dereva wa gari hili la utafiti wa simba katika hifadhi ya wanyama ya ngorongoro wikiendi hii lilikula mweleka hifadhini. bahati njema dereva alikuwa peke yake na alinusurika. mdau wa globu ya jamii aliyekuwa vekesheni huko alifika hapo muda mchache baada ya mzinga na kukuta dereva akiokota makabrasha yaliyotapakaa kila sehemu. inasemekana angeenda mbele mita tano tu a ngetumbukia kwenye bonde lililokuwa mbele yake. chanzo hakikuweza kufahamika


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. JAMANI KILA MTU NA FANI YAKE YAANI NAJIULIZA NINGEKUWA MIMI NINGESHUKA KWELI KUOKOTA MAKARABRASHA?, NADHANI NINGEJIBAKIA NDANI MPAKA WATU WATOKEE MAANA HUWEZI JUA AWEZA KUTOKEA SIMBA AKUGEUZE SOSEJI

    ReplyDelete
  2. hii style miti inataka kuchukua ufemasiiii naona ehh !

    ReplyDelete
  3. Hizi ajali nyingi za kujitakia...juzi kawe jamaa mwingine alipaki discovery kwenye mti

    ReplyDelete
  4. Naona siku hizi fashion kutundika gari mitini,..darajani kwa komba leo ngorongoro,..alafu ankal tafadhali fanya mpango ufanya mahojiano na jamaa aliyetundika ile range rover pale darajani kwa komba,...aeleze ilikuaje ile ajali balaaa...kama movie tena comedy.

    ReplyDelete
  5. Be careful with landrovers especially unapokuwa unaendesha jirani na miti.

    Nimeipenda hiyo style ya kupachika gari kwenye mti.

    ReplyDelete
  6. Baada ya watu kui-rate ile ajali ya Mbezi Darajani kuwa ni ya Mwaka jamaa alitaka kuvunja record ya yule wa Land-rover Discovery lakini hata nusu hakuweza... Ok lets wait more 2 come...

    ReplyDelete
  7. Mwaka mpya! style mpya ya ajali!

    ReplyDelete
  8. Hii sasa kali,
    Ankali naomba kuuliza swali. hizi picha zaajali dizainio hii huwa unazipataje. Unajua kwa wenzetu hizo zingekuwa "image of the year" yaani hizi ajali za namna hii hata huwezi sikitika bali inabidi ushangae na ukisoma maoni ya wananchi tena hapo unaangua na kicheko...hii ni kama simema hivi. Nimeangalia ile ya juzi tena nayo ni kituko...
    nawapongeza hawa wapiga hizi picha na nawapa "RED CARD" hawa madereva Uchwara....

    ReplyDelete
  9. Hii ajali imekaa kiaina yake. Gari kwa upande tunaouna inaonekana ipo intact. Muti pia ni mdogo lakini umekaa wima, ni vipi umeweza kuning'iniza hiyo gari at that angle, mupiga picha ni bora angetutumia picha kutokea upande mwingine.
    Kama hii picha siyo doctored kuna gazeti maarufu la magari huwa linachapisha picha za magari kwenye unusual situations. Hii inaweza ikapata angalau medali ya silver.

    ReplyDelete
  10. Mchezo tu wa kuigiza. Kama ile filamu inayoitwa "gods must be crazy"...!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...