Tungo zao mara nyingi zimekuwa na tabia ya kugeuka na kuwa misemo ya mjini,gumzo la mitaani na hata kutumiwa “kibiashara” na makampuni kadhaa ya biashara. Bila shaka unakumbuka chanzo cha misemo kama vile Habari Ndio Hiyo,Nangoja Ageuke, Unaoa lini:Bado nipo nipo,Bed and Breakfast nk

Ni vijana ambao mpaka hivi sasa wanaweza kusema ‘wana mafanikio” fulani kutokana na kazi zao za muziki.Walianzia East Coast na mara kundi hilo lililokuwa na makazi yake pale Upanga-Dar-es-salaam,liliposambaratika wao wameendelea kuwa pamoja kama marafiki na pia wasanii wanaoshirikiana.

Tunawaongelea Mwana FA na A.Y ambaye siku chache zilizopita alipata tuzo ya Teenz kutoka nchini Kenya kama Favourite Artist wa East Africa. Safari hii wimbo unaitwa Usije Mjini. Kwanini nisije mjini wakati mjini nasikia ndio mambo yote? Kila mtu anataka kuja mjini.Mjini hata kwa kuuza maji tu unaweza kujipatia kipato.Mjini kuna starehe zote…inaaminika. Sasa kwanini A.Y na Mwana FA wanasema Usije Mjini? Sikiliza kwa makini tungo hizi;
Nenda kwa Globu kaka ya Jamii Bongo Celebrity

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Daa!
    Wimbo umetulia ile mbaya. Big up Mwana FA and AY kazi nzuri.

    Usije mjini kuna manyoya na wamasai wamewanyang'anya deal wamakonde huku mjini hawawindi Simba wanasuka dada zetu tu!Ni baadhi ya maneno ya wimbo huo, nimecheka sana.

    Mdau

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...