Mzee Pwagu enzi za uhai wake


HABARI ZILIZOIFIKIA GLOBU YA JAMII HIVI PUNDE TOKA HOSPITALI YA MWANANYAMALA JIJINI DAR, ZINASEMA KWAMBA MUASISI WA SANAA YA UIGIZAJI NCHINI, MZEE RAJABU HATIA A.K.A PWAGU AMEFARIKI DUNIA JIONI HII MAJIRA YA SAA KUMI KATIKA HOSPITALI YA MWANANYAMALA JIJINI DAR ALIKOKUWA AMELAZWA KWA MARADHI YALIYOKUWA YAKIMSUMBUA KWA MUDA MREFU.

MZEE PWAGU NDIYE MUASISI KUNDI LA SANAA KAOLE GROUP AMBAYO IMETOA WASANII WENGI SANA MPAKA SASA, WAKIWEMO RAY, KANUMBA NA CLAUDE. ALITAMBA SANA KATIKA KIPINDI CHA PWAGU NA PWAGUZI CHA RTD ENZI HIZO AKISHIRIKIANA NA MAREHEMU ALLY KETTO.

MAZISHI YANATARAJIWA KUFANYIKA KESHO KWENYE MAKABURI YA KIGOGO JIJINI DAR. MSIBA UPO NYUMBANI KWAKE HAPO HAPO KIGOGO KARIBU NA ROUND-ABOUT YA KIGOGO NA MAGIMENI.

TIMU NZIMA YA GLOBU YA JAMII TUNAMUOMBEA KWA MUNGU AIWEKE ROHO YA MZEE PWAGU MAHALA PEMA PEPONI. SISI TULIMPENDA LAKINI MOLA ALIMPENDA ZAIDI....

-AMIN
------------------------------
HABARI ZAIDI ZA MZEE PWAGU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 28, 2010

    R.I.P naona hata wakina zekomedi waliiga kidogo kutoka kwake

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 28, 2010

    pole sana wafiwa namkumkuba sana huyu mzee.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 28, 2010

    Upumzike kwa amani Mzee wetu Pwagu. Asante kwa kutuburudisha. Tutakukumbuka milele. Poleni sana familia ya mzee Pwagu.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 28, 2010

    Kwanza Shukrani sana bro Michu kwa habari hii. Hiki kifo kimenigusa sana kwani mzee pwagu ni kama mzee we2 pale Kigogo Mbuyuni mpaka Kigogo CCM. Mzee ambae anajulikana sana, mkalimu na msaidiaji wa jamii kwa lolote.

    Kigogo Boi

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 28, 2010

    ama kweli kamichu thanks na pole manake mzee pwagu kusikia habari zake nimesikitishwa sana ila umenikumbusha nyumbani kweli kweli nikikumbuka radio tanzania walivyokuwa wanaweka kipindi cha pwagu na yule mwenzie nimemsahau jina ila ndio mungu kapenda.

    R.I.P Pwagu sote twaelekea huko.

    Poleni familia nzima ya pwagu, kwakweli hawa ndio maselebrity tunaopenda kuwasikia hawana makuu na wanafanya kazi zao kimapenzi, si kwa pesa wala si kwa kujulikana, pwagu kwa kweli kipaji chako hakitapatikana tena bongo siku hizi watu wanaweka pesa mbele, ila mfano wako ni utang'aa milele. asante kwa yote.

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 28, 2010

    Nimepokea habari hii kwa masikitiko makubwa sana. Kifo cahake ni pengo kubwa sana katika tasnia ya sanaa nchini Tanzania. Mungu aiweke roho yake mahala pema peponi AMEN.


    Mpg bx

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 28, 2010

    inalillah wainaillahi rajiun. Inshallah Allah amsamehe dhambi zake.

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 28, 2010

    Duh, rest in peace mzee wetu.

    huyu mzee kwa kweli enzi za utoto wangu alinifanya nisikae mbali na redio siku ya kipindi cha "pwagu na pwaguzi".

    ni msiba kwa kweli!

    mdau- amsterdam

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 28, 2010

    Pumzika kwa amani kiongozi, tutakukumbuka kwa mchango wako katika tasnia ya sanaa nchini, ulikuwa chachu muhimu sana. Sitasahau utangulizi wako na Pwaguzi katika kipindi cha mama na mwana Radio Tanzania enzi zile..."mahokaaaaa!" Japo hadi leo sijajua maana yake :-0

    Pole sana kwa familia, ndungu, jamaa, marafiki na jamii nzima ya Watanzania kwa msiba wa nguli huyu.
    Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi, Amina.

