Na Ripota wa Globu ya Jamii, Shangai
Leo ni siku ya maadhimisho ya siku ya Mawasiliano Jamii Habari Duniani, nchi zote duniani zinaadhimisha siku hii muhimu kwa maendeleo ya dunia yetu kwa shughuli mbalimbali, ikiwemo maonesho na makongamano yaliyojikita katika kujadili kauli mbiu ya maadhimisho ya Mwaka huu, "Miji Bora, Maisha Bora na TEKNOHAMA".
Maadhimisho haya yanafanyika kimataifa katika jiji la Shanghai ambako kuna maonesho makubwa ya kuadhimisha kauli mbiu ya mwaka huu kwa vitendo katika kila sekta, yenye lengo la kuonesha umuhimu wa kuwa na miji na makazi bora katika kuboresha maisha ya watu duniani.
Kauli mbiu ya mwaka huu, hususani kwa sekta ya Mawasiliano, inakusudia kutoa changamoto katika kuhakikisha serikali mbalimbali duniani zinajipanga kuwaletea wananchi wake maendeleo kwa kupanga na kujenga miji bora ili kuboresha maisha.Tanzania haiwezi kubaki kama kisiwa, ni muhimu tuimarishe matumizi ya TEKNOHAMA katika shughuli zetu zote za maendeleo hsusani katika kupanga miji yetu na matumizi mazuri ya TEKNOHAMA kwa maendeleo ya Taifa letu.
Jana jioni katika dhifa ya kitaifa ya kukaribisha siku ya maadhimisho haya, Katibu Mkuu wa ITU (International Telecommunications Union) Dr. Hamadou Toure alitaka dunia kuangalia kwa makini umuhimu wa kutumia TEKNOHAMA katika kuboresha miji duniani ili kuwa na maisha bora. Taarifa Maalumu ya Katibu Mkuu huyo inafuatia hapa chini.
For TCRA's Statement to mark the day
CLICK HERE
ankal nimeona atiko yako na nyingine, una KIngereza cha Oxford halafu hapa kwenye blogi unatuzuga english not richebo.
ReplyDelete(US Blogger)