri kwa hamu Julius nyaisanga katika Kipindi cha Matshushita. Anayejua anikumbushe wahusika walikuwa kina nani wakati huo.
ReplyDeleteMfundo Germany
Naaam, nyuzi bin nyuzi za wazee wazima, kila idara imekamilika.
ReplyDeleteTunataka sasa wazee wazima warudishe ushindani wa bendi na bendi, maanake miziki ya CD back-up ina-bore.
Kuangalia mtu akipuliza midomo ya bata,wapinga magitaa n.k huleta ladha fulani.
Mimi nilikuwa mdogo enzi za Maquiz lakini nawakubali mpaka sasa.
Tunafuatilia michuzi-effect katika kupromoti miziki yetu kwa karibu ktk Youtube, kwenye video hii ktk youtube sehemu iliyoandikwa statistics & data utapata dataz jinsi blogu ya jamii inavyopromoti hits(view) kwa clips zinazoletwa hapa.
ReplyDeletemdau
mfuatiliji wa kufufua muziki wa dansi.
ORCH.MAQUIS CO.LTD OMACO
ReplyDeleteKamanyola Bila Jasho
Concert hii ilikua tarehe 17.Okt.2008 Police Officers Mess Osterbay Mjini Dar-Es-Salaam.
Solo-Gitaa:Maestro Vumbi Dekula.
Rythm-Gitaa: Petit Pierre(Mangelepa)
Besi-Gitaa:Fariala Mbutu.
Keyboard:Geofrey Kumburu.
Drums:Chocho-Lee,Congas:Roy Mukuna.
Tarumbeta:Kanku Kelly.
Tenor Sax:King Maluu.
Alton Sax:Mafumu Bilali Bombenga
Waimbaji: Kasaloo Kyanga(mwenye nyekundu),Issa Nundu,Parash Mukumbule,Tshimanga Assosa pia alikuwepo Kasongo Mpinda clayton na Mwema Mujanga aka Mzee Chekecha(Rapa) enzi hizo Rap haijaingia Tanzania,kongo na Afrika.
MC ni Julius Nyaisangah wa TV &Radio One
KIONGO: ilitungwa nampiga Besi Banza Mchafu( marehenu).DVD ya Concert hii karibu itakua sokoni,wasiliana na Dekula kahanga email:dekula2@hotmail.com
Mdau Vumbi Dekula Sweden
Michuzi asante sana kwa hii, Dekula pia asante. Mnatukumbusha mbali, nyimbo zina hisia za kweli, zitungwa kwa visa vya kweli na kuimbwa kwa hisia halisia, tofauti na sasa, nyimba zinatungiwa pesa na kuwasilishwa kwa furahisha genge.
Nyimbo kama Kiongo ni kundi moja la nyimbo kama 'Maumivu Makali', 'Molema','Safari yetu Mbeya' etc. Mimi ni Mdau Pasco wa Jamiiforums au JF.
Uncle haya ndio mambo ya kutuleta.
ReplyDeleteMsema kweli mpenzi wa Mungu Louisa Mbutu na manywele yake feki au TID na Maquiz hawaoni ndani kwa mziki uliotulia kama huu.
Uncle usinibanie maana ndio zako hizo.