Waziri Mkuu nchini Uingereza Mh. Gordon Brown (pichani) atajiuluzu kuwa kiongozi wa Chama Cha Labour Party.

Mh. Brown ametangaza uamuzi huo baada ya Chama chake kushindwa kupata kura za kuongoza nchi katika uchaguzi uliofanyika Alhamisi.

Uchaguzi huo uliwafanya wananchi wa Uingereza kushindwa kuamua chama ambacho kitaweza kuwaongoza baada ya vyama vyote kushindwa kufikia viti 326 vinavyowezesha kuiongoza nchi.

Mh. Brown ataendelea kuingoza nchi na kuwa kiongozi wa chama hicho mpaka atakapopatikana kiongozi mwingine wa kukiongoza chama na Serikali.

Akizungumzia kuhusu masuala ya serikali ya nchi amesema kwamba shughuli zote za kiserikali zinaendelea kama kawaida.

Wakati huohuo chama cha Labour Party na Liberal Democrats vinakutana kujadili mwelekeo wa kuweza kuungana na kuunda serikali ya kuingoza nchi.

Ally Muhdin
wa
habari kamili

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 10, 2010

    Siyo kweli wananchi wa Uingereza wameshindwa kuchagua chama wanachokipenda.

    Matokeo rasmi ya uchaguzi na viti vyama walivyonyakua ktk mabano:
    Conservative 306
    Labour 258
    Liberal 57
    vyama vingine 28

    Sheria ya Uingereza ili chama kiweze kutambulikana kama chama kinachoongoza serikali lazima kipate angalau viti vya ubunge 326.

    Ikiwa hakuna chama kilichopata viti hivyo, basi itabidi vyama viwili au zaidi viendeshe serikali ya mseto itakayokuwa na viti angalau 326, ili kuwezesha serikali kupitisha miswada na sheria kwa wingi wa kura 'majority'.

    Majority hiyo hupatikana kwa chama kuwa na viti 326 au kwa mseto wa vyama kuwa na viti angalau 326.

    Kifupi sheria ndiyo imevibana vyama, lakini watu wanajua vyama vipi vinakubalika na wananchi wa Uingereza.

    ReplyDelete
  2. hawa viongozi wa vyama vitatu wangejifunza kama yale yaliyotokea Kenya na Zimbabwe haya ni makoloni yao na walikua wakishabikia hivi vyama kuungana kama vile haitoshi walitishia vikwazo kama wasinge ungana je! wao watatishwa na nani? kizungumkuti hicho baba.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 11, 2010

    Maana ya kushindwa ni kutokuwa na msimamo wa kuchagua chama gani kiweze kuwaongoza siyo kupiga kura.

    Wananchi wote wanajua kama viti vingapi vinatakiwa ili chama kiweze kuongoza nchi lakini wamegawanyika katika msimo na maamuzi yao. hiyo ndiyo sababu ya kushindwa kuchagua chama cha kuwaongoza.

    Ikiwa kama Labour Party imeweza kuongoza nchi tangu miaka 13 iliyopita kwanini wasiendelee kukichagua hicho chama?

    Wameamua kufanya mabadiliko ya kuchagua chama cha Conservative lakini mabadiliko hayo hayakuwa na nguvu.

    Kama umefuatilia uchaguzi Wanachi wa Barking na Dagenham kwanini walijitokeza kwawingi kwenda kupiga kura? ni jimbo ambalo liliongoza nchi nzima kwa kuwa na wapiga kura wengi katika uchaguzi huo. Sababu walichoka na sera za ubaguzi ambazo chama cha BNP zilionyesha kwenye kampeni zake

    Chama cha BNP kilishindwa vibaya sana na kupokonywa uongozi wote uliokuwa maana walikuwa na wawakilishi 13 katika jimbo hilo NA WOTE WALISHINDWA.

    ELEWA MAANA YA KUSHINDWA NI KUTOKUWA NA MSIMAMO WA CHAMA GANI WANATAKA KIWAONGOZE MAANA WANGEPENDA CHAMA KIMOJA KATI YA HIVYO BASI KINGESHINDA BILA MATATIZO NA SIYO KAMA HALI ILIVYO HIVI SASA.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...