Mosinyoro Bahati akiwapaka majivu waamini wa Kanisa Katoliki la Chango’mbe wakati wa ibada ya kuanza kwaresma iliyofanyika katika kanisa hilo leo, ambayo ni Jumatano ya Majivu, siku ya mwanzo wa kipindi cha Kwaresma ambacho ni siku 40 za mfungo na kuomba toba miongoni mwa waumini wa Kikristo.

Siku hizo 40, huhitimishwa na Sikukuu ya Pasaka ambayo ni ya ufufuko wa Yesu Kristo, hiyo ni kwa mujibu wa Wakristo.

Jumatano ya Majivu hukusanya waaumini wengi ndani ya makanisa kwa ajili ya ibada ya majivu, japo si siku inayoadhimishwa kwa shangwe na nderemo kama ilivyo siku za Krismasi na Pasaka, ambazo hutawaliwa na shangwe zaidi.

Maadhimisho ya siku hii huwa ni ya kipekee na waamini huiadhimisha kwa namna ya kipekee pia, ambapo hufurika kwa kishindo ndani ya makanisa kwani wengi hawaiachi ipite bure bila kuhudhuria ibada na kupakwa majivu kwenye paji la uso.

Hata kwa baadhi ya waumini ambao ni nadra kwao kuhudhuria makanisani, hujitahidi kuhudhuria ibada ya Jumatano ya Majivu na kushiriki katika adhimisho hilo la kuanza kwa kipindi cha Kwaresma.

Kwa kusoma zaidi:
-------------------------------------
KWA NIABA YA WADAU WOTE GLOBU YA JAMII INAWATAKIA KWARESMA NJEMA WADAU WOTE WATAOFUNGA KATIKA SIKU HIZI 40 KUANZIA LEO.

-Michuzi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Tunakushukuru sana Mkuu wa wilaya na ankal wa blog ya jamii. Na mimi nakutakia Kwaresima njema pamoja na wadau wenzangu wote ktk blog yetu.

    ReplyDelete
  2. Asante sana Michuzi kwa kuwa mtu wa watu wote. Na sisi wakristu tutakukumbuka katika sala zetu wakati huuu wa kwaresma.

    ReplyDelete
  3. ankal kwa kupigia debe ukatoliki?! mbona sikukuu za waislamu huzielezei kwa undani??
    najua utabania maoani yangu kwani hupendi kukosolewa wewe!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...