Meneja wa kilaji cha Kilimanjaro ambao ndio wadhamini wakuu wa Tanzania Music Awards, George Kavishe (pili shoto) akiwa na prezidaa wa Ngwasuma Nyoshi el Sadaat, King Kikii na Matei Super Minofu kwenye mnuso wa kumalizia semina elekezi ya wanamuziki iliyoandaliwa ili kuwekana sawa juu ya mchakato wa kupata wanamuziki bora wa 2009. Nyota kibao wa muziki walimiminika kwenye semina hiyo iliyofanyika ukumbi wa Paradise City hotel jijini Dar na wote waliridhika kwa jinsi mchakato huo shirikishi ulivyoandaliwa
furaha ilitawala nyota walikutana: hapa shoto ni Matonya akiwa
na Taasis Masela wa wazee wa masauti Akudo Impact.
Banza Stone mwana wa Masanja akiteta na Lwiza Mbuttu

Toka shoto ni Jay More, Mr. Ebbo na Hussein Machozi
Bwana mkubwa King Kikii akiwa na Banza Stone na Kalala jr (shoto)
Gwiji wa taarabu Sabah Muchacho (shoto)
akibadilishana mawazo na Ras Inno Nganyagwa na Bizman
Kila mtu alitaka picha na Bwana Mkubwa King Kikii. Toka shoto ni Mheshimiwa Temba, Banza Stone, Kalala jr, Wanne Star, Jose Mara na Profesa J wa Mitulinga
Mkurugenzi wa Masoko wa TBL David Minja (shoto, chini)
akila pozi na baadhi ya nyota wa muziki waliohudhuria semina hiyo

Picha ya pamoja ya baadhi ya wanamuziki hao
toka shoto ni Lwiza Mbuttu, Lady JD na Keisha.
anayekatiza nyuma yao ni Ras Nas
Mchanganyiko wa nyota wa muziki kwenye semina hiyo
Toka shoto ni Mwinyi, Lady JD, Fid Q, Jaffarai na Mchizi Mox
Ras Nas akila pozi na Masoud Kipanya aliyekuwa MC (shoto) na Nyoshi el Saadat
ankal akiwa na Bitchuka, Matei Minofu, Ras Nas na King Kikii
Ras Nas akiwa na AY na Inspekta Haroun (kati)
Nyota hao wakibugujika baada ya picha ya pamoja
George Kavishe akipozi na nyota hao
ni furaha, vicheko na maelewano kwa kwenda mbele





































Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. Kaka Michuzi,
    Mimi nina swali kidogo. Nimekuwa nikifuatilia sana hawa jamaa wa TBL wakitoa/wakidhamini matamasha, na kutoa ma-award kwa wanamuziki na wasanii kibao...Sasa nauliza ni lini watatupa hizo award sisi wanywaji wake ambao ndo tunawapa hela hao TBL, SBL?. Kwa mwaka mimi natuamia almost 1.3 milioni katika bia(wastani wa l12,000/= kwa mwezi)

    Ni swali la kizushi tuu

    ReplyDelete
  2. TBL huyo baba anaomba msaada hapo msaidieni.

    Huku ninakoishi kuna mfanyabiashara mmoja alikua natoa mchango wake kusaidia shule ya watoto hapo anapoishi. Shule ile ilikataa mchango wake kwa vile yeye ana duka la kuuza guns. Basi shule ile kukataa mchango ule publicity aliyopata ni kubwa kuliko hata ile angeipata kama wangekubali hela yake.

    Hivyo TBL mpeni hizo hela za pmbe zenu huyo mtu akikataa mtapata big publicity kuliko kuwapa hao mastar

    ReplyDelete
  3. JUMA NATURE mbona sijamuona apo?


    bwatuka.

    ReplyDelete
  4. Inspektar Haron nafikili ungebadilika kidogo si kila saa na kila sehemu na kila wakati basi wewe na nusu seruali tu!!! siku nyingine inapendeza ukiwa na suruali kamili.

    ReplyDelete
  5. Kwaniaba ya wanamuziki makini tunamiss sana mchango wa John Kitime. Hope huko uliko utatoa mchango wako hata kwa maandishi baada ya kupata semina elekezi kwa njia ya mtandao kama TBL watakuwa na ujasiri wa kukutumia.

    ReplyDelete
  6. huyu mwana fa si alisema hatohudhuria kili awards, imekuwaje tena yumo. hii kweli bongo flava

    ReplyDelete
  7. Jamani mimi nina swali au sijui niseme ushauri,hivi kweli wanamuziki wetu wanaelewa umuhimu wa kufanya mazoezi kwenye muziki? leo hii unamuona hivi kesho kavimba, naona karibia kila mwanamuziki kanenepa ukiachilia wachache kama Jide,Shaa etc, naomba niwaambie kwamba wanahitaji afya bora ili kuendeleza libeneke la uanamuziki. Na pia mwanamuziki anatakiwa kuwa na identity sio unavaa ovyo tu, nadhani watu waige mfano wa Shaa ni star wa kweli

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...