Mkurugenzi wa Biashara za wateja binafsi wa Benki ya Barclays, Manoj Anchan (kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa huduma mpya ya Premier Life iliyofanyika kwenye Hoteli ya Kempisk Dar es Salaam jana.Kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko wa Benki hiyo,David Lubira.
Mkurugenzi wa Biashara za wateja binafsi wa Benki ya Barclays,Manoj Anchan wa akizindua huduma mpya ya Premier Life kwa wateja wa Benki hiyo iliyofanyika kwenye Hoteli ya Kempisk Dar es Salaam jana.Waliokaa mezani kutoka kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Premier Life,William Mungai na Mkurugenzi wa Masoko wa Benki hiyo,David Lubira
Michuzi, mbona unakuwa hauwafanyii haki hawa jamaa wa Barclays? Nilitarajia kwa taaluma yako ya uandishi wa habari, angalau ungeeleza kwa ufupi hiyo huduma ya Premier Life ni nini hasa. Lakini kutuonesha picha za matukio peke yake, sidhani kama unatusaidia sisi wadau wako na pia hauwasaidii hao jamaa wa Barclays. Huu ni ushauri tu!!
ReplyDeleteMdau wa kwanza kabisa hapo juu ukiona hivyo ujue Michuzi na yeye katoka kapa, labda hajaelewa hiyo Premier Life ndio mdudu gani. Michuzi anajua Premier League bwana.
ReplyDeleteInatakiwa watu wa Barclays kupitia kwa PR Department yao watengeneze Press Release ambayo Michuzi atakachofanya ni kuibandika kama ilivyo. Siio wampe Michuzi kibarua cha ziada kuelewa Premier Life ndio mdudu gani. Akikosea je akaielezea ndivyo sivyo si atakuwa amewaharibia soko?