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 28, 2010

    INNA LILLAHI WAINNA ILAIHI RAAJIUN.
    kila kilichoumbwa kitakufa 2 kitake
    kisitake,wewe,mm,yule na vyote vitaondoka isipokuwa MUUMBA 2.
    2JIANDAE VEMA DUNIA ISHAKWISHA HIII
    2PO WAUNGWANA ???????????????????????

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 28, 2010

    inna lillahi waina illahi rajiun, rahman atiye peponi awe miongoni mwa waja wa peponi. Allah ma amin.

    mdau new york

    ReplyDelete
  12. Mdau K.VMay 28, 2010

    So sad... may his soul rest in peace.

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 28, 2010

    R.I.P mzee wetu,umetungalia mbele ya haki.
    Napenda kutoa pole kwa ndugu,jamaa,majirani na wale wote wanaoguswa na msiba huu. Mwenyezi mungu awape nguvu katika kipindi cha msiba.

    Amen

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 29, 2010

    RIP Sir. Kipaji chako kiligusa maisha ya wengi.
    Poleni ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu popote pale mlipo.

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 29, 2010

    RIP

    natumaini jina lake litawekwa kwenye vitabu vya sanaa pia

    Huyu alitufurahisha wengi tukiwa wadogo.. pwagu na pwaguzi

    ReplyDelete
  16. AnonymousMay 29, 2010

    NIMEPOKEA KWA MAJONZI MAKUBWA KIFO CHA MZEE WETU PWAGU NAANDIKA HII COMMENT HUKU MACHOZI YANANITOKA

    KINACHOFANYA MACHOZI YANITOKE NI KUMBUKUMBU KUBWA YA MZEE PWAGU NA MWENZIE PWAGUZI KATIKA VIPINDI VYAO RTD

    NIKIKUMBUKA MAJIRA YA USIKU USIKU BAADA YA KUPATA CHAKULA CHA JIONI KULE KIJIJINI KWETU AMBAPO HATUKUWA NA UMEME KWENYE NYUMBA YETU

    ILIKUWA NI KIRADIO CHA MBAO KINACHOJULIKANA KWA JINA LA 2 77 CHA KUTUMIA BETRI

    ILIKUWA KILA SIKU IKIFIKA MAJIRA HAYO LAZIMA TUSOGELEE RADIO YETU TUNAKUWA KIKUNDI TAKRIBANI MTAA MZIMA TUNAKAZUNGUKA KARADIO KUPATA UHONDO WA KIPINDI CHA MZEE PWAGU

    POLENI SANA WANA FAMILIA NA NAWATAKIA UVUMILIVU KATIKA KIPINDI HICHI KIGUMU

    MSIBA WA MZEE PWAGU NI MZIBA WA WATANZANIA WOTE KWA UJUMLA

    WAZEE KAMA HAO WANAPASWA KUKUMBUKWA KWA MCHANGO WAO KATIKA JAMII KWANI KILA ALIETAKA KICHEKESHO ENZI HIZO HANA BUDI KUSIKILIZA KIPINDI CHA PWAGU NA PWAGUZI

    MUNGU AKULAZE PEMA PEPONI MZEE WETU PWAGU DAIMA TUTAKUKUMBUKA MBELE YAKO NYUMA YETU

    RADIO ZA TANZANIA NA TV ZINAPASWA KUWEKA VIPINDI VYA MZEE PWAGU KATIKA WIKI HII YA MSIBA WAKE ILI KUMUENZI

    mdau wa mahakama kuu ya dunia nipo kwenye huzuni na majonzi makubwa

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 29, 2010

    inna lillahi wainna ilaihi raji'un.kila nafsi itaonja maut,mwenyezi akulaze mahala pema peponi amin.pwagu na pwaguzi was entertainment for a lot of us who did not own a tv.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...