Tume ya Uchaguzi imetangaza kuwa leo na kesho ni siku za kujiandikisha kwa wananchi katika daftari la kudumu la wapiga kura. Kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi, muda huu wa siku mbili umeongezwa ili...

Tume ya Uchaguzi imetangaza kuwa leo na kesho ni siku za kujiandikisha kwa wananchi katika daftari la kudumu la wapiga kura.

Kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi, muda huu wa siku mbili umeongezwa ili wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waliokosa fursa hiyo waweze kufanya hivyo.

Hii ni nafasi yako mdau kushiriki katika zoezi hili muhimu katika kuchagua viongozi imara kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Natoa rai kwa wakazi wa Dar es Salaam ambao hawana kadi za wapiga kura waende kwenye vituo na kujiandikisha. Mchango wako katika kuchagua viongozi bora unaanzia kwako.
Mdau wa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 22, 2010

    Je kutakuwa na nafasi nyingine ya kujiandikisha? Kuna utaratibu gani wa Watanzania walioko nje ya nchi kujiandikisha?

    ReplyDelete
  2. Yah nami pia nimeguswa na hilo maana nategemea kurudi home baada ya miezi mne hivyo nitakua nimepoteza haki yangu ya kujiandikisha?

    Braza Mvano

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 22, 2010

    kwa tulioko nje ya Tz hakuna kuvote jamani??? na km sintakuwa na kadi this year inabidi nisubiri tena hadi uchaguzi mwingine ndo nijiandikish nipate kadi!! ama sio wadau.Hii inakuwaje?

    ReplyDelete
  4. "It's not the people who vote that count. It's the people who count the votes." (Josef Stalin)

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...