historia ya JK Msoga
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, pamoja na Mama Salma Kikwete, jana, Jumatano, Machi 3, 2010, wamejiandikisha kama wapiga kura katika kijiji cha kwao cha Msoga, Wilaya ya Bagamoyo, Mkoa wa Pwani.
Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete waliwasili kwenye kituo cha kuandikisha wapiga kura cha Shule ya Msingi Msoga, kijiji cha Msoga, kiasi cha saa nne asubuhi, na kupokelewa na msimamizi wa kituo hicho, Ndugu Diana Frederick.
Kwenye uchaguzi mkuu uliopita wa mwaka 2005, Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete walipiga kura kwenye mji mdogo wa Chalinze wilaya hiyo hiyo ya Bagamoyo lakini zamu hii wameamua kujiandisha, ili waweze kupiga kura kijijini kwao.
Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wamejiandikisha katika kituo kipya kufuatia kuanza kwa zoezi la uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura kwa Kanda ya Mashariki.
Uboreshaji wa Daftari la Wapigaji Kura kwa Kanda ya Mashariki ulianza Jumatatu ya wiki hii, Machi Mosi, 2010, na umepangwa kumalizika keshokutwa, Machi 6, 2010.
Chini ya uboreshaji huo, wanaandikishwa wapigaji kura wapya, walioamua kubadilisha vituo vyao vya kupiga kura, ama waliopoteza shahada zao za kupigia kura.
Kufuatia hatua yake hiyo, Rais Kikwete amerudia tena wito wake kwa wananchi wenye sifa za kupiga kura kutumia nafasi ya uboreshaji wa daftari la wapiga kura kwa kujiandikisha kwa mara ya kwanza kama wapigaji kura, na kwa wale waliopoteza shahada zao kujiandikisha upya, ili wapate sifa za kutumia haki yao ya kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba, mwaka huu.
haaaa!!
ReplyDeletemimi nakumbuka niliandikishwa,sikujiandikia!mbona mwenye nchi ana andika mwenyewe?!na huu utaratibu wa mwenye ofisi kusimama na mteja kukaa unakuaje!?
hahahaaaaaaaaa anoy wa hapo juu 12:05:00pm comment yako imeniacha hoi sanaaa!!!
ReplyDeletemdau-Ukerewe
hivi mtu unajiandikisha mahali popote au pale unapoishi? maana huyu tawi lake na kila kitu huwa anaenda ile kata ya mchafukoge na ndo kituo chake cha kupigia kula, 2005 nilikuwa nakaa tabata sasa nimehamia sinza nitajiandikisha na sinza afu nipige kula sehemu zote
ReplyDeleteMhmm!12:05, protocal izo jamani,ila hapo chichemi kitu nchije nkapigwa nchale.
ReplyDeleteHuyu mKuu wa kijiji si anaishi Magogoni na 2005 akikuwa Mikocheni.....sasa hii inakuwaje?
ReplyDeleteBradha naweza kupata kontakts za huyo Msimamizi hapo?
ReplyDeleteMpeni kura Msoga
ReplyDeleteNi uelewa mdogo kwa wengi wetu. Nikifika Ikulu ofisi ni yake lakini akija kwangu mie ndo mwenyekiti, sasa dada kamwachia kiti wakati ndo haki yake. Mapokeo ya ujamaa na ukiritimba vigumu kufutika mpaka kitabu kiwapitie wote wajue haki yao
ReplyDeleteHuyo Mwandikishaji ni lazima kapitia mchujo mzito na kuambiwa cha kufanya pindi muheshimiwa akifika. Unatakiwa kusimama umpishe akae then ajiandikishe mwenyewe wewe kazi yako ni kuangalia tu.
ReplyDeleteEBU TULETEENI HIZO CLIPS ZA VIDEO NI NZURI SANA JAMANI EBU ENDELEENI KUTUNDIKA
ReplyDeleteJamani kama hapo ndio kijijini kwa mheshimiwa na amekuwa akienda kujiandikisha kwenye uchaguzi mara kadhaa mnategemea kweli sehemu nyingine za nchi yetu zitabadilike? Kama hata huwezi kupatengeneza kwako utawezaje kutengeneza kwa mwenzio!!?
ReplyDeleteHapa tumeliwa kwa kweli hata kashule ka maana? barabara, zahanati, maji safi?? au ndio usawa, kwamba hata na kijijini kwake hapapendelei? Jamani hamna hata comment moja imeongelea hilo swala ina maana tumeridhika au ndio tusehe wengine hiyo clip hamjaiona??
Mdau Ukonga
Kwa Mdau Ukonga (Fri Mar 05, 09:56:00 AM).
ReplyDeleteViongozi wetu wangekuwa na mtazamo kama wako, hali ingekuwa mbaya. Unataka shule iwe na vigae wakati kuna maeneo ambayo hayana hata shule. Maamuzi ya rasilimali gani iende wapi yanatakiwa yafanyike kwa kuzingatia uhitaji siyo NINATOKA WAPI.
Hivi watu kwa nini wanalilia hivi vyeo RAISI,WAZIRI MKUU,ni shida tupu JK kabla ya Urais au hata ile miaka miwili ya kwanza alikuwa anawakawaka handsome but now mnajionea wenyewe sasa akimaliza je?si bora ule kuku kwa mrija kama mimi hapa?
ReplyDeletehii si heshima yaani mbele ya raisi mwanamama anavaa kinyume na maadili,nilipokua cameraman bongo wakati nikirikodi raisi au mawaziri tu bsi hufatwa na maafisa wa usalama kuniambia vua cap au badilisha t-shir za kimarekani vaa nguo za heshima sasa mambo yamebadilika,Pili ingekua JK ni Raisi wa Zanzibar angejiandikisha mahala gani?maana kila siku yupo nje ya nchi na Zenji ukaazi ni miaka 5,naomba jibu wazee,michuzi niachie hii tu!
ReplyDelete