A four years Ugandan pupil Christina Kwezi hands over a bouquet of flowers to President Jakaya Kikwete shortly after he arrived at Entebbe international airport this evening.President Kikwete is Uganda to attend the International Criminal Court(ICC) Review Conference.
President Jakaya Mrisho Kikwete inspects a guard of honour mounted by the Uganda's People Defence Force shortly after he arrived at Entebbe Airport in Uganda to attend the International Criminal Court Review conference.
Buganda Traditional royal Dancers entertains President Jakaya kikwete and his delegation shortly after he arrived at Entebbe airport this evening to attend the ICC Review Conference(photos by Freddy Maro)
---------------------------------------------------------------
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameondoka nchini jioni ya leo, Mei 30, 2010, kwenda Kampala, Uganda, kuhudhuria Mkutano wa Kwanza wa Nchi Wanachama wa Mkataba Ulioanzisha Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC).

Rais Kikwete anahudhuria Mkutano huo kwa mwaliko wa
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Mheshimiwa Ban Ki Moon.

Mkutano huo unaoanza kesho, Jumatatu, Mei 31, 2010, miongoni mwa mambo mengine utapitia na kufanya marekebisho katika Mkataba ulioanzisha ICC.

Mkutano huo unatarajiwa kumalizika Juni 11, 2010, lakini Rais Kikwete anatarajiwa kurejea nyumbani keshokutwa, Juni Mosi, 2010.

Aidha, mkutano huo unatarajiwa kupitia orodha ya makosa manne yanayoorodheshwa chini ya Mamlaka ya ICC kwa lengo la kuongeza ama kuyatolea ufafanuzi zaidi makosa hayo.

ICC ina Mamlaka ya kuhukumu makosa manne ambayo ni Mauaji ya Kimbari (Genocide), Makosa Yafanyikayo Wakati wa Vita (War Crimes), Makosa Dhidi ya Binadamu (Crimes Against Humanity) na Uchokozi ama Ushari (Aggression), kosa ambalo halijapata tafsiri inayokubalika kimataifa katika Mkataba huo wa Roma

Mkutano pia utafanya tathmini ya shughuli za Mahakama hiyo tangu ilipoanzishwa Agosti, 1998, mjini Roma, Italia na kupendekeza namna ya kuboresha shughuli hizo.
Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi.
Ikulu-Dar Es Salaam
Mei 30, 2010

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 31, 2010

    Uniform ya askari wao na jinsi walivyojipanga bila kubanana inaonesha kuwa jesi lao liko makini zaidi

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 31, 2010

    International Criminal Court Review Conference. Are they (politicians) lawyers?

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 31, 2010

    this is official engegment why our president is not wearing proper suit

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 31, 2010

    A four years old.......sio right just to say a four years....a four years what relationship, colege, school, vision etc etc

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 01, 2010

    Afrika mitindo ya wakubwa kuimbiwa nyimbo za kuwasifu haiishi? Kwa mtindo huo wangapi wanapoteza muda wa kazi zao na kuishia kusubiri wakubwa watue uwanja wa ndege masaa kadhaa na kujipanga barabarani kuwashabikia.
    Tufikiria mambo kiuchumi na hayo yanayotendeke yanaathiri vipi uchumi wa matiafa ya kiafrika.
    Wangapi wanaacha kazi ofisini. viwandani, mama ntilie, machinga nk kwenda kuwalaki wakuu waliotoka kutumia mapato ya walipa kodi?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...