Ankal,
Naomba wajuzi wa sheria wanijuze juu sheria ya kazi ya Tanzania inavyosema juu ya mfanyakazi anaeumia kazini au kuugua muda mrefe pasi kufanya kazi! Compensation zake zikoje na ni wajibu wa nani mifuko ya hifadhi like NSSF au muajiri? Nataka kusaini mkataba wa kazi lakini swala hili silielewi kidogo.
Many thanks
Mdau Edwin
Naomba wajuzi wa sheria wanijuze juu sheria ya kazi ya Tanzania inavyosema juu ya mfanyakazi anaeumia kazini au kuugua muda mrefe pasi kufanya kazi! Compensation zake zikoje na ni wajibu wa nani mifuko ya hifadhi like NSSF au muajiri? Nataka kusaini mkataba wa kazi lakini swala hili silielewi kidogo.
Many thanks
Mdau Edwin
bongo sheria zipo ila zipo kwenye vitabu tu , we ingia huo mkataba ufie kazini....
ReplyDeleteunacheza na bongo
uliza kwanini inaitwa bongo ?
Nakushauri umuulize muajiri wako mtarajiwa, kwani naamini sera zinatofautiana kutoka kampuni moja hadi nyingine. Wengine ukiugua unafutwa kazi (na bosi wala haji kukujulia hali) na wengine (kama kampuni ya Athumani mpiga picha) ukiugua wanathamini jinsi unavyohitaji msaada na hivyo hawakutupi. Ongea na wafanyakazi wa hiyo kampuni kama ni ngumu kumuuliza muajiri. Usiangalie sana sheria ya nchi, watekelezaji wananunulika na mabosi.
ReplyDeleteWewe umepata kazi tena Bongo halafu unaanza kuulizia masuala ya kuumwa au kuumia kazini.
ReplyDeleteMtu wangu wewe ingia kazini na sign mkataba. Kwa vyoyote vile kama alivyosema jamaa hapo juu kwamba likitokea tatizo kama hilo basi tena inabidi tu ushukuru Mungu kwani watekelezaji wa sheria wanakula sahani moja na boss wako.
Piga mzigo jibaba, kazi njema.
Kuna ofisi za serikali pale UWT na Morogoro Road, Junction. Nilipofunga biashara yangu miaka ya nyuma niliwachukua wafanyakazi na kwenda nao huko ili wajue haki zao. Ni ofisi zinazohusika na haki za wafanyakazi. Niliambiwa kama sikosei kama mgonjwa basi alipwe kama kawaida (mmoja wa wafanyakazi alikuwa mgonjwa muda mrefu). Ni mshahara wa mwezi mmoja kwa kila mwaka aliyofanya kazi. Pili, alipwe nauli ya kwenda nyumbani. Ni hayo tu. Nikamlipia gharama za hospitali ingawa sihitajiki kulipa. Muhimu ni kwa mfanyakazi kulipiwa pensheni (NPF) kila mwezi ili aweze kupata pesa akimaliza kazi. Bado serikali haina program yoyote ya kumsaidia mfanyakazi ambae anaumwa ghafla na kupoteza mshahara. (unemployment benefits).
ReplyDeletewatakiwa kutumia akili yako na kama ulivyo andikishiana mkataba na mwajiri wako. alafu Shshshshwaaaaaaaa kama mbayuwayu
ReplyDelete