Mwanamziki mkongwe wa mziki wa dansi nchini toka nchini Kongo Kinshasa, Fredy Mayaula Mayoni (RIP) amefariki dunia siku ya 27-05-2010 huko jijini Brussels, Ubeligiji, kwa ugonjwa kansa ya ubongo (brain trumour).

Marehem Mayaula Mayoni (64) ni mwanamziki aliyekulia na kusomea jijini Dar wakati wa utoto wake miaka ya 60s, kwani baba yake alikuwa ni moja wanadiplomasia katika ubalozi wa Kongo(Zaire) nchini Tanzania. Marehem pia aliwahi kucheza kandanda katika timu maarufu nchini Yanga(Young Africa) ya jijini Dar.

Vijana wa kizamani watamkumbuka marehemu Mayaula pale alipojiunga na bendi ya TP OK Jazz,iliyokuwa inaongozwa na gwiji Franco Luambo Makiadi, uko Kongo. Mayaula alijiunga TP OK Jazz baada ya kurudi kwao Kongo (DRC) na kujikita katika ulimwengu wa mziki ,ambako aliachia wimbo maarufu "Cherie Bondowe" au "Sherry bondowe", wimbo ambao ulimpa umaarufu sana.marehemu pia aliwahi kufanya kazi na mwanamziki ambaye pia marehemu Mpongo Love.

Mungu amlaze pema peponi Mayaula Mayoni
Amin

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 27, 2010

    May the Lord Our God Shine His (God's) Eternal Light Upon Him, and May He (Deceased) Rest in Peace. Amen.

    A Loss is a Loss, but, WHAT A LOSS!

    His (Deceased's) Legacy will live on, definitely.

    Amen.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 27, 2010

    Mayaula Mayoni(RIP)mungu akaulaze mahala pema peponi.
    Ankal misupu asante kwa taharifa hizi za kusikitisha.naukumbuka wimbo wa Sherry bondoe,wimbo ambao nikiusikiliza unanikumbusha ujanani,na wakati kilo ya sukari sent 80,ambapo dar maisha yalikuwa poa.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 27, 2010

    Rest in Peace,we are all in the same way.Amen

    Mjusi

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 27, 2010

    Ankal Michuzi,

    Najua wewe ni Bingwa wa kubana maoni Africa Mashariki na Kati. Hii pia naomba usiirushe hewani, ni kwa taarifa tu.

    Kuna maoni nimetuma hapo kuhusu, WHAT A LOSS! sawa, sikumaanisha kumlenga mtu yeyote yule zaidi ya wale watu wangu waleee.

    Hivyo waambie wadau wa Sherry I Love You, Sherry na Motema ee; wasijishitukie. Shukran.

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 27, 2010

    Mungu akulaze pema Mayaula,utakumbukwa kwa yale ulioyafanya.
    Yanga Imara

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 27, 2010

    Rest in Peace MAYAULA, u'll be remembered much! Your time @ youn african fc, and the unforgetable music of your own creation! Bwana ametoa na bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe!

    ReplyDelete
  7. shaibu mwambunguMay 28, 2010

    Kembaseke nzela ya moto nyoso(kaburi ndio njia ya watu wote) mungu amlaze mahali pema Mayaula Shemeji yetu huyo kwa akina Ted Amri -Mwambungu Mbinga,Ruvuma.

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 28, 2010

    Mayaula ingawa ulikuwa mkongo lakini wewe ni mtanzania, u r one of us, RIP, we love u.

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 28, 2010

    Oh Mayaula Mayoni tulifurahia mno nyimbo zako lakini tunakuombea heri Mungu akulaze pema peponi. Amen

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 28, 2010

    RIP Brother. You will be missed.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